Mchungaji akamatwa vurugu za Geita

Mchungaji akamatwa vurugu za Geita

Sumasuma

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2011
Posts
342
Reaction score
110
MCHUNGAJI wa Kanisa la PAGT, Isaya Rutta (52), mkazi wa Kijiji cha Katoro, Wilaya ya Geita, mkoani Geita, anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuchinja ng'ombe mmoja na mbuzi wawili kinyume cha sheria, hali iliyosababisha vurugu kati ya Waislamu na Wakristo.

Vurugu hizo zilitokea juzi na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye ni mchungaji wa kanisa moja wilayani hapa huku watu wengine 10 wakijeruhiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Paulo Kasabango, alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi katika kijiji hicho ambapo inadaiwa kuwa alihusika kuchinja mifugo eneo la Kanisa la AIC bila ya kuhusisha daktari wa mifugo kwa lengo la kuthibitishwa kama nyama hiyo ni salama kuliwa na binadamu.

Kasabango alisema kuwa mbali na kukamatwa kwa kosa hilo, pia anadaiwa kufanya makosa ya kuchinja eneo ambalo si rasmi kwa mujibu wa sheria ya kifungu namba 17 ya mwaka 2003.

Alisema kuwa mtuhumiwa mwingine Ramadhani Pastory, ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, anadaiwa kumuua Mchungaji Mathayo Kachila wa Kanisa la PAGT Buseresere na kwamba atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo wakati wowote akipata nafuu.

Uchunguzi wa gazeti hili uliothibitishwa na polisi umebaini kuwa baadhi ya watu katika Kijiji cha Buseresere wametelekeza familia zao na kukimbilia kusikojulikana ili kukwepa mkono wa sheria, kwa hofu ya kukamatwa na kuhusishwa na vurugu hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Magalula Saidi Magalula, alikemea vikali kitendo walichokifanya baadhi ya wananchi cha kujichukulia sheria mkononi, akisema kuwa kinahatarisha amani.

Naye Mganga Mfawidh wa Hospitali ya Mkoa wa Geita, John, alisema hali za majeruhi zinaendelea vizuri na kwamba hawajapokea majeruhi wengine isipokuwa kati ya waliopokewa jana Ramadhani Pastory (52) na Sadiki Yahaya (40), wamehamishiwa Bugando kutokana na hali zao kuwa mbaya.

source:Tanzania daima
 
Nimeipata hii kutoka gazeti la raia mwema:

Mgogoro wa nani ana haki ya kuchinja umekuwa ukifukuta Mkoani Mwanza tangu Mei mwaka jana baada ya kulipuka wakati wa mazishi ya mzee Kamuli ambaye alikuwa muumini wa Kanisa la AICT Nyehunge. Katika msiba huo mchungaji wake, James Lutambi, alichinja ng’ombe kwa ajili ya kitoweo msibani.


Waislamu waliohudhuria msiba walihoji nani aliyekuwa amechinja wakaambiwa ni mchungaji. Wakataka kujua kwanini amechinja, yakatokea majibizano kidogo kabla ya waislamu kuondoka na kisha wakamwandikia Mtendaji wa Kijiji barua ya kutangaza kujitenga kushirikiana na wakristo katika misiba na sherehe.


Baada ya tangazo hilo, wakristo nao wakaamua kuwa na bucha yao. Baada ya kushughulikiwa katika ngazi mbalimbali za uongozi tangu katika kata hadi wilaya na kutopatikana suluhu, ndipo alipolazimika kwenda Mkuu wa Mkoa ambaye ni kama alikwenda kuuwasha moto zaidi badala ya kuutuliza.


