Mchungaji Msigwa: Hatuwezi kuwa na wachoyo wachache wanaoona ng'ombe wao na biashara zao muhimu kuliko Ngorongoro yenye maslahi ya Taifa

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
969
Reaction score
1,055

Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa zamani wa Iringa mjini na waziri kivuli wa maliasili na utalii ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Mwenyekiti wa chama hicho kanda ya Nyasa amesema kuwa pamoja na Tofauti zao za kisiasa na kupishana kwa mambo kadhaa ya hapa na pale, jambo moja muhimu ambalo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anapaswa kuwafanyia WATANZANIA na likabaki kama LEGACY kwake basi ni kuiokoa Hifadhi hii ya NGORONGORO ambayo inazidi kuteketea kutokana na ongezeko kubwa la watu, ongezeko kubwa la mifugo, ongezeko kubwa la Nyumba zisizoendana na uhifadhi ikiwemo ujenzi wa Maghorofa, ujenzi holela na hali mbaya ya maisha inayowakuta wananchi wanaoishi eneo hilo huku wale wanaojinasibu kuwatetea wakiishi maeneo nyeti na mazuri yenye huduma zote za msingi jijini Dar es salaam

"Hatuwezi kuwa na wachoyo wachache, ambao ng'ombe zao, biashara zao ziwe muhimu kuliko Ngorongoro inayoingizia mabilioni ya fedha zinazosaidia kupeleka huduma kwa jamii" amesema Mchungaji Msigwa

Mwalimu Nyerere alituachia urithi huu, ni wajibu wetu kuutunza, Serikali ya CCM imeshindwa kuutunza, na ndio maana tunaipinga na tunataka kuiondoa madarakani, haiwezekani watu wanajenga majumba hifadhini, wanazidisha mifugo nakadharika na CCM WAPO TU aliongeza Msigwa.

OKOA NGORONGORO
 
Ni kweli kabisa. Na hapa tunaona dhahiri kuna siasa za kimaslahi zinazunguka jambo hili nyeti. Na bila ya kusahau kulindana maana wanaofanya uhuni kule wanafahamika.
 
Naunga mkono hoja. Kwa nini wanaharakati wanafurahia binadamu wenzetu kuishi kama wanyama? Mwanadamu amepita stage nyingi za maendeleo kuanzia
Dryopithecus,
Ramapithecus,
Australopithecus,
Homo Erectus,
Homo Sapiens na hatimaye
Civilization

Kwa nini tunapenda watanzania wenzetu wabakie kama Sanaa ya kutazamwa na watalii? Kuna wamasai wako Handeni, Mvomero, Chalinze, mbona wanaendelea na maisha? Wengine wako Dar na Zanzibar wanafanya ulinzi, ususi wa nywele na kuuza sandalsWamasai watoke tu Ngorongoro
 
Kwa sababu wananufaika pengine na mifugo yao kupata malisho ya bure
 
Ni kweli kabisa.Na hapa tunaona dhahiri kuna siasa za kimaslahi zinazunguka jambo hili nyeti.Na bila ya kusahau kulindana maana wanaofanya uhuni kule wanafahamika.
Na kama wanafahamika washughulikiwe
 
Wewe ni mpumbavu. Kuna sehemu malisho ya ng'ombe wa kichungwa yanalipwa hapa nchini?
Zipo sehemu nyingi tu za kulipia....Majosho yanalipiwa, nyasi zinauzwa, madawa na mifugo inalipiwa...lakini pale Ngorongoro mtaji ni miguu yako tu kila kitu bure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…