Meli mbili Ziwa Nyasa zakumbwa na dhoruba kali

Meli mbili Ziwa Nyasa zakumbwa na dhoruba kali

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
3 May 2021
Matema Beach,
Tanzania

MELI ZA TANZANIA ZAKUMBWA NA DHORUBA KALI KTK ZIWA NYASA

Kutoka Ziwa Nyasa meli mbili zinazomilikiwa na Mamlaka ya Bandari ya Tanzania zimekumbana na dhoruba kali inayoambatana na mvua kubwa.



Meli ya abiria MV Mbeya II imepigwa na mawimbi makali jioni hii huku ikiwa na abiria 87, maofisa na mabaharia 25 na kusukumwa mpaka Pwani na kukwama. Uwezo wa meli ya MV Mbeya II ni abiria 200 na mizigo tani 200.

Meli hii MV Mbeya II yenye mitambo ya kisasa kama echosounder, GPS, Radar , magnetic compass, spidi 11 knots na ni meli aina ya landing craft inayoweza pia kushusha mizigo na abiria popote kusipokuwepo na gati.

Meli nyingine ndogo ya mizigo MV Songea pia inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari ya Tanzania TPA imekumbwa na mawimbi makubwa makali muda wa mchana na kunasa ktk pwani ya mchanga (fungu) kutokana na hali mbaya