Mchambuzi Mbwaduke, Kila mchezaji anamsifia, hajawahi kukosoa

ubarinolutu

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
2,424
Reaction score
4,954
Huyu ramadhani Mbwaduke ni moja kati ya wachambuzi waliojipatia sifa katika uchambuzi hasa eneo la takwimu.

Mchambuzi huyu ni mzuri lakini ana mapungufu makubwa mno, kwanza hataki kabisa kuonekana ni shabiki wa timu Gani, japo Mimi najua. Na uchambuzi wake umejikita fair kabisa.

Kutokana na kutafuta views na kutaka kukubalika na timu zote Tanzania, mchambuzi huyu Mbwaduke anatumia staili ya Unafiki, na Kila mchezaji anayemchambua Huwa anamsifia tu na kutoa takwimu chanya.

Yaani huyu Kila mchezaji kwake ni Mzuri, mchezaji alifanya makosa anamtetea, huyu jamaa ni tofauti na wachambuzi wengine. Hapondi kabisa hata kama beki akijifunga atamtetea.

Lakini naamini atapata mashabiki wa timu zote
 
Ulitakaje sasa mkuu? Kila mtu ni bora, ubora ukiwa chini ya kiwango tunaita ubovu...

Aanatumia tafsida. Anakuachia kazi hiyo wewe kujaza mabox hewa kuwajua hao wabovu. Tumia mpishano wa takwimu kumjua mchezaji kilaza
 
Mbwaduke anakuja na takwimu, wewe umekuja na uji(sio uzi)
Mbwaduke ababaishi, nilimkubali siku tulipocheza na Wydady kule kwao. Siku iyo katika uchambuzi wake alizungumza kabisa kuwa Simba wanawaweza hao Waarabu, ila alitahadharisha Simba kuwa makini na mipira ya kutengwa sababu hao Waarabu wakiruka huwa wanampasia mtu wa nyuma ambae ndie anayeweza kufunga
Na hicho ndicho tokea ktk hiyo mechi ktk dakika za lala salama
 
huwa najiuliza timu zetu hizi kwann hawawezi kucheza mipira ya juu ka waarabu nakosa majibu.
 
Kapata umaarufu uzeeni,sijui ujanani alikuwa jalala la wapi huyu mbwaduke
 
Isije tu ikawa umeingiwa na wivu. Nimeona nitoe tu tahadhari mapema. Maana nwisho wa siku unaweza kujikuta umekuwa mchawi.
 
Jemedari akiwaponda mnamuita wamchongo,
Kuna mahala mnakwama wabongo
 
[emoji23][emoji23][emoji23]had sasa umepata majibu
 
Kwani kukosoa ni lazima? yaani wabongo mshazoea sana shida kiasi kwamba kuambiwa mazuri hamtaki kabisa.
 
Reactions: NYS
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…