Mdau: Mlitaka Rais afanye nini kuhusu tozo ya miamala ya simu?

Waanze wao kwanza kwa mwaka huu wabane matumizi hakuna kutembelea magari ya gharama waishi maisha kama ya kwetu sisi then mwaka wa pili walete sasa hizo tozo tutatoa kwa moyo mkunjufu. Sio tunabanwa kwenye tozo wao kutwa viguu na njia wapo safarini wanakula posho hapo hatutaelewana
 
Hatukatai hizi tozo,waangalie ukubwa wa tozo.mfano anaetuma 10000 wangechukua (500)tu hadi anayetuma200000. 2000 kwa 210000 hadi 600000 (2500) kwa610000 hadi 1,000000 (3000)kwa 1,001000 na kuendelea
 
Rais kasema na yeye ameona ni kubwa sana andaa andiko lingine.
 
Hatukatai hizi tozo,waangalie ukubwa wa tozo.mfano anaetuma 10000 wangechukua (500)tu hadi anayetuma200000. 2000 kwa 210000 hadi 600000 (2500) kwa610000 hadi 1,000000 (3000)kwa 1,001000 na kuendelea

Na Hilo ndilo linakwenda kutizamwa, Mwalimu Nyerere alisema ni lazima tuchukue kodi lakini kwa wakati ule alisema kwa sasa sichukui toka kwao kwakua hawana kitu, maana yake ni kwamba serikali itazingatia hali za wananchi
 
😂😂😂😂Suluhisho la kutoka kwenye mtikisiko wa kiuchumi ni kuongeza kodi?
 
Mama umeongea vizuri sana kwenye kukusanya, vipi kwenye matumizi na vyanzo vipya visivyo na mawaha.

Mmepanga bajeti ya 2020/2021 zaidi ya 33t, Sasa kwenye matumizi ya kawaida ni zaidi ya 20t na matumizi ya maendeleo ni zaidi 13t inakuja kuona matumizi ya kawaida ni 3× ya matumizi ya maendeleo maana yake nini serikali ina matumizi mengi yasiyoenda moja kwa moja kwenye maendeleo zaidi ya kulipa mishahara,posho na Mambo mengini Sasa je kwa namna hiyo ndio mmekuja kutaka nyongeza ya pesa kwenye matumizi yenu ya kawaida? Kwa gharama ya jasho la walala hoi?

Vyanzo vipya vya mapato ina maana ubunifu na mawazo yenu yameishia kwenye tozo na Kodi kandamizi? Mfano kwanini tusitumie PPP kwenye kuwekeza vyanzo vipya itakavyoleta mapato zaidi pasipokutumia jasho la mlala hoi i.e summer beach parks kwenye pwani yetu, migodi kwenye madini yetu, wazo Kama la badamoyo likaboreshwa tutapata pesa nyingi sana na ajira pia kusisimua uchumi

Kutengeneza sera na sheria rafiki kwa uchumi na uwekezaji ili kuvuta zaidi uwekezaji utakakaochochea uchumi na mzunguko wa pesa ili kupunguza kubana Kodi mpaka kwenye maeneo yanayoumiza hali za wananchi
Kwa kumalizia mlituambia tuko uchumi wa kati ina maana umedondoka kwa miezi 3, je ile style ya kununua madege cash vipi au ndio ile report magumashi ya BOT imekuja kuwastua kuwa hazina hakuna hela mkaamua mje na mkakati wa kutunyonya
Jamani muwe na huruma watanzania wengi ni masikini, vijana hawana ajira hakuna wakuwasemea maana wabunge wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi, CCM ipo busy kupiga propaganda sio kutoa majibu ya matatizo
 
Hatukatai, ila tozo zilizowekwa hazilipiki. Mitandao wenyewe wameona ada iwe 8000 kwa muamala wa milioni moja. jamaa na tozo zao juu yake wanaongeza zaidi ya 8000. Narudia zaidi ya 8000, unaenda makato zaidi ya mara mbili kwa muamala,hata ilipoongezwa ile ya benk haikuenda hivo. Its too much. Raia tunalipa kodi nyingi sana kama Value added Tax. Zitumike vzur na kila jambo litakuwa sawa.
 
Ningekuona wa maana Sana ungesema mishahara ya wabunge,wakuu wa mikoa na wilaya ma RAs,DAS,DED ipunguzwe kwanza na posho zao,ili tuwe wamoja kuliko hicho unachotetea.
 
Afanye nini ?
Kwamba hii Kodi ni muhimu kwa maendeleo ?
Je unajua kwamba huenda hizi Tozo zikapunguza watuamiaji hence kukosa hata walichopata mwanzo ?

 
Wasikilize maoni ya wadau kwanza ,wananchi wanaochangia hiyo tozo ndio watoe maoni yao wanataka iwe vipi ,hatukatai tozo ila iwe reasonable , maendeleo ni muhimu sana ila yasiwaumize wananchi na pia yasiathiri uchumi.

Yaani kutoa Tsh elfu 10 unakatwa Tsh 2000? Really? Makato ni makubwa sana!! Serikali ibanane na makampuni ya simu kuchukua kodi zaidi kwenye yale makato yao maana wanapata faida kubwa sana!!
 
Tukipunguza milioni mbili kwa wabunge 376 tunapata sh ngapi? Mara miaka mitano?
Tukiondoa milioni moja kwa Kila DC na DED katika wilaya 126 za TANZANIA nzima Mara 12 Mara miaka 5 tunapata sh ngapi?
2000000 Mara 126 Mara 2 Mara miezi sitini,tunapata sh ngapi? Wewe mleta bandiko? Piga hesabu hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…