#COVID19 Mchango wetu kwa Watanzania katikati ya wimbi la Corona

#COVID19 Mchango wetu kwa Watanzania katikati ya wimbi la Corona

Joined
Jun 1, 2021
Posts
99
Reaction score
104
Wakati dunia bado inahangaika na janga la corona au UVIKO19, nasi tumeona tutoe mchango wetu kwa wanaotafuta riziki kupitia biashara zao hususan wale wanaofuata bidhaa zao huko China, Uingereza, Uarabuni na mataifa mengine.

Siku hizi kusafiri imekuwa shida sana, shida zaidi ni kuagiza na kufuata mzigo nje ya Tanzania. Wajasiriamali wanakutana na vikwazo pale wanapotaka kufuata mzigo na hawajachanja chanjo ya corona. Hii imekwamisha biashara za watu wengi achilia mbali kuchelewesha huduma katika sekta mbalimbali.

MCHANGO WETU NI UPI?

Ili kulinda afya za watanzania na kunusuru biashara za wajasiriamali na sekta nyingine zinazoagiza na kufuata mizigo nje ya nchi, sasa tutakuwa tunafuata mizigo na bidhaa popote pale nje ya nchi na kuwasaidia kusafirisha kuja nchini. Hii itaepusha usumbufu wa safari, gharama pamoja na kutolazimisha wale wasiotaka kuchoma chanjo kwa sasa, kuchoma kwa sababu tu za kibiashara.

Tunaamini kwa kufanya hivi tutaweza kusaidia kuchochea uchumi na kuepusha vifo vya biashara na ucheleweshaji wa huduma. Huu utakuwa ni mchango wetu na tunaamini unaendana na dira ya serikali katika kuinua uchumi wa nchi yetu.

Tunakaribisha maswali, maoni na ushauri.
 
Wakati dunia bado inahangaika na janga la corona au UVIKO19, nasi tumeona tutoe mchango wetu kwa wanaotafuta riziki kupitia biashara zao hususan wale wanaofuata bidhaa zao huko China, Uingereza, Uarabuni na mataifa mengine.

Siku hizi kusafiri imekuwa shida sana, shida zaidi ni kuagiza na kufuata mzigo nje ya Tanzania. Wajasiriamali wanakutana na vikwazo pale wanapotaka kufuata mzigo na hawajachanja chanjo ya corona. Hii imekwamisha biashara za watu wengi achilia mbali kuchelewesha huduma katika sekta mbalimbali.

MCHANGO WETU NI UPI?

Ili kulinda afya za watanzania na kunusuru biashara za wajasiriamali na sekta nyingine zinazoagiza na kufuata mizigo nje ya nchi, sasa tutakuwa tunafuata mizigo na bidhaa popote pale nje ya nchi na kuwasaidia kusafirisha kuja nchini. Hii itaepusha usumbufu wa safari, gharama pamoja na kutolazimisha wale wasiotaka kuchoma chanjo kwa sasa, kuchoma kwa sababu tu za kibiashara.

Tunaamini kwa kufanya hivi tutaweza kusaidia kuchochea uchumi na kuepusha vifo vya biashara na ucheleweshaji wa huduma. Huu utakuwa ni mchango wetu na tunaamini unaendana na dira ya serikali katika kuinua uchumi wa nchi yetu.

Tunakaribisha maswali, maoni na ushauri.

Mkuu, gonjwa hili ninyi mmeona fursa siyo?

Nilidhani mnatokea tushirikiane sasa kuifanya serikali itambue si sahihi hata kidogo:

1. kutuongezea kodi na tozo katika kipindi hiki cha gonjwa hili ambapo pana ugumu haswa wa kufanya biashara?
2. kututelekezea janga ikiwamo kutuachia kujilipia gharama za matibabu tunapokumbwa na gonjwa hili?
3. kuendelea na miradi yake yote kana kwamba kila kitu ni shwari kabisa?
4. kutokuwa na mpango mkakati madhubuti wa kuwahami watu dhidi ya gonjwa hili?
5. Nk.

Yako mengi mkuu.

