Mchuzi rahisi wa samaki na ugali

Mchuzi rahisi wa samaki na ugali

Wang Shu

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
2,562
Reaction score
3,715
Inafaa kwa mabachela kama mimi nimejipikia haraka sana bila kuchelewa nikala nikashiba mchana ukapita.

Mahitaji.
Chumvi
Mafuta
Kitunguu kimoja
Samaki wa kukaanga.
Nyanya (idadi uipendayo)

Jinsi ya kupika.
1.Katakata nyanya na vitunguu sehemu tofauti
2.Injika sufuria weka mafuta kiasi yaache yapate moto.
3.Tia vitunguu kaangaa kidogo ikifuatia na nyanya pamoja na chumvi.
IMG_20200722_133514.jpg

4.Funika iache zichemke kwa pamoja dk 10,koroga nyanya zivurugike vizuri tia samaki uache mchuzi uchemke tena upate radha ya samaki.
IMG_20200722_134333.jpg

5.Ipua tayari kwa kuliwa na ugali wako utafurahia mchana wako.
IMG_20200722_135813.jpg


Usisahau na juice mi nilikosa haraka zangu na njaa nikala na ndizi.

Karibuni ya kwisha.
IMG_20200722_141856.jpg
 
Vyombo unavyotumia kupikia ni vichafu. Halafu plastics si njema kuzitumia kama vyombo wa kuweka chakula
 
Vyombo unavyotumia kupikia ni vichafu. Halafu plastics si njema kuzitumia kama vyombo wa kuweka chakula

Maisha hayafanani kijana..nani amekwambia vyombo ni vichafu..nyie wa ushuani mna mbwembwe sana
 
Mkuu chukuchuku ya bamia, nyanyachungu (sio ngogwe), kitunguu na majani ya giligilani kula na ugali wa dona au muhogo; 800 tu mlo unakamilika
 
Back
Top Bottom