Mechi ya Kirafiki: Simba vs Mwadui

Hivi simba ipo?
Simba bado ipo mkuu Deo Corleon ila sio simba ile unayoifahamu wewe, Simba ya sasa hivi sio ya timu ya mpira wa miguu, simba ya siku hizi ni ya kundi la wasanii waimba taarabu na mipasho akina Hajji Manara, akina Hans Poppe na wasanii wengine.
Ukishangaa ya Danny Serrunkuma utayaona ya Papa Niang kutoka Senegal.
 

Asante kwa taarifa Mkuu.
 
Last edited by a moderator:


Hii ndio tofauti ya wapenzi wa mpira na wanazi. Ukweli unasemwa kama ukweli badala ya kusifia kitu ambacho hakina maana. Kula tano mkuu!
 
Usijifariji kwa vijimaneno uchwara, wa kimataifa wapo na wa mchangani wapo hapa hapa Tanzania. Ukweli unauma, lakini hakuna jinsi!


Ukweli ni kuwa ni timu moja tu Tanzania ndiyo inayojulikana na mamilioni ya Watanzania na Waafrika wengi kuwa ni ''Ya Kimataifa', lkn ni ukweli pia kuwa kuna timu inajitambulisha kwenye mitandao kuwa ni ya kimataifa!!!!
 

kama ccm vile
 
Basi farijianeni kwa maneno hayo (1 Thes. 4:18) <https://www.wordproject.org/bibles/sw/52/4.htm>


Mkuu Matale tatizo sio mimi; ni mamilioni ya Watanzania ndio wana-associate timu moja na mafanikio ya kimataifa (watu wa marketing wanaweza kulielezea vzr hili) wakati huo huo wana associate timu nyingine na mafanikio ya ndani. Huu ni ukweli mchungu lkn kama ni dawa watu hawana budi kuinywa tu.

Lkn angalizo, sijazitaja hizo timu ila unachokifikiria ndicho basi ujue ndicho.
 

Unavyodhani mikia hawalijui hilo,wanalijua sana sema wanajitoa ufahamu tu😀
 
Matokeo ya leo: Simba 0-0 Mwadui FC. Hakuna cha Niang wala mikia wengine!

Julio: Simba bado sana, mashabiki wasitegemee jipya watabaki vile vile tu kama msimu uliopita na misimu mingine iliyopita.

CC. Masuke, sembo, Katavi et al.

mkuu Kwan msenegal kucheza?? maana nashangaa kuona ukimya toka kwa kwa wanaz wa mikia fc tofauti na jinsi walivyokuwa wanaipa promo hiyo mechi ya kirafiki utadhan ni fainali ya CAN

Hivi simba ipo?


Wakuu zangu, kwa heshima na taadhima naomba niwataarifu, jana Azam FC walikua dimbani kupambana na Mwadui.. matokeo ni 1-1.
Simba SC ilipodraw na Mwadui mliongea sana.. Mara Simba bado sana.. Hivi Simba mpo?.. Mara Simba siku hizi ni kundi la waimba taarabu.. n.k

Nahitaji kauli zenu pia kuhusu mechi ya Azam na Mwadui.
 

First Eleven ya Azam FC iko Uturuki, Mwadui FC wamecheza na jina tu la Azam. Tusubiri ligi ianze utaniambia Mkuu.
 
kama simba ilishakufa limebak jina mbona kila tukikutana na nyie yeboyebo daily tunawagonga
 

Msimu uliopita hao wote uliowataja walikuwepo mlishika nafasi ya ngapi ? Kwa hilo la kila krosi 80% goli je mmetoa mfungaji bora kwa average hiyo?

Mtani kubalini kuwa Simba kwa sasa kurudi katika form inahitaji juhudi na maarifa binafsi ya wachezaji na si kocha wa benchi la ufundi. Timu mliyokuwa mnaijenga miaka michache iliyopita ingekuwepo leo mngekuwa tishio sana. Ila poor planning na kukomoana katika klabu ndiyo kinachowaponza.

Hai wachezaji wapya mliochukua na huyo kocha mpya itahitaji muda sana kuwa na timu imara na tishio, najua matokeo mabaya yanawafadhaisha ila huo ndio ukweli vumilieni tuu.

Washaurini viongozi wenu kuwa teamwork ndio mpango mzima, jengeni kwanza umoja na mshikamano kwa viongozi wenu pia huyo aveva chapeni hata viboko kumi ili aache kuindesha simba kwa makundi hapo mtapata mafanikio.

Inaniuma sana kuona eti leo mtani wa jadi anakuwa shost yenu Azam, jaribuni kuweka mambo sawa ndani ya club yenu, ili ile heshima ya utani wa jadi urudi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…