Mchezaji wa Njombe Mji ajeruhiwa na shabiki ,fujo za tawala uwanjani..Hakika juma nyoso alikuwa sahihi kumpiga shabiki

Mchezaji wa Njombe Mji ajeruhiwa na shabiki ,fujo za tawala uwanjani..Hakika juma nyoso alikuwa sahihi kumpiga shabiki

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
Katika hali ya kushangaza mechi ya Njombe mji na majimaji ilitawaliwa na fujo ,mashabiki wa timu ya majimaji kudai taulo la goli kipa wa Njombe mji aliloliweka pembezoni mwa goli kwaajili ya kufutia kuwa ilikuwa inawanyima ushindi

Shabiki wa majimaji aliingia uwanjani na kwenda kumpiga na kumjeruhi goli kipa wa Njombe mji vibaya sana jambo lililosabahisha fujo kutawala


Katika mahojiano mashabiki wa majimaji walidai taulo hilo lilikuwa linazuia magoli kwa nguvu za Giza na kama lingeondolewa basi wangerudi kwao songea na ushindi[emoji116]




NB:Juzi Juma Nyosso alimpiga shabiki wa simba ngumi moja na yule shabiki kuzimia sababu kubwa ni yule shabiki kumfuata nyosso na kumpulizia vuvuzela sikioni huku akimtukana ..watu wengi walimlaumu Nyosso

Je hili tukio la shabiki kutoka jukwaani na kuingia uwanjani ilhali mechi inaendelea na kuanza kumshushia makonde golikipa mpaka kumjeruhi sababu tu ya taulo tuitafsiriaje mfano huyu kipa angempiga shabiki mpaka kuzimia tungeanza kumlaumu na kusingizia nidhamu mbovu


8ca606851c756855b23ac08384b8d4b7.jpg


c37264b298e3c4d55cf9fae75c74dd36.jpg



Jamani mbona makipa wa ulaya wanaweka taulo golini kwao kwaajili ya kufutia mikono yao "gloves" kuondoa utelezi..
 
Back
Top Bottom