Mchungaji!!

Kimey

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2009
Posts
4,117
Reaction score
833
Mgonjwa mmoja mahututi alikuwa
hawezi kuongea na kuwekewa oxgen.
Akawa anaombewa na Mchungaji.
Akiwa anaombewa, yule mgonjwa
akachukua kalamu na karatasi,


Akaandika na akampa yule Mchungaji. Ambaye
badala ya kuisoma ile karatasi, akaitia kwenye
mfuko wa joho na kuendelea na maombi hadi
yule mgonjwa, AKAKATA ROHO.

Mchungaji hakuisoma ile karatasi akijua kua

ni wosia wa marehemu. Akasubiri baada ya
mazishi kwenye kikao cha ndugu akasema;

"KUNA KITU NILIPEWA NA MAREHEMU SIKU
NILIYOKUA NAMUOMBEA"

Akampa mmoja wa wanandugu akisome.

Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa na
yule mgonjwa:
"UMEKANYAGA WAYA WA OXYGEN,
NAKOSA HEWA".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…