Mchangiaji maarufu Radio One na ambaye pia ni Mganga achafua hali ya hewa

Mchangiaji maarufu Radio One na ambaye pia ni Mganga achafua hali ya hewa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Ilikuwa ni jana katika Kipindi kizuri kabisa cha kila Jumapili cha Familia ambacho hurushwa na Kituo cha Super Brand nchini Radio One kuanzia Saa 1 na nusu hadi Saa 4 kamili asubuhi pale ambapo ' mchangiaji ' mmoja ambaye ni ' maarufu ' mno lakini pia ni Mganga wa Kienyeji aitwae Fundi Shomari alipokuwa na ' taarifa ' ambayo kiukweli imechafua kabisa hali ya hewa katika Familia nyingi sana hapa Tanzania tokea jana.

Mada iliyokuwepo jana ilikuwa ni kwanini siku hizi Wapenzi / Wanandoa hawaaminiani hata kidogo katika Mahusiano yao? Wapo Watu wengi waliochangia kama kawaida akina Mama Manka, Mama Abuu wa ukweli na wengineno ila huyu mchangiaji maarufu na Mganga aitwae Fundi Shomari ndiyo alimaliza shughuli yote.

Fundi Shomari alisema kuwa kutokana na ' Utaalam ' wake wa masuala ya Uganga na pia ameshafanya ' tafiti ' zake kwa muda mrefu tu ameamua ' kupasua ' ukweli wake na kutoa ' Siri ' kwa kusema kuwa nanukuu " Kaka Abdallah Mwaipaya na Dada Farhia Middle amini msiamini katika Familia zote zenye Watoto zaidi ya mmoja pale Mtoto halali wa Yule Mwanaume / Mume pale ndani ni yule tu wa Kwanza ila wale waliofuata 99% huyo Mwanaume / Mume amezalishiwa na Mwanaume mwenzake " mwisho wa kumnukuu.

Alipoulizwa nini sababu Fundi Shomari alisema kuwa Kikawaida na kwa Saikolojia ya Wanawake ni kwamba Wanawake wengi hupenda kuwa na Mahusiano mapya kila baada ya miezi mitatu au sita ya Mahusioano yao na kwamba Wanawake huwa ni wepesi sana Kuwakinai Wapenzi wao huku wakiwahisi kuwa labda ni Kaka zao hali ambayo huwafanya kutoka nje kupata Mapenzi / Mahaba mapya.

Binafsi Fundi Shomari tokea jana kanifanya Chakula chochote kile kisiweze kuingia katika Tumbo langu na muda wote tokea jana hadi hivi naandika huu uzi nimekuwa ' mpweke ' mno kutokana na ukweli kwamba nina Wake Watatu halafu wote nimewazalisha Watoto Wanne Wanne hivyo kwa maelezo ya Fundi Shomari ni kwamba hapo GENTAMYCINE Watoto wake halali ni Watatu tu na waliobaki wote Tisa ' nimechapiwa '.

Hapa jirani tu nina Mzee mmoja wa Kigogo Yeye ana wake zake Wawili tu ila wote wawili hao amewazalisha Vikosi viwili vya Simba na Yanga ( namaanisha ana Watoto 22 ) hivyo kwa ' Mahesabu ' ya haraka tu na kwa mujibu wa Fundi Shomari ni kwamba huyu ' Mgogo ' jirani yangu Watoto wake halali ni Wawili tu na hao wengine 20 analea ' mabao ' ya Wenzake tu.

Tokea jana hadi leo ' mood ' yangu haipo kabisa baada ya kumsikia jana Fundi Shomari akitiririka na kuserereka vile ndani ya Kituo Super Brand kabisa Afrika ya Mashariki cha Radio One. Haya wale wenzangu na mie tulio na Watoto Timu za Mpira hebu karibuni hapa tuweze kujadili hili je Fundi Shomari ni mkweli / katukamata au amekenguka / katulisha tango pori?

Hakuna maumivu makubwa kwa Mwanaume yoyote yule kujua kuwa analea ' bao ' la mwenzake!

Nawasilisha ila nikiwa na uchungu mkubwa sana.
 
