Mchungaji asema Mbowe ni tapeli hawezi kupigania Katiba Mpya itakayoleta ukomo wa uongozi wakati yeye miaka 20 na hana Mpango wa kuachia Uongozi

Halafu eti anataka kuing'oa CCM, hahahaa, wakati chama cha chadema, (chama chake), hakijafanya zoezi la kumng'oa yeye

Hawa viongozi wa vyama vya siasa wakipata nyazifa vyama vinakuwa vya kwao, haviwi tena vya wanachama
 
Yeye kasema hivi"

"....mimi ni mfanyabiashara mkubwa. Nina biashara zangu nyingi ndani na nje ya nchi...."

Ndiyo maana anataka achaguliwe tena na tena na tena na tena.....!

Jamaa (Freeman Mbowe) siku hizi is behaving very strangely. Hajiamini, hana hoja kabisa..

Na hana hoja kwa sababu malengo na agenda zinazoishikilia CHADEMA hazipo kwake tena, keshawauzia CCM na Mama Abdul...!!

Rushwa ni hatari. Rushwa huharibu na kupofushwa ufahamu wa kiongozi..

Freeman Mbowe rushwa imemmaliza kabisa lakini wakati huohuo anasema yeye ni "mfanyabiashara mkubwa". Kumbe ni biashara ya rushwa..

Okoa CHADEMA
 
Unapiganiaje kitu ambacho wewe hukiishi,mfano Nyerere alipingana na rushwa lakini yeye mwenyewe alikuwa mtiifu Na.1 kwa kutokula rushwa.
 
Mbowe hana hoja yoyote ya kutaka agombee tena, hoja yake ni kwamba hadi afikishe miaka 68 kama watangulizi wake, hiki ni kituko cha mwaka.

Mbaya zaidi anaulizwa ukomo wa uongozi anasema ukomo ni kama watu wanakukataa ama wanakukubali, sijui wakati anaongea haya alikua amelewa ama kutumia kilevi cha aina yoyote ama lah, sijui.

Kesho Mbowe ataongelea kweli ccm kung'ang'ania madarakani kwa miaka zaidi ya 60?
 
Wachungaji was mchongo
Huu ujumbe uwafikie wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CHADEMA ili wajue gharama ya kumrudisha Mbowe madarakani. CCM hawa hawa wanaomtetea Mbowe leo hii, ndio wataanza kukikashifu CHADEMA ya Mbowe. Huyu mchungaji kaanza kutuonyesha mapema ni nini itakuwa gharama ya kumchagua tena Mbowe.
 
Kwanini Chadema wanafanya uchaguzi kuelekea uchaguzi mkuu? huu ni wakati wa wao kuvurugana kweli?
Tatizo siyo chadema kufanya uchaguzi, bali tatizo ni Mbowe kung'ang'ania uenyekiti. Miaka 20 hataki kutoka.

2021 aliahidi kwamba 2023 kung"atuka lkn sasa kabadilika.

Anadai chadema ni mali yake, maana Ametumia hela yake kuijenga chadema. Rubbish!!
 
..Adv.Fatma Karume amesema UONGO.

..Ccm hawana ukomo wa madaraka ktk katiba ya chama chao.

..kwa kumbukumbu za haraka chama chenye katiba yenye ukomo wa madaraka ni ACT-wazalendo.
Uwe unasoma na kuelewa
 

[emoji3][emoji3][emoji3] Naomba Msigwa huko aliko atusaidie kupigania katiba mpya badala ya Mbowe [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Tatizo siyo chadema kufanya uchaguzi, bali tatizo ni Mbowe kung'ang'ania uenyekiti. Miaka 20 hataki kutoka.

2021 aliahidi kwamba 2023 kung"atuka lkn sasa kabadilika.

Anadai chadema ni mali yake, maana Ametumia hela yake kuijenga chadema. Rubbish!!

Ag’ang’anii madaraka bali anagombea kama wengine kikatiba sema tu labda kama wewe unakerwa na kushinda kwake kila anapogombea[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Yaani nikikumbuka akina Soka, Ali Kibao roho inaniuma sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…