Inaelezwa na baadhi ya wananchi wa Nyehunge kwamba Desemba 31, 2012 mchungaji Paul Range wa kanisa la EAGT alikamatwa na polisi na kuwekwa mahabusu kwa kosa la kuchinja ng’ombe machinjioni. Pamoja naye, mmiliki wa ngombe huyo naye aliwekwa mahabusu kwa kosa hilo hilo, tukio hilo lilisababisha pia Mkuu wa mkoa wa Mwanza kuamuru mtendaji wa kijiji cha Nyehunge kufukuzwa kazi kwa kushindwa kudhibiti uchinjaji huo.

Source: Raia Mwema
 
Naona mchungaji wa watu anakamatishwa kesi hivi hivi mchana kweupe kwani hayo makosa yanaonekana ni ya kuungaunga tu. Yote hiyo ni kutotaka kuwaudhi wakubwa ili ionekane tu kwamba na wakristo nao walikuwa na makosa na wamepelekwa mahakamani. Aibu tupu! Tuliite koleo kwa jina lake la koleo na si sahihi kusema ni kijiko kikubwa.
 
Unajua mi sikujua nini sababu ya haya yote! Kumbe inshu ni njaaa hapo ndugu mwanzo Wa ukorofi wote ni njaa!!! Kwamba waislamu walisusa kula Kisa kibudu!!!! Umaskini jamani utatuingiza kwenye vita! Moshi kama unafuka tutegee moto kuwaka!sasa mnapo sema wanasiasa mnapata habari wapi? amaa uvivu Wa kufikiria na kusoma na kufuatilia habari? Mkuu Wa mkoa ndo angekuwa Wa kwanza kuwajibishwa ili anusuru raia!!!!!!
 
Mbona huko vijijini watu wanajichinjia tu jamani?
Huu ni uonevu mtu akitaka kumchinja mnyama wake lazima awe na kibari?
 
Nimeipata hii kutoka gazeti la raia mwema:

Mgogoro wa nani ana haki ya kuchinja umekuwa ukifukuta Mkoani Mwanza tangu Mei mwaka jana baada ya kulipuka wakati wa mazishi ya mzee Kamuli ambaye alikuwa muumini wa Kanisa la AICT Nyehunge. Katika msiba huo mchungaji wake, James Lutambi, alichinja ng'ombe kwa ajili ya kitoweo msibani.


Waislamu waliohudhuria msiba walihoji nani aliyekuwa amechinja wakaambiwa ni mchungaji. Wakataka kujua kwanini amechinja, yakatokea majibizano kidogo kabla ya waislamu kuondoka na kisha wakamwandikia Mtendaji wa Kijiji barua ya kutangaza kujitenga kushirikiana na wakristo katika misiba na sherehe.


Baada ya tangazo hilo, wakristo nao wakaamua kuwa na bucha yao. Baada ya kushughulikiwa katika ngazi mbalimbali za uongozi tangu katika kata hadi wilaya na kutopatikana suluhu, ndipo alipolazimika kwenda Mkuu wa Mkoa ambaye ni kama alikwenda kuuwasha moto zaidi badala ya kuutuliza.


Inaelezwa na baadhi ya wananchi wa Nyehunge kwamba Desemba 31, 2012 mchungaji Paul Range wa kanisa la EAGT alikamatwa na polisi na kuwekwa mahabusu kwa kosa la kuchinja ng'ombe machinjioni. Pamoja naye, mmiliki wa ngombe huyo naye aliwekwa mahabusu kwa kosa hilo hilo, tukio hilo lilisababisha pia Mkuu wa mkoa wa Mwanza kuamuru mtendaji wa kijiji cha Nyehunge kufukuzwa kazi kwa kushindwa kudhibiti uchinjaji huo.

Source: Raia Mwema

Yes ni kweli kabisa hii habari. Tena mchungaji aliandaa SAMAKI kwa ajili ya wale ambao hawatakuwa tayari kula hiyo nyama. Kwa wasioijua Nyehunge ni kijiji kule katika Jimbo la Buchosa la Mh Dr Tizeba
 
Ahaa, kosa la mchungaji ni kuanzisha bucha isiyo rasmi, na kuchinja bila kuhusisha daktari wa mifugo, at least labda ikiungwaungwa hivyo inaweza ikaleta mantiki kidogo ili kuonyesha tu kwamba wakristo nao walikuwa na makosa, lakini ukisema ni tuhuma za mauaji, ingekuwa mzaha.
 
