Mechi ya fainali Esperence vs Wydad casablanca yatuvua nguo waafrica.

Manofu

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2018
Posts
1,317
Reaction score
2,020
Jana bwana pale Tunisia ulipigwa mtanange wa fainali ya pili baada ile ya kwanza iliyochezwa wikimoja iliyopita kule morrocco kuisha kwa 1-1. Kwenye ile mechi ya mkondo wa kwanza lilifungwa goli la utata VAR ikafanya kazi sawasawa, kituko kwenye mechi ya marejeano ya jana usiku Esperence walitangulia kufunga goli wydad wakachomoa kwa goli la kichwa refa akasema ni offside ikabidi wakarejee kwenye VAR kufika kwenye VAR eti ikagoma kufanya kazi. Refa akawaita wydad waludi kuendelea na mpira wydad wakagoma refa akasubili dakika kumi na tano wydad wakagoma kabisa kuendelea na mchezo, CAF wakaipa ubigwa Esperence. Yani mpira wa africa ni ovyo ovyo sio TFF wala CAF wote ni watoto wa baba mmoja.
 
Aisee bora fainali iwe inachezwa kwenye neutral ground wanaweza wakaamua mwaka ujao ifanyike Tanzania au Gabon au nchi nyoyote yenye uwanja mzuri lkn ili swala la fainali kuchezwa nyumbani na ugenini ndo tatizo kubwa, ata kama kisingizio ni mashabiki kutokuja viwanjani kama ilo litapitishwa ila ni bora mashabiki wasije ila fainali iwe ya haki.
 
var waliizima makusudi maana esperence alikuwa nyumbani. na lile goli lilikuwa linamuua esperence. wahuni wakaizima.VAR fasta
sina uhakika kuzima kwa makusudi au hapana ila correction lingekuwa goal ingekuwa wako draw maana mechi ya kwanza pai ilikuwa moja kwa moja.
 
hata champions league ya america fainali ni 2.. kina neymar wamezicheza sana hizo.... hata champions league ya asia fainali ni 2.... ulaya peke yake ndiyo wana 1 final
Nadhani ni kutokana na uwezo wa watu wa Africa na S.America. watu hawana pesa au usafiri wa kutosha wa kusafirisha maelfu ya watu hata Hotel hakuna tofauti na wenzetu wa Ulaya uwezo wa kipesa wanao na miundombinu inaruhusu na zaidi hakuna visa free japo S.America pia hakuna visa lakini umaskini tatizo. ila ni vizuri kuwa na final moja tu. kwa jana ilikuwa aibu sana team kutoka uwanjani hapana. Ulaya kabla VAR kulikuwa na ma goal ya utata sana tena sana lakini huwezi kuona team inatoka uwanjani. kwa jana Africa tumepata aibu kubwa sana tena sana.
 
sasa wao walikuwa hawataki liwe goli.. ili washinde
ndio maana nasema tuchukue mfano hakuna VAR mwaka jana kweli team katika final kubwa africa unatoka uwanjani? tumeona mangapi ulaya magoal mazuri yanakataliwa na offside goal lakini refa anaheshimiwa na game inaendelea mambo ya kutoka uwanjani ya kizamani sana ni aibu jana.
 

wydad wamekasirika sababu kwao walikataliwa goli... na pia kama sheria imesema kuna VAR.. why kwenye goli lao la kusawazisha waseme VAR mbovu..

caf wamejichanganya sana kuweka VAR ... walipaswa waseme haipo kabisa ili kila anaecheza ajue haipo..

ila ukisema VAR ipo.. mwingine ukamkatalia goli.. mwingine ukampa goli.. hapo inakuwa double standard
 
hata champions league ya america fainali ni 2.. kina neymar wamezicheza sana hizo.... hata champions league ya asia fainali ni 2.... ulaya peke yake ndiyo wana 1 final

Kumbe tunaendesha mashindano kwa kufuata mkumbo?
 
Nimeshangaa bin kushangaa. Africa tuna matatizo tena makubwa. Eti VAR haifanyi kazi fainali jamani. Halafu mechi ya kwanza i.e first leg ilichezwa saa saba usiku ya Tanzania. Kule penalt ilikataliwa,captain akalimwa red card. Jana napo lille lilikuwa goli,likakataliwa. Inshort Esperance alipangwa ashinde njoo mvua njoo jua. Africa is shit continent.
 

esperence kabebwa toka game ya kwanza ya fainal ndio maana wydad wakasusa... hata nusu na mazembe esperence alibebwa sana
 
Wanasema eti washabiki Africa hawana tabia ya kusafiri. Wanaangalia kuuzika kwa ticket zaidi. Hata mimi naungana na mawazo yako. Halafu wafanye fainali moja tu.
 
Wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…