Pre GE2025 Mdahalo wa wagombea Urais wa TLS ulikuwa "fantastic". Wagombea Urais Uchaguzi Mkuu 2025 waige mfano huo

Pre GE2025 Mdahalo wa wagombea Urais wa TLS ulikuwa "fantastic". Wagombea Urais Uchaguzi Mkuu 2025 waige mfano huo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Nilishuhudia mdahalo wa wagombea Urais wa TLS, uliofanyika katika kituo Cha luninga Cha Star TV, ukiongozwa na mtangazaji wao mahiri, Chifu Odemba, ulioendeshwa Kwa takribani masaa mawili na nusu, ambao ulikuwa mzuri sana na wa kiwango Cha kimataifa, ambao uligusa Kila aina ya nyanja ya taaluma hiyo ya sheria na Taifa Kwa ujumla.

Ningependelea na naamini watanzania walio wengi, ndivyo watakavyopendelea kuona mdahalo wa aina hiyo, Kwenye uchaguzi Mkuu wa mwakani wa wagombea wa vyama vya siasa mwakani, ukiendeshwa na kituo hicho, chini ya mtangazaji nguli Chifu Odemba.

Hata hivyo najua kuwa kulifanyika juhudi kubwa miaka ya nyuma, Kila ilipofika wakati wa uchaguzi mkuu, kuwataka wagombea wa vyama vya siasa, washiriki Kwenye mdahalo wa aina hiyo, lakini kizingiti kikubwa ilikuwa chama Cha CCM, ambacho kimekuwa kikiukataa mdahalo huo!

Ninaamini pia kupitia Kwenye mdahalo huo, ndipo tutawajua wagombea Urais wa vyama mbalimbali, kuhusu sera zao na namna watakavyokabiliana na uongozi na namna ya kuliletea maendeleo makubwa Taifa letu

Tutambue pia kuwa ni Karibu mataifa yote duniani, yanatumia mtindo huu wa mdahalo wa wagombea Urais, Kila inapofika nyakati za uchaguzi.

Mathalani tulishuhudia hivi karibuni huko nchini Marekani, wagombea Urais wa vyama vya Democrats, Joe Biden na mwenzske wa Republican, Donald Trump, wakichuana vikali katika mdahalo huo, ambao hatimaye umemuweka pembeni mgombea Urais wa chama Cha Democrats, Joe Biden, baada ya kufanya vibaya Kwenye mdahalo huo, sababu zikielezwa kuwa ni kutokana na umri mkubwa.

Hivi bila mdahalo huo, nchi ya Marekani ingeweza kuwa na mgombea Urais wa Chama Cha Democrats, Kamara Harris??

Jibu ni Hapana

Kwa hiyo Kwa kuwa tunajua umuhimu mkubwa wa kuwa na Rais Bora kwa Taifa lolote ni jukumu kubwa sana Kwa maendeleo ya wananchi wa Taifa husika, Kwa hiyo naamini upo ulazima wa kuendesha mdahalo wa aina hiyo, Ili tuweze kuwapima wagombea wetu wa Urais, tunaotegemea kuwapigia kura, Ili waweze kuliongoza Kwa weledi mkubwa Taifa letu.

Mungu ibariki Tanzania

Pia, soma: Mdahalo wa Wagombea Urais wa Chama cha Mawakili Tanzania Bara 2024
 
Hawataweza, CCM ni Wakomunisti uchwara, wewe umeshawahi kuona mdahalo Urusi au China?!

Modahalo ni kwenye Nchi za kidemokrasia sio hawa wezi wa Chaguzi.
 
CCM hawata kubali
Ni lazima wakubali, Kwa kuwa hatuchagui Mwenyekiti wa chama Chao, Bali tunachagua Rais wa nchi.

Kwa kuwa ni sisi wananchi tunaoutaka mdahalo huo, hawana budi kuukubali😀
 
Sio hii ccm ninayoijua. They're baseless hawawezi hata kidogo kuji~engage na midahalo
 
Ningependelea na naamini watanzania walio wengi, ndivyo watakavyopendelea kuona mdahalo wa aina hiyo, Kwenye uchaguzi Mkuu wa mwakani wa wagombea wa vyama vya siasa mwakani, ukiendeshwa na kituo hicho, chini ya mtangazaji nguli Chifu Odemba.
Mtego huo!
 
Hizo porojo ndio mnaziweka , hamtokuja kupata maendeleo ng'o kwa kubwabwanya midomo ...Moja ya vitu vya kijinga kabisa kufuatilia hizo sheria zenyewe ni kukariri tu .

Wenzenu wapo kweny exhibition kubwa za teknolojia nyie maneno kibao .
 
Midahalo ya kisiasa hususani siasa zetu midahalo bado sana, tutashuhudia vituko vya aina yake.
 
Midahalo ya kisiasa hususani siasa zetu midahalo bado sana, tutashuhudia vituko vya aina yake.
Unasema Kwenye nchi yetu, midahalo hiyo bado sana, hivi unadhani lini midahalo hiyo itakuwa muda muafaka, Kwa nchi yetu??

Ni chama Cha CCM pekee, ndicho "kinachokacha" midahalo hiyo😀
 
FANYENI MIDAHARO YOTE LAKINI MSIJE WEKA MDAHALO WA URAIS. MSIJARIBU HUKO. ALIYEKUWA NA AKILI HIYO ALIKUWA NI NYERERE NA MKAPA TU. HAWA WALIKUWA SMART KICHWANI.
Unataka kusema hawa hawako smart kichwani?
 
Nilipata nafasi ya Kufuatilia kidogo, it was very interesting, na kwa asilimia kubwa wale wagombea wapo vizuri kichwani japo kuna kuzidiana.
 
Back
Top Bottom