Mwaka mpya wa kichina ndio huo umekaribia, katika jamii ya Wachina kila mchina kwa kadri awezavyo anatakiwa kurudi nyumbani kwake. Katika jamii hii ya Wachina wazazi hujisikia sifa na kumkweza mtoto wao pindi anaporudi nyumbani akiwa na mchumba yake haswaa kama anavutia, ana hela nk.
Kitu ambacho ni nadra kwa jamii yetu ya Tanzania, leo katika pitapita zangu mitandaoni nikakutana na matangazo(haswaa kwenye mitandao ya Groupon) yanayotoa punguzo na offer kwa kukodi mchumba wa kurudi naye nyumbani.
Katika jamii ya Wachina, kukodisha mchumba si jambo la hatari kwakuwa wengi wao wanaendeshwa kwa kuuza sura(jinsi watu wanavyokudhani). Nimewahi kuuona mkataba wa uchumba wa kukodi, mkataba huo humtaka muhusika kuzuga kadri awezavyo ili wazazi au marafiki wasijue kinachoendelea, ila hawaruhusiwi kuwa na mahusiano yoyote ya kimapenzi, pia wakiwa ndani ya mkataba mkodiwa anatakiwa kufuata amri za bosi wake, kinyume chake kitapeleka kutolipwa mafao.
Je unalionaje hili suala la kukodisha boyfriend au Girlfriend ili kukupa company kwa mtazamo wa kikwetukwetu, pia nyumbani huduma hii inapatikana?
Souce: Ughaibuni.com
Kitu ambacho ni nadra kwa jamii yetu ya Tanzania, leo katika pitapita zangu mitandaoni nikakutana na matangazo(haswaa kwenye mitandao ya Groupon) yanayotoa punguzo na offer kwa kukodi mchumba wa kurudi naye nyumbani.
Katika jamii ya Wachina, kukodisha mchumba si jambo la hatari kwakuwa wengi wao wanaendeshwa kwa kuuza sura(jinsi watu wanavyokudhani). Nimewahi kuuona mkataba wa uchumba wa kukodi, mkataba huo humtaka muhusika kuzuga kadri awezavyo ili wazazi au marafiki wasijue kinachoendelea, ila hawaruhusiwi kuwa na mahusiano yoyote ya kimapenzi, pia wakiwa ndani ya mkataba mkodiwa anatakiwa kufuata amri za bosi wake, kinyume chake kitapeleka kutolipwa mafao.
Je unalionaje hili suala la kukodisha boyfriend au Girlfriend ili kukupa company kwa mtazamo wa kikwetukwetu, pia nyumbani huduma hii inapatikana?
Souce: Ughaibuni.com