LGE2024 Mchengerwa: Muda bado upo, wagombea wakate rufaa

LGE2024 Mchengerwa: Muda bado upo, wagombea wakate rufaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Wakienda kukata rufaa wanakuta ofisi zimefungwa! Imekuwa kama mchezo wa paka na panya!

====

Screenshot_20241112_160302_Instagram.jpg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amesema wagombea wa uchaguzi wa Serikali za mitaa ambao hawakutendewa haki, bado wanayo nafasi ya kukata rufaa.

Kupata nyuzi kimkoa Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mchengerwa amesema rufaa hizo zinazokatwa ngazi ya wilaya zinapaswa kukatwa na wagombea wenyewe na si vyama vya siasa. Muda wa rufaa umeanza Novemba 10 hadi kesho Jumatano, Novemba 13, 2024.

Waziri huyo amesema hayo leo Jumanne, Novemba 12, 2024 jijini Dar es Salaam katika semina ya wahariri kuhusu Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

"Muda wa kukata rufaa bado upo, watu wakate rufaa wasikae majumbani na kuviachia vyama vyao, rufaa inakatwa na mgombea. Kwa hiyo wale ambao wanaona hawajatendewa haki wakate rufaa sasa," amesema.

Aidha, Mchengerwa amesema uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano ya Novemba 27, 2024 umeshirikisha vyama vyote 19.
 
Kifua Kipana na wewe bado ni mhitimu wa UDISM? Ni kweli au si kweli au ni uongo?
 
Wakuu,

Wakienda kukata rufaa wanakuta ofisi zimefungwa! Imekuwa kama mchezo wa paka na panya!

====


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amesema wagombea wa uchaguzi wa Serikali za mitaa ambao hawakutendewa haki, bado wanayo nafasi ya kukata rufaa.

Kupata nyuzi kimkoa Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mchengerwa amesema rufaa hizo zinazokatwa ngazi ya wilaya zinapaswa kukatwa na wagombea wenyewe na si vyama vya siasa. Muda wa rufaa umeanza Novemba 10 hadi kesho Jumatano, Novemba 13, 2024.

Waziri huyo amesema hayo leo Jumanne, Novemba 12, 2024 jijini Dar es Salaam katika semina ya wahariri kuhusu Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

"Muda wa kukata rufaa bado upo, watu wakate rufaa wasikae majumbani na kuviachia vyama vyao, rufaa inakatwa na mgombea. Kwa hiyo wale ambao wanaona hawajatendewa haki wakate rufaa sasa," amesema.

Aidha, Mchengerwa amesema uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano ya Novemba 27, 2024 umeshirikisha vyama vyote 19.
Mchengerwa kwa uhuni uliofanya kuharibu huu uchaguzi tunapeleka mashtaka yetu kwa Mungu, wewe una Samia mkweo sisi tuna Mungu tutaona nani zaidi kati ya Mungu na Samia.
 
Wakuu,

Wakienda kukata rufaa wanakuta ofisi zimefungwa! Imekuwa kama mchezo wa paka na panya!

====


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amesema wagombea wa uchaguzi wa Serikali za mitaa ambao hawakutendewa haki, bado wanayo nafasi ya kukata rufaa.

Kupata nyuzi kimkoa Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mchengerwa amesema rufaa hizo zinazokatwa ngazi ya wilaya zinapaswa kukatwa na wagombea wenyewe na si vyama vya siasa. Muda wa rufaa umeanza Novemba 10 hadi kesho Jumatano, Novemba 13, 2024.

Waziri huyo amesema hayo leo Jumanne, Novemba 12, 2024 jijini Dar es Salaam katika semina ya wahariri kuhusu Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

"Muda wa kukata rufaa bado upo, watu wakate rufaa wasikae majumbani na kuviachia vyama vyao, rufaa inakatwa na mgombea. Kwa hiyo wale ambao wanaona hawajatendewa haki wakate rufaa sasa," amesema.

Aidha, Mchengerwa amesema uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano ya Novemba 27, 2024 umeshirikisha vyama vyote 19.
Hamtafunga ofisi?
 
Wanafanya mambo ya kipuuzi halafu wanajfichia kwenye rufaa. Upinzani wanapaswa kutangaza kugomea huu uchaguzi wa kifua kipana
 
Sisi tunasema Chadema waendelee na mipango mingine ya kisiasa ila huu uchaguzi tayari ushakuwa upumbavu wa hali ya juu. Never trust them anymore
 
Wakuu,

Wakienda kukata rufaa wanakuta ofisi zimefungwa! Imekuwa kama mchezo wa paka na panya!

====


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amesema wagombea wa uchaguzi wa Serikali za mitaa ambao hawakutendewa haki, bado wanayo nafasi ya kukata rufaa.

Kupata nyuzi kimkoa Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mchengerwa amesema rufaa hizo zinazokatwa ngazi ya wilaya zinapaswa kukatwa na wagombea wenyewe na si vyama vya siasa. Muda wa rufaa umeanza Novemba 10 hadi kesho Jumatano, Novemba 13, 2024.

Waziri huyo amesema hayo leo Jumanne, Novemba 12, 2024 jijini Dar es Salaam katika semina ya wahariri kuhusu Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

"Muda wa kukata rufaa bado upo, watu wakate rufaa wasikae majumbani na kuviachia vyama vyao, rufaa inakatwa na mgombea. Kwa hiyo wale ambao wanaona hawajatendewa haki wakate rufaa sasa," amesema.

Aidha, Mchengerwa amesema uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano ya Novemba 27, 2024 umeshirikisha vyama vyote 19.
Miaka 60 ya kutawala ccm wanaogopa uchaguzi mpk kuwaengua wtz wenzao wanaogopa nn ? Tunahitaji katiba mpya haraka sana ili tujenge taifa lenye usawa
 
Back
Top Bottom