Ilikuwa ni jana katika Kipindi kizuri kabisa cha kila Jumapili cha Familia ambacho hurushwa na Kituo cha Super Brand nchini Radio One kuanzia Saa 1 na nusu hadi Saa 4 kamili asubuhi pale ambapo ' mchangiaji ' mmoja ambaye ni ' maarufu ' mno lakini pia ni Mganga wa Kienyeji aitwae Fundi Shomari alipokuwa na ' taarifa ' ambayo kiukweli imechafua kabisa hali ya hewa katika Familia nyingi sana hapa Tanzania tokea jana.

Mada iliyokuwepo jana ilikuwa ni kwanini siku hizi Wapenzi / Wanandoa hawaaminiani hata kidogo katika Mahusiano yao? Wapo Watu wengi waliochangia kama kawaida akina Mama Manka, Mama Abuu wa ukweli na wengineno ila huyu mchangiaji maarufu na Mganga aitwae Fundi Shomari ndiyo alimaliza shughuli yote.

Fundi Shomari alisema kuwa kutokana na ' Utaalam ' wake wa masuala ya Uganga na pia ameshafanya ' tafiti ' zake kwa muda mrefu tu ameamua ' kupasua ' ukweli wake na kutoa ' Siri ' kwa kusema kuwa nanukuu " Kaka Abdallah Mwaipaya na Dada Farhia Middle amini msiamini katika Familia zote zenye Watoto zaidi ya mmoja pale Mtoto halali wa Yule Mwanaume / Mume pale ndani ni yule tu wa Kwanza ila wale waliofuata 99% huyo Mwanaume / Mume amezalishiwa na Mwanaume mwenzake " mwisho wa kumnukuu.

Alipoulizwa nini sababu Fundi Shomari alisema kuwa Kikawaida na kwa Saikolojia ya Wanawake ni kwamba Wanawake wengi hupenda kuwa na Mahusiano mapya kila baada ya miezi mitatu au sita ya Mahusioano yao na kwamba Wanawake huwa ni wepesi sana Kuwakinai Wapenzi wao huku wakiwahisi kuwa labda ni Kaka zao hali ambayo huwafanya kutoka nje kupata Mapenzi / Mahaba mapya.

Binafsi Fundi Shomari tokea jana kanifanya Chakula chochote kile kisiweze kuingia katika Tumbo langu na muda wote tokea jana hadi hivi naandika huu uzi nimekuwa ' mpweke ' mno kutokana na ukweli kwamba nina Wake Watatu halafu wote nimewazalisha Watoto Wanne Wanne hivyo kwa maelezo ya Fundi Shomari ni kwamba hapo GENTAMYCINE Watoto wake halali ni Watatu tu na waliobaki wote Tisa ' nimechapiwa '.

Hapa jirani tu nina Mzee mmoja wa Kigogo Yeye ana wake zake Wawili tu ila wote wawili hao amewazalisha Vikosi viwili vya Simba na Yanga ( namaanisha ana Watoto 22 ) hivyo kwa ' Mahesabu ' ya haraka tu na kwa mujibu wa Fundi Shomari ni kwamba huyu ' Mgogo ' jirani yangu Watoto wake halali ni Wawili tu na hao wengine 20 analea ' mabao ' ya Wenzake tu.

Tokea jana hadi leo ' mood ' yangu haipo kabisa baada ya kumsikia jana Fundi Shomari akitiririka na kuserereka vile ndani ya Kituo Super Brand kabisa Afrika ya Mashariki cha Radio One. Haya wale wenzangu na mie tulio na Watoto Timu za Mpira hebu karibuni hapa tuweze kujadili hili je Fundi Shomari ni mkweli / katukamata au amekenguka / katulisha tango pori?

Hakuna maumivu makubwa kwa Mwanaume yoyote yule kujua kuwa analea ' bao ' la mwenzake!

Nawasilisha ila nikiwa na uchungu mkubwa sana.
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] yawezakuwa ni kweli ila amekosea tathimini kati ya watoto 5 katika hao ishirin ni wa huyo mgogo kwa sababu ya majira ya mzunguko wa hedhi kwa mwanamke

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo mganga muongo,,,si wanawake tunasema muongo,,,,
 
Huyo mganga Fitna sanaaa,anataka kusema na yeye pia huyo anaetumia jina lake sio Babake? aende zake uko,au wanawe kama anao anajua kwa asilimia 99% sio wa kwake na analea tuu just like that?
 
Thredi ya kijinga kabisa.
Kwa iyo we ndo mara yako ya kwanza kusikia? mbona sisi hayo mambo tunayasikia huko kwenye vijiwa lakini hatukuja kujaza server humu?
 
Back
Top Bottom