KALOKAGATHOS
Member
- Jul 9, 2013
- 38
- 6
Hapa TEKU kuna "mchwa" wanaotafuna pesa kila semester punde tu zitokapo HESLB.Boom tunalopata ni faida kutokana na pesa zetu.wafanyabiashara wakubwa wapo hapahapa chuoni,mzigo ukitua kutoka bodi hushambuliwa na mchwa hawa bila huruma,kule kwetu BUTURI kuna msemo usemao "kwoma itie e michiemie" yaani unapofanyia kazi ndipo unapopatia mlo.sasa hawa majamaa wanakula kwenye pesa zetu ambazo tutazilipa siku za usoni.hii ni wiki ya tano tupo field,tumesaini laki nne na themanini elfu tu,na hizo ndo pesa za mwisho kusaini kwa mwaka wa kwanza semester ya pili.kusaini zingine mpaka october au november ambapo kuja kuzipata ni december.wanazifanyia biashara kwanza mpaka waone wanachuo wanampango wa kugoma au kuandamana ndo wanatoa pesa hizo.kuna dubwana flani hapa TEKU ambalo lina jina la kutetea wanachuo lakini linachaguliwa na uongozi wa chuo,litaitwa TEKUSO,halina mbela wala nyuma,lipo tu,akina MLELWA ndo wametunisha mashavu yao humo na miwani ya ajabu.pesa zetu zinatafunwa na hao wapo tu.HESLB vipi huko MSASANI?