Dah inavyoonekana kuna upotoshaji mkubwa sana wa kile kinachofanyika huko Mwanza... Ila naona hawa jamaa ni ukorofi tu ...uvumilivu huwa hawana......
 
kazi ipo kweli, mpaka kila mtu akubali kutulia! Mambo ya jazba hayo.
 
Kuanzia leo nitachinja mwenyewe kuku wangu hapa nyumbani..................kumbe ni ujinga wa njaa za watu zitutie shida
 
Baada ya kupata hii sababisho nimegundua tuna kazi kubwa ya kuelimisha vijana wetu kuheshimu imani za wenzao...Mnakumbuka yaliyotokea Mbagala watoto wanabishana mambo ya kitoto watu wazima wanatumia akili za panzi wanaharibu mali za watu bila hata kufikiri mara 2.......Tunahitaji kiongozi mkuu anayeweza kukemea kwa kusema hiki na hiki sikitaki na harudi nyuma kusema tofauti. Sio kiongozi anayetabasamu hata msibani huku wafiwa wakinyong'onyea kwa huzuni ya kumpoteza mpendwa wao. Lazima tuamke waTZ sura hazielezei mioyo ya watu.
 
Yes ni kweli kabisa hii habari. Tena mchungaji aliandaa SAMAKI kwa ajili ya wale ambao hawatakuwa tayari kula hiyo nyama. Kwa wasioijua Nyehunge ni kijiji kule katika Jimbo la Buchosa la Mh Dr Tizeba
aliandaa samaki gani maana samaki wanatofautiana ati!
 
sisi wa dar hatuna shida na mtu.Shida itoke wapi na wakati tuna samaki aina ya pweza;ni watamu,nyama yake laini, hawana mfupa, uhalali wake hauna shaka,wana nyama nyeupe, wanapatikana kirahisi na bei yake ni safi.Ka kipande shilingi 100, ya nini tupate shida na migogoro ya kipuuzi! Mungu wabariki wauza samaki na hasa hii aina ya pweza na wajalie maisha marefu na yenye baraka.Ngoja nikapate kabakuli ka mchuzi hapa jirani.
 
Mwanza mjini, maeneo ya Nyegezi. Mwaka jana kuna kijana alichinja kuku katika sherehe ya wakristu. Waislam wakataka kujua mchinjaji maana pia walialikwa. Wakaambiwa aliechinja, eeeh bwana wee vijana wavaa pedo na yeboyebo walimbeba juu juu mpaka kituo cha Police central, kisa amechinja! Jamani uhalali uko wapi?
 
Umoja wa makanisa ya kikristu jijini Mwanza yatamtetea, maana walishatoa tamko la kwamba wakristu wachinje kwa imani yao. Attachiwa huru tu hapo hakuna kesi ya kujibu. Wanajaribu kutaka kumuonyesha boss wao fastjet kwamba wanatenda kazi. Hakuna jipya hapo
 
huu ni upuuzi tu, haya tukubali kuwa mchungaji alichinja kinyume na sheria hasa kwamba hakuchinja maeneo yanayokubalika na umma, lakini je aliwalazimisha watu kuja kununua hadi wakavamia bucha? Je kuna uhusiano gani kati ya kuchinja maeneo yasiyo rasmi na kuuwa mchungaji?
 
kwa nini suluhisho la hili isiwe kuweka mipaka..ya kuwa kila sehemu kati ya haya makundi mawili kuchinja yake kwa utaratibu wao..badala ya kila mmoja kujiona kuwa yeye ni sahihi zaidi ya mwingine..ifike muda tuwe na uamuzi wa kujitegemea..
 
Back
Top Bottom