Mechi ya Yanga FC Vs TP Mazembe - Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

Hakuna neno Ripoti kwenye Kiswahili. Ninyi mkoje? Yaani hamjui lugha zote mnazozungumza. Kuna ugumu gani kusema Taarifa? Ndo veelazer wa Udom .

QUOTE="FaizaFoxy, post: 16672208, member: 43551"]= ripoti[/QUOTE]
 
Kazi nzuri sana Mazembe. Umbwa wako kimya saa hii. Hahahahah wa Kimataifa au matopeni?
 
No, Yanga leo karuka ruka kama Chura mwishoni kabisa kafungwa!

Kama Chura wa Snura aliruka ruka then akaingia gereza la TCRA!
Mmh!!! Hahahahaaa mna visa nyie. Hata hamjionei huruma masikini, mko matopeni. Siye wa Kimataifa haswaaaa...
 
Uwezo wa kuingia hamna mmeingizwa bure, siye yetu yanatuendea. Kufungwa ni sehemu ya mchezo. Tuwaulize nyie paka wa matopeni. Sisi habari yetu ndio hiyo...
CAF inaidai Yanga sh. 530M kadirio la mapato ili ikate asilimia zake
 
CAF inaidai Yanga sh. 530M kadirio la mapato ili ikate asilimia zake
Wewe bwana hebu acha kwanza wa kimataifa waliofumuliwa kamoja kwa shiiida wapate kupumua japo kwa huu usiku wa leo wakijikanda kupoza maumivu
 
Asanteni sana TP Mazembe kwa kutunyamazishia jiji na taifa kwa ujumla!!!
Yaani hawa jamaa tusingelala kabisa maana wangegeuka popo kuanzia Taifa mpaka Morogoro. Poleni watani zangu maana mmepigwa kamoja tu ka hamu
 
Hata huku barabarani sisikii makelele yao huenda bado kamoja kamewauma
 
Yanga ninayoifahamu mimi...bila refa kutoa ushirikiano matokea huwa kama hivi..!!hakuna penati za bure wala red cards. huwa inabaki tulicheza mpira mwingi japo ball posessions ni 47 % Yanga na 57% TP Mazembe.Kobe yupo mtini tunajiuliza amefikaje
 
Yanga anatoka jasho Simba anapata raha, Sasa nimejua kwa nini mwanamke kwenye sita sita hata mechi iwe Kali Kiasi gani lakini hatoki jasho.!
kwani hilo bao moja kapigwa Nani jioni hii ?
 
Yaani hawa jamaa tusingelala kabisa maana wangegeuka popo kuanzia Taifa mpaka Morogoro. Poleni watani zangu maana mmepigwa kamoja tu ka hamu
Mi nataka kusikia tambo za yule msemaji wao sijui wanamwita muru sijui mura ah watajua wenyewe.
 
Hii inaitwa ringa tena...au unaimba " amerudi analia eeh..... Anatia huruma....mtanzania mwenzetu ametutoa kimasomaso
 
Mi nataka kusikia tambo za yule msemaji wao sijui wanamwita muru sijui mura ah watajua wenyewe.
Atamtambia nani, maneno mengi kama kasuku lakini vitendo hakuna maana hawa raia wanaolilia kujenga uwanja bondeni kwenye mafuriko ambako NEMC wamekataza hawana sera
 
Hii inaitwa ringa tena...au unaimba " amerudi analia eeh..... Anatia huruma....mtanzania mwenzetu ametutoa kimasomaso
Duu ama kweli leo mwali kapatikana, hivi huu wimbo ulikuepo au umeutunga leoleo kifree style baada ya matokeo.
Wakimataifwa hoi hoyyeee!
 
Jenny Murua yeye anachofurahia ni kupanda ndege nadhan siku akiacha kuwa msema chochote wa yanga huyu dada akawe air hostess huko ndo atapanda sana ndege.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…