TANZIA Meja Jenerali Mstaafu Martin Shiminzi Busungu afariki dunia

TANZIA Meja Jenerali Mstaafu Martin Shiminzi Busungu afariki dunia

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametangaza kwa masikitiko kifo cha Meja Jenerali Martin Shiminzi Busungu (Mstaafu), kilichotokea tarehe 24 Disemba, 2024 majira ya saa 10:15 jioni wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Enzi za utumishi wake Jeshini Jenerali Busungu aliwahi kushika madaraka mbalimbali yakiwemo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa mwaka 2018 hadi 2019.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Kanali Gaudentius Gervas Ilonda, taarifa za utoaji wa heshima za mwisho kwa marehemu na shughuli za mazishi zitatolewa baadaye.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali Pema Peponi, Amina.

Screenshot 2024-12-25 002335.png
 
Rest In Eternal Peace General. This so called death...does not recognize even the hard-core soldiers. Men with decorations all over their shirts.
Mbele yetu, sisi twaja mdogo mdogo
 
Mwenyezi Mungu awafariji wafiwa wote
 
Dah, Mungu aipumzishe roho yake pema peponi na aipe faraja nyingi sana familia yake.

Kufariki wakati wa kipindi cha sherehe za krismas kunaiacha familia na kovu kubwa sana kwani siku za mbeleni hawataweza kusherehekea krismas tena bila kumkumbuka jenerali.

Siku Hayati Magufuli anampandisha cheo Hayati Mbuge kuwa Brigadia generali, Hayati Busungu alikuwa mkuu wa JKT na ndiye aliyenza kumpa mkono wa hongera Hayati Mbuge kwa kupandishwa cheo.

Mola wetu, ikikupendeza, ziwekeroho za mashujaaa wetu hao pema peponi.
 
Back
Top Bottom