Pre GE2025 Mchungaji Davina: Mungu amenionesha Uchaguzi wa 2025 hautakuwa wa kawaida

Pre GE2025 Mchungaji Davina: Mungu amenionesha Uchaguzi wa 2025 hautakuwa wa kawaida

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Mchungaji kutokea Kanisa la Pentekote, Davina Kahwa ameibuka hivi karibuni kuzungumzia uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika 2025.

Mchungaji huyo ambaye pia anatokea kwenye huduma ya uombaji wa kitaifa na kimataifa amedokeza kuwa uchaguzi huo unaokuja hautakuwa wa kawaida na kwamba

Uchaguzi wa mwaka 2025 utakuwa ni uchaguzi ambao haujawahi kutokea Tanzania. Sasa mtanzania, mtumishi wa Mungu tunahitaji kuwa na umoja. Watumishi wa Mungu wazee wetu ambao mmetutangulia hawa waumini tunawapeleka wapi?

Mchungaji huyo pia aliendelea kuhusu ukimya wa viongozi wa dini kwenye matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini

Kama mauaji yanaendelea hata kama atakuwa amekufa mtu mmoja maana ni kwamba atakuwa amekufa sio kwa mapenzi ya Mungu. Kwanini huyu mtu afe? Lakini sasa hivi tunaogopa hata kutembea. Nikwambie mtanzania, nikwambie mwana wa Mungu majira haya sio ya kukaa kawaida.

Source: Jambo TV
 
Kwani kuna uchaguzi uliowahi kuwa wakawaida? Kwanza wakawaida unakuwaje na usiokuwa wa kawaida upoje? Aseme labda kama atakufa mgombea au utafutwa au upinzani watashinda au nchi itapinduliwa lkn sio kusema utakuwa sio wa kawaida wakati kawaida yenyewe hatuijui. Litoke aseme nilisema. Huo ujanja ujanja hatutaki
 
Kwani kuna uchaguzi uliowahi kuwa wakawaida? Kwanza wakawaida unakuwaje na usiokuwa wa kawaida upoje? Aseme labda kama atakufa mgombea au utafutwa au upinzani watashinda au nchi itapinduliwa lkn sio kusema utakuwa sio wa kawaida wakati kawaida yenyewe hatuijui. Litoke aseme nilisema. Huo ujanja ujanja hatutaki
Mchungaji anamaanisha kuwa uchaguzi utakuwa wa wizi na utakumbwa na vurugu nyingi.
 
Wanapisema ni maono kutoka kwa Mungu wananiacha hoi!! Yeye ni nani ili Mungu ampe hayo maono? Ni huyu Mungu wa Israel au anaotokana na jadi yake? Angesema mizimu yake imemfunulia hapo sawa.
 
Mchungaji kutokea Kanisa la Pentekote, Davina Kahwa ameibuka hivi karibuni kuzungumzia uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika 2025.

Mchungaji huyo ambaye pia anatokea kwenye huduma ya uombaji wa kitaifa na kimataifa amedokeza kuwa uchaguzi huo unaokuja hautakuwa wa kawaida na kwamba

Uchaguzi wa mwaka 2025 utakuwa ni uchaguzi ambao haujawahi kutokea Tanzania. Sasa mtanzania, mtumishi wa Mungu tunahitaji kuwa na umoja. Watumishi wa Mungu wazee wetu ambao mmetutangulia hawa waumini tunawapeleka wapi?

Mchungaji huyo pia aliendelea kuhusu ukimya wa viongozi wa dini kwenye matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini

Kama mauaji yanaendelea hata kama atakuwa amekufa mtu mmoja maana ni kwamba atakuwa amekufa sio kwa mapenzi ya Mungu. Kwanini huyu mtu afe? Lakini sasa hivi tunaogopa hata kutembea. Nikwambie mtanzania, nikwambie mwana wa Mungu majira haya sio ya kukaa kawaida.

Source: Jambo TV
Mkajipange
 
Back
Top Bottom