Wako wapi kina jiwe walio-jimwambafy na kuyajaribu maisha kana kwamba gonjwa hili halipo?

Kwani walikosea waliosema "tamaa mbele mauti nyuma?"

Kwa hali ilivyo mtaani nani ajuaye hata kama tutatoboa tukiwa bado hai hata kwa mwaka huu tu?
 
Mkuu, gonjwa hili ninyi mmeona fursa siyo?

Nilidhani mnatokea tushirikiane sasa kuifanya serikali itambue si sahihi hata kidogo:

1. Kutuongezea kodi na tozo katika kipindi hiki cha gonjwa hili ambapo pana ugumu haswa wa kufanya biashara.
2. Kututelekezea janga ikiwamo kutuachia kujilipia gharama za matibabu tunapokumbwa na gonjwa hili.
3. Kuendelea na miradi yake yote kana kwamba kila kitu ni shwari kabisa.
4. Kutokuwa na mpango mkakati madhubuti wa kuwahami watu dhidi ya gonjwa hili.
5. Nk.

Yako mengi mkuu.

Wako wapi kina jiwe walio-jimwambafy na kuyajaribu maisha kana kwamba gonjwa hili halipo?

Kwani walikosea waliosema "tamaa mbele mauti nyuma?"

Kwa hali ilivyo mtaani nani ajuaye hata kama tutatoboa tukiwa bado hai hata kwa mwaka huu tu?

Mkuu brazaj,

Asante kwa maoni na ushauri.

Kwenye hili janga la UVIKO19, kila mmoja kwa nafasi yake anajaribu kufanya lile analoweza kushiriki katika kuhakikisha maisha yanaendelea kama kawaida. Sisi kwa upande wetu tumeanza na hilo, pengine tutaendelea na mengine kwa kadri nafasi yetu itakavyoturuhusu.

Tunatoa wito kwa wadau wengine ukiwemo wewe kutoa mchango wako pia, ili sote kwa pamoja tupunguze athari zilizosababishwa na zinazoendelea kusababishwa na maradhi haya.
 
Mkuu brazaj,

Asante kwa maoni na ushauri.

Kwenye hili janga la UVIKO19, kila mmoja kwa nafasi yake anajaribu kufanya lile analoweza kushiriki katika kuhakikisha maisha yanaendelea kama kawaida. Sisi kwa upande wetu tumeanza na hilo, pengine tutaendelea na mengine kwa kadri nafasi yetu itakavyoturuhusu.

Tunatoa wito kwa wadau wengine ukiwemo wewe kutoa mchango wako pia, ili sote kwa pamoja tupunguze athari zilizosababishwa na zinazoendelea kusababishwa na maradhi haya.

Mkuu inataka moyo mgumu kama wa jiwe kutokutambua hali tete ya maisha inayotukabili kama viumbe hai ndani ya gonjwa hili.

IMG_20210718_063455_991.jpg


Inahitaji ujasiri wa ndege kama huyu kudhani kuwa yuko salama dhidi chui wenye njaa, kwetu sisi kufikiri tuko salama kiasi cha kuendelea na maisha kama kawaida.

Inatatiza kusikia mipango ya mwakani bila ya kujua mikakati ya kuwepo hai mwakani.

Uko wapi mkakati wetu wa kuwa hai kabla ya kujikita kwenye uwekezaji na hata kukabiliana na tozo na kodi zilizo boreshwa?
 
Mkuu inataka moyo mgumu kama wa jiwe kutokutambua hali tete ya maisha inayotukabili kama viumbe hai ndani ya gonjwa hili.

View attachment 1900191

Inahitaji ujasiri wa ndege kama huyu kudhani kuwa yuko salama dhidi chui wenye njaa, kwetu sisi kufikiri tuko salama kiasi cha kuendelea na maisha kama kawaida.

Inatatiza kusikia mipango ya mwakani bila ya kujua mikakati ya kuwepo hai mwakani.

Uko wapi mkakati wetu wa kuwa hai kabla ya kujikita kwenye uwekezaji na hata kukabiliana na tozo na kodi zilizo boreshwa?
Tunathamini mchango wako mdau
 
Back
Top Bottom