Pre GE2025 Mchengerwa awaagiza wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi kupanga ratiba ya uzinduzi wa miradi iliyosalia kwa kushirikisha wabunge

Pre GE2025 Mchengerwa awaagiza wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi kupanga ratiba ya uzinduzi wa miradi iliyosalia kwa kushirikisha wabunge

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri kupanga ratiba ya uzinduzi wa miradi mbalimbali iliyosalia kwa kushirikisha wabunge.

Akizungumzia suala hilo, Mchengerwa amesema “Sasa kwa kuwa tunayo miradi mingi ambayo bado haijafunguliwa, wabunge hawa wamefanya kazi nzuri. Nitumie fursa hii kuwaelekeza wakuu wa mikoa, wilaya hapa, wakurugenzi wa halmashauri sasa kuwapangia wabunge hawa miradi yote ambayo haijazinduliwa. Waende mara moja katika majimbo yetu yote mia mbili kumi na tano.

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Wakurugenzi, wakuu wa mikoa na wakurugenzi waandae utaratibu uleule kama nakwenda waziri kiongozi wa juu kabisa waende wabunge wa kuzindua miradi hii kwa sababu wabunge hawa ndiyo waliosemea miradi hii ikashuka kule kwenye majimbo yetu. Wabunge hawa. Wamefanya kazi kubwa na kazi nzuri sana”.

Mchengerwa alitoa agizo hilo leo, Jumanne, Februari 11, 2025, wakati akichangia hoja za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, katika kikao kilichofanyika bungeni jijini Dodoma

 
Tunachohitaji ni upatikanaji au utekelezwaji wa hiyo miradi na sio uzinduzi pekee. Wanazindua mradi mfano wa maji, zahanati/ hospitali; baada ya uzinduzi huduma hazipatikani
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri kupanga ratiba ya uzinduzi wa miradi mbalimbali iliyosalia kwa kushirikisha wabunge.

Akizungumzia suala hilo, Mchengerwa amesema “Sasa kwa kuwa tunayo miradi mingi ambayo bado haijafunguliwa, wabunge hawa wamefanya kazi nzuri. Nitumie fursa hii kuwaelekeza wakuu wa mikoa, wilaya hapa, wakurugenzi wa halmashauri sasa kuwapangia wabunge hawa miradi yote ambayo haijazinduliwa. Waende mara moja katika majimbo yetu yote mia mbili kumi na tano.

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Wakurugenzi, wakuu wa mikoa na wakurugenzi waandae utaratibu uleule kama nakwenda waziri kiongozi wa juu kabisa waende wabunge wa kuzindua miradi hii kwa sababu wabunge hawa ndiyo waliosemea miradi hii ikashuka kule kwenye majimbo yetu. Wabunge hawa. Wamefanya kazi kubwa na kazi nzuri sana”.

Mchengerwa alitoa agizo hilo leo, Jumanne, Februari 11, 2025, wakati akichangia hoja za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, katika kikao kilichofanyika bungeni jijini Dodoma

View attachment 3233326
Ghafla wamezinduka! Siku zote walikuwa wapi?!
Kweli KULA/KURA si mchezo!
Uchaguzi 2025 watu joto la tumbo!
 
Back
Top Bottom