JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Waziri Silaa ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 13, 2025 jijini Arusha.
“Nia ya Mheshimiwa Rais ni kuona bunifu za startups zinasaidiwa na zinaweza kuvuka mipaka,” alisema Waziri Slaa.
Ameongeza kuwa, ni jukumu la Serikali kuhakikisha bunifu za kampuni changa (startups) zinaweza kufikia malengo.
“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amezindua Mkakati wa Uchumi wa Kidijitali wa mwaka 2024-2034 wenye nguzo sita, ambapo moja ya nguzo hizo ni kuhakikisha kuwa vijana hawa wanakuwa na maendeleo katika maeneo yao ya ubunifu”, amesisitiza Waziri Silaa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA, Dkt. Nkundwe Mwasaga, aliwasihi vijana waliohudhuria mkutano huo kuomba nafasi za ufadhili wa masomo zinazotangazwa na Tume hiyo ili kuongeza ujuzi na kufanikisha malengo yao.
Dkt. Pamela Chogo, mdau wa startups, pia alishukuru Serikali kwa kuanza mchakato wa kuunda sera ya kampuni changa, akisema ni hatua jumuishi na wazi.