Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,761
- 216,011
Mchuzi huu hufaa wale wenye familia kubwa,
Mahitaji:
fungu moja la vibua,
vitunguu,
nyanya,
tomato paste,
limao,
chumvi, oxo.
Osha vibua toa utumbo na vichwa,
Weka limao na chumvi,
Chemsha kwa dakika kumi toa na uwache wapoe.
Wakipoa toa ule mwiba wa katikati na miba mingine ukiweza. Chambua minofu Ile ya samaki iwe kama nyama ya kusaga.
Kaanga kitunguu mpaka kiwe hudhurungi,
Kata nyanya vipande vidogo kaanga pamoja na vitunguu,
Ongezea pilipili (kama ni mpenzi),
Weka tomato paste, na minofu ya vibua, chumvi na limao, acha ichemke kwa moto mdogo kwa nusu saa.
Mchuzi huu huliwa na ugali au ugali wa muhogo.
Mahitaji:
fungu moja la vibua,
vitunguu,
nyanya,
tomato paste,
limao,
chumvi, oxo.
Osha vibua toa utumbo na vichwa,
Weka limao na chumvi,
Chemsha kwa dakika kumi toa na uwache wapoe.
Wakipoa toa ule mwiba wa katikati na miba mingine ukiweza. Chambua minofu Ile ya samaki iwe kama nyama ya kusaga.
Kaanga kitunguu mpaka kiwe hudhurungi,
Kata nyanya vipande vidogo kaanga pamoja na vitunguu,
Ongezea pilipili (kama ni mpenzi),
Weka tomato paste, na minofu ya vibua, chumvi na limao, acha ichemke kwa moto mdogo kwa nusu saa.
Mchuzi huu huliwa na ugali au ugali wa muhogo.