Mchumba wa Miss Judith!



hata mie namsubiri ajibu hapa....maana tumefunga sana kwa ajili yake...
 
Bifu la Babu wa Loliondo kati yenu limeisha??
 
samahani sana wapendwa,

nimechelewa kuiona hii thread hadi imefika ukuasa huu!! nimefurahishwa na PJ kwa kukumbusha ahadi yangu ya kuwajulisheni nini kinaendelea baada ya maombi mazito ya siku 30. kipekee namshukuru sana Mayasa kwa kujitahidi kuwaweka sawa wengine. ubarikiwe sana dada. pia nawashukuru wote kwa upendo huu mkubwa mliouonyesha kwangu, nasema asanteni sana.

kwa kifupi, pamoja na kuzidiwa na majukumu mengi kikazi, Mungu aliyajibu maombi tena vizuri sana. mchumba wangu anaitwa Naiman na ni mzaliwa wa Iringa. kama mjuanvyo masuala haya yana logistics nyingi na hivyo kukamilisha yote yaliyo ya muhimu inahitaji muda. hadi sasa mengine hayajakamilika. hapo katikati nilibahatika kupata scholarship ya kuripoti chuoni september mwaka huu na hivyo mtaona kuna kibarua cha kupangilia mambo hapo, kupata ruhusa na likizo ya masomo kazini na kuandaa harusi na wakati huohuo kutakiwa kuwa chuoni. so baada ya panga pangua, natarajia kwenda choni kwanza na kisha kurudi nyumbani november kwa ajili ya kufunga ndoa.

pia kuna thread inaitwa Wingu na Mbingu, ni shairi linalotoa majibu niliyoahidi, baada ya kumsoma PJ kwenye thread ya loliondo ilinilazimu kukaa chini kwa dakika chache ili niwape feedback kwa mtindo wa shairi.

nawapenda wote wapendwa na mbarikiwe sana na Bwana

Glory to God!

basi Mungu na ashukuriwe
atupaye sisi kushinda
basi ndugu na uimarike
uzidi kuitenda kazi
hata mwisho uifikie
furaha ile ya milele
 
hahaha humu ndani kuna kila aina ya burudani. Unajua majibu ya maombi kama hayo inachukua muda. Hivi kupata mchumba ni kitu kidogo. sana sana unaweza angukia kwa married man aliyepretend sijao. Hii ni lazima uwe mvumilivu na uwe na maombi ya ukweli ikibidi kwenda mlimani siku 40 hayo ni mwanaume bwana! mimi sina hamu naangalia tu!
 

asante mpendwa,
ubarikiwe sana
 
TUNAKUSHUKURU SANA DADA YETU MISS JUDITH sijui hapo nipo sawa, coz nahis wastahili kuitwa Ms. Judith instead of Miss Judith! Dada umeweka mambo sawa, naimani umeeleweka vizuri, twakuombea logistics zako za uchumba ziende sawa, upate ruhusa kazini na uende masom6. Usije tusahau wa Jamvini!
 

Ameen..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…