Mchezo wa soka unaongozwa na kanuni sio mihemko ya watu

Mchezo wa soka unaongozwa na kanuni sio mihemko ya watu

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia soka la hapa bongo,ni kama lina kanuni zake tofauti na kanuni za FIFA.

Imekuwa kitu cha kawaida na hata kwa waamuzi kudhani kwa kuwa ngozi nyeusi inaonesha ugumu au usugu fulani dhidi ya mazingira ya jua,basi ni ishara kuwa watu weusi wana nguvu.Hivyo uwanjani mchezaji akichezewa faulo eneo la kumi na nane,hadi aumie sana ndipo inakuwa penalty.

Yaani kwa mujibu wa hisia za hawa watanzania wakiwemo wachambuzi wa soka,ikibidi mchezaji avunjwe miguu ndani ya box ndipo pigo la penalty liamuriwe.

Inashangaza kidogo kusikia wakisema magoli ya penalty yana hadhi ndogo kwa kuwa hawakuona kadenge na mpira kashuti goo!

Kanuni zinasema timu mgeni ifanye mazoezi katika uwanja wa mwenyeji muda ule ule mechi itakapochezwa.

Kuna maana ya kuweka kanuni hii.Wamekaa wataalamu wabobevu wa soka wakaiweka kanuni hii ikiwa na maana sana.

Wanakuja waluga luga ambao hawaamini katika kanuni za soka wanasema hamtakiwi kufanya mazoezi humu kwani kipi msichojua kuhusu uwanja huu!

Hayo ni maajabu sana,kwani timu inayocheza,wachezaji hubadilika mara kwa mara,na huenda wapo wachezaji watahitaji kujua uwanja unakuwaje.

Ninaamini soka likiachwa lichezwe kwa kanuni,kuna timu zitadondoka na kutostahili kuwa hapo zilipo,ingawa kipimo cha ukweli huwa ni mechi za kimataifa.

Huko kanuni hufuatwa na ndio maana timu kama haiko sawa ,haiwezi kufika popote.

Tubaki tu hapa kwetu tukiwa na sheria na kanuni zetu wenyewe,kama za mechi za ndondo huku tukiwaza ushirikina na tunatumia pesa nyingi kusajili.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Mara ooh huu mchezo siyo muhimu kwetu, ni kama mazoezi.
Sasa mnalia nini?
 
Utopolo ni timu iliyojifia tayari, ili inyanyuke inahitaji figisu kama hizo na nyingine nyingi za nje ya uwanja, ndo wajione bado bora kumbe timu imekwisha jifia tayari.

Yaani umewahi kuona wapi timu ikawa bora ndani msimu mmoja ikafundishwa na MAKOCHA wasio pungua SITA kwa nyakati tofauti!?...
 
"Katika Sintofahamu hiyo, Simba iliarifiwa na Meneja wa Uwanja kuwa hana maelekezo ya kuruhusu mazoezi kufanyika bila maelekezo ya kamishna wa Mchezo".
"... Kamishna wa michezo akafika hadi uwanjani usiku huo na kutoa maelekezo kwa meneja. Meneja akaruhusu mazoezi yafanyike, lakini wahuni bila kutaja sababu, wakazuia basi la wachezaji lisiingie."
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Usiku wote huu mshatia mpira kwapani? ndugu zetu mnadeka sana.
 
Tusaidie na kakuni zinazoruhusu mechi kuahirishwa.
 
CORRUPTION IN SOCCER YETU IS A NEW CULTURE

HII GAME ITUONYESHE MENO YA PCCB
 
Utopolo ni timu iliyojifia tayari, ili inyanyuke inahitaji figisu kama hizo na nyingine nyingi za nje ya uwanja, ndo wajione bado bora kumbe timu imekwisha jifia tayari.

Yaani umewahi kuona wapi timu ikawa bora ndani msimu mmoja ikafundishwa na MAKOCHA wasio pungua SITA kwa nyakati tofauti!?...
Unalinganisha ligi za wenzetu ambazo level za ushindani unakaribiana. Hapa Tanzania ukiitoa Azam, Simba na Yanga timu zilizobaki zipo dhoofu sana katika ubora. Gap ni kubwa sana mzee hilo mliweke kichwani.

