Mchawi wao.

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Alitokea mchawi, kawaroga watu hawa.
Akawapa ukiziwi, na magonjwa yaso dawa.
Kawafanya wawe kiwi, ndege wasio na mbawa.
Mchawa alipania, kuwatesa si kuua.

Kawaroga mashujaa, kafanya wawe wanyonge.
Kawaroga wenye njaa, kwa uchawi wa matonge.
Karoga saa na taa, kuvizuzua viringe.
Mchawi alipania, kuwatesa si kuua.

Kawafisha kiurongo, kawafanya mizukule.
Amewaroga ubongo, kwa wao akili nywele.
Karoga jino na pengo, vya kumung'unya ndo wale.
Mchawi alipania, kuwatesa si kuua.

Kawatupia majini, mengi ya'so na idadi.
Akawatenda kihuni, hata kipofu shahidi.
Wanaenda hawaoni, karoga kichwa na bodi.
Mchawi alipania, kuwatesa si kuua.

Anga za malenga.
 
namaanisha hiv...kama unahisi unakula vitu vizuri...basi vizuie visitoke..ila vibaki tumboni tu. ashakum si matusi mkuu
 
Kiswahili si kigumu ila nikitamu...kama alivyosema marehemu Shaaban Roberts..."titi la mama litamu...,"

Na ukitaka kuujuwa utamuwe sharti unyonye hilo ziwa, basi waweza linyonya hilo ziwa kwa methali, misemo, tenzi na mashairi kama tunavyoona kwenye beti hizo za Mchawi wao.

Tatizo tumeacha mila zetu na kufata za wageni...kisha hukaa pembeni na kususuwikwa kwa majozi kwa kukumbuka mambo ya wazee wetu wa kale walivyo enzi kiswahili kwa tabia na vitendo basi...

"kusi na kaskazi maji yametuzingia
si kunde wala mbaazi zote zimetukimbia
mambo ya juzi na jana leo tuna yalilia???"

basi tukienzi kiswahili kwa tabia na vitendo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…