McLaren W1 Supercar yazinduliwa. Ndio itawarithi McLaren P1 na F1. Itauzwa Billion 5.7 za Kitanzania tu!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
McLaren Automotive jana tarehe 06 October wametangaza chuma yao mpya McLaren W1 wameipa codename P18.

Hii Plugin-hybrid itaanza kuuzwa mwakani 2025 na ndio itakayowarithi wakongwe P1 na F1 waliokuwepo tokea miaka ya 90s (F1) na miaka ya 2010s (P1).

W1 ni 2-doors coupé itakayokuja na gull-wing doors.

McLaren W1 ina 4.0L twin-turbo V8 hybrid engine inayotoa 928 hp, na 8 speed dual clutch transmission yenye electric reverse.

Hadi sasa, W1 ndio McLaren yenye acceleration kubwa kuwahi kuundwa, na inaenda 0-100 km/h ndani ya 2.7 seconds na 0-200km/h ndani ya 5.8 sec. Pia top speed inasemekana kua 350 km/h.

Bei ya W1 itakua approximately Billion 5.7 za Kitanzania na zitatengenezwa jumla ya gari 399 tu.
 
Kuna gari limited edition unakuta zinatengenezwa 10 tu Dunia nzima na baada ya hapo hawaruhusiwi kutengeneza zingine, 400 nyingi sana
yeap ni kama ndege tu. Kwa mfano sahivi kampuni ya boeing haitengenezi version ya B747.
 
Hiyo ndinga lazima niimiliki kama si duniani hata mbinguni ikibidi.
 
Kuna gari limited edition unakuta zinatengenezwa 10 tu Dunia nzima na baada ya hapo hawaruhusiwi kutengeneza zingine, 400 nyingi sana
Mnakua na group lenu la WhatsApp. Unajua mfano Ferrari ukitaka kununua gari lao jipya ni lazima uwe ushawahi kumiliki used Ferrari kwanza.

Na kuna baadhi ya model kama LaFerrari ili uinunue lazima uwe umeshawahi kununua Ferrari nyingine mpya kabla.

Tutafute hela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…