dawa yenu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 2,825
- 3,675
messi atapiga goli mbili takatifu huku neymer akiweka kimiani goli moja lililojaa ufundi wa kutosha na kuisisimua jumuiya ya wapenda soka duniani. Goli la Neymer litatokana na pasi bora kabisa kutoka kwa fundi wa mpira duniani yaani messi. Goli la kwanza ambalo litafungwa na Messi katika dakika ya kumi na sita litatokana na pasi nzuri kutoka kwa suarez ambaye atafanya maajabu mengi sana uwanjani ambayo ni nadra kuyashuhudia katika kizazi, hakika itakuwa gumzo kubwa duniani. Dakika tatu kabla ya kipindi cha kwanza kuisha fundi Iniesta atapiga pasi ndefu kutoka katikati ya uwanja na pasi hiyo itamfikia Messi ambapo atafanya manyanga pale na kiwatoka mabeki takriban watatu na kutupia wavun goli moja la ukweli sana. kwa upande wa juve watacheza jihad na kubahatika kupata goli moja ambalo halitaeleweka limefungwaje maana itakuwa ni butua butua tu hamna ubunifu, ufundi wala umaridadi wowote, hiyo ni katika dakika ya themanini na mbili ya mchezo. Hivi ndivyo itakavyokuwa.