Halafu kuhusu Simba kutofanya mazoezi katika uwanja wa Mkapa, ni kama Simba kutafuta sababu ya kuikimbia mechi. Derby zote zilizopita baina ya Simba na Yanga huwa timu zinafanyia mazoezi ya mwisho kwenye viwanja vyao vya mitaani na sio kwenda kuingia uwanja wa unaotumika katika mechi kwenda kufanya mazoezi
 
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikifuatilia soka la hapa bongo,ni kama lina kanuni zake tofauti na kanuni za FIFA.

Imekuwa kitu cha kawaida na hata kwa waamuzi kudhani kwa kuwa ngozi nyeusi inaonesha ugumu au usugu fulani dhidi ya mazingira ya jua,basi ni ishara kuwa watu weusi wana nguvu.Hivyo uwanjani mchezaji akichezewa faulo eneo la kumi na nane,hadi aumie sana ndipo inakuwa penalty.

Yaani kwa mujibu wa hisia za hawa watanzania wakiwemo wachambuzi wa soka,ikibidi mchezaji avunjwe miguu ndani ya box ndipo pigo la penalty liamuriwe.

Inashangaza kidogo kusikia wakisema magoli ya penalty yana hadhi ndogo kwa kuwa hawakuona kadenge na mpira kashuti goo!

Kanuni zinasema timu mgeni ifanye mazoezi katika uwanja wa mwenyeji muda ule ule mechi itakapochezwa.

Kuna maana ya kuweka kanuni hii.Wamekaa wataalamu wabobevu wa soka wakaiweka kanuni hii ikiwa na maana sana.

Wanakuja waluga luga ambao hawaamini katika kanuni za soka wanasema hamtakiwi kufanya mazoezi humu kwani kipi msichojua kuhusu uwanja huu!

Hayo ni maajabu sana,kwani timu inayocheza,wachezaji hubadilika mara kwa mara,na huenda wapo wachezaji watahitaji kujua uwanja unakuwaje.

Ninaamini soka likiachwa lichezwe kwa kanuni,kuna timu zitadondoka na kutostahili kuwa hapo zilipo,ingawa kipimo cha ukweli huwa ni mechi za kimataifa.

Huko kanuni hufuatwa na ndio maana timu kama haiko sawa ,haiwezi kufika popote.

Tubaki tu hapa kwetu tukiwa na sheria na kanuni zetu wenyewe,kama za mechi za ndondo huku tukiwaza ushirikina na tunatumia pesa nyingi kusajili.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Kwenye kanuni hizo hizo tueleze ni kanuni ipi inasema ukizuiwa kufanya mazoezi ya mwisho basi timu mgeni inatakiwa igomee kucheza mechi? Simba msitafute kichaka cha kujifichia inaonekana plani zenu za ulozi zilibuma na viongozi wenu waliona ni heri lawama kuliko fedheha baada ya kuona mnaenda kuaibika,,
Unasema yanga walizuia walizuiaje? Yanga wanamiliki uwanja? Wasimamizi wa uwanja si walikuwepo,,kwanini awakupewa taarifa kwamba Kuna timu itakuja kufanya mazoezi usiku?
 
"... Kamishna wa michezo akafika hadi uwanjani usiku huo na kutoa maelekezo kwa meneja. Meneja akaruhusu mazoezi yafanyike, lakini wahuni bila kutaja sababu, wakazuia basi la wachezaji lisiingie."
Hakika mpira wa Tz, TFF na bodi ya ligi ni vichekesho vya pasua vichwa. Yaani kuna wahuni wanaoweza kufanya lolote, hawakamatiki mpaka wazuie gari lisiingie uwanjani?
 
Nilipoona hii picha nilijua kuna shida inakuja mbele.

1000057989.jpg
 
Kwenye kanuni hizo hizo tueleze ni kanuni ipi inasema ukizuiwa kufanya mazoezi ya mwisho basi timu mgeni inatakiwa igomee kucheza mechi? Simba msitafute kichaka cha kujifichia inaonekana plani zenu za ulozi zilibuma na viongozi wenu waliona ni heri lawama kuliko fedheha baada ya kuona mnaenda kuaibika,,
Unasema yanga walizuia walizuiaje? Yanga wanamiliki uwanja? Wasimamizi wa uwanja si walikuwepo,,kwanini awakupewa taarifa kwamba Kuna timu itakuja kufanya mazoezi usiku?
Mbumbu hawawezi kukuelewa.
 
Back
Top Bottom