Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Mimi nazan bora hata gwajima anayeweza kucmama na kukemea maovu ya serkar kuliko wachungaj na maaskofu wanafki wanaojifanya wanaliombea taifa aman wakat haki haipo.
 
Ndio yy ni zaid ya rais maana yy ni mtumish wa Mungu na mungu ni zaid rais ..kwanza wenye mamlaka ni wananchi na siyo rais
Mungu yup? Unamjua Mungu? Una ushahidi kuwa katumwa na Mungu?
 
Bw.Gwajima ana matokeo ya shule aliyosoma Bw.Daud Bashite yanayoonyesha Bashite alipata F zote.
Mwenyewe kashasema ata akipata zero ndo kashakua RC wenye wivu mjinyonge, najua wivu unawasumbua mmesota weeee mwishowe mnaambulia kuwa ma jobless
 
Mtumishi wa Mungu hupaswi kuwa muoga..
Gwajima sio kama wale wanaona mambo yanaenda mlama wakakaa kimya..
 
Hukumu ya Mungu ni tofauti na wanadamu, hatuwezi kuona watu wanafanya upuuzi kwa kisingizio eti tusiwahukumu, mbona wao wanahukumu watu, wao ni Mungu?
 
makonda kachokoa maslahi ya gwajima ulitaka gwajima atulie tu?
Gwajima anavuta bangi na madawa ya kulevya, nyie muangalieni tu akiongea na tabia yake, bangi bangi yani hana hekima ya Mungu, jamaa shetani sana
 
HIV tucta mko wapi kuwaunga mkono walimu tuache kucheka Cheka hali so nzuri kwa nini wasikamatwe waliokuwa wanalipa waeleze walikuwa wanamlipa nani hewa haiwezi kupokea malipo. kwa mini waumizwe wafanyakazi halali kwa kusema hewa. watanzania ebu kwa pamoja tupaze sauti zetu tutaua elimu yetu.
 
Kumbuka yesu kristo alivyokuwa akiwaita mafarisayo
 
Hajasema ana matokeo, amesema ana vyeti mezani kwake, hivi kweli kuna cheti cha divisheni 0 ya miaka hiyo?.

Paskali
Kaka Paskali, hapo ndipo utajua kuwa vijana wengi wa sasa wameharibikiwa vichwa kwa sababu ya bangi na "unga". Division 0 hapewi cheti, lakini watu wameshindwa kabisa kufikiria jambo dogo kama hilo!.
 
Yeye ni binadamu je unatuhumiwa kwa vitu ambavyo huvifanyi lazima uumie
Kwahiyo
 
Ndugu Pasco!

-Kwanza kabisa mimi niseme tu kwamba, Mtumishi wa Mungu yoyote yule hususani Mchungaji, ni mtu mwenye thamani kubwa mbele za Mungu, huyu ni Mkuu na ni bora na ni mtawala na ni mfalme kuliko Rais yoyote yule duniani.

-Nikueleze tu kwamba, mtu anayetawala roho ndie anayetawala mwili, mtu wa rohoni atamuendesha mtu wa mwilini anavyotaka yeye. Kama huamini basi fanya uchunguzi mmoja, mchunguze tajiri yoyote au boss yoyote yule ambae ana mganga wa kienyeji, yupo tayari kukosana na familia yake au hata wafanyakazi wenzie lakini awe na amani kwa mganga wake. Na kwa wanaowatumia Watumishi wa Mungu ni hivyo hivyo.

-Gwajima ni kiongozi wa kiroho (Iwe ni kweli Mtumishi wa Mungu au Lah), na kama ni kiongozi wa kiroho kwa nafasi yake yeye amepewa jukumu la kuongoza watu ili wafike kwa Mungu wao siku ya hukumu. Kazi ya Mchungaji ni ngumu kuliko hata Rais. Rais anaweza akaingia maagano na Mungu akataka kutandika nchi nzima ila viongozi wa kiroho wakasimana kuomba rehema na Mungu akarehemu. Rais hana nafasi ya kumsogeza mtu kwa Mungu ila Mchungaji anaweza.


SWALI YA KUJIULIZA!

KIPI NI CHA MAANA KWAKO, ROHO YAKO AU MWILI WAKO?
 
Pascal Mayyalla kuna mambo uko vizuri lakini hoja ulizojenga leo kwa suala hili zimepwaya sana. Hata rejea yako ya yesu kristo siyo relavant sana.
Binafsi nimefurahia statement za Gwajima 90% yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuusema ukweli na Gwajima kausema ukweli wake kosa lake liko wapi. Yesu aliwafundisha wanafunzi kumuogopa anayeua mwili na roho na Gwajima hamuogopi mtu wala cheo chake kawaambia ukweli. Kiroho Gwajima ni zaidi ya raisi wa nchi kama ilivyo kimwili raisi kuwa zaidi ya wote tz. Rais hutafuta baraka kwa viongozi wa dini kwanini kiongozi wa dini asiye zaidi yake. Mayyala usisome biblia kama gazeti la udaku au ukasoma kurani kama unavyosoma gazeti la mwanaspoti.
 
Mkuu, wachungaji wengi wa Afrika ni wasanii tu. Usidanganywe na yale yanayofanyika mbele za runinga, usidanganywe na mahubiri marefu. Wanafanya mengi machafu, wakiwa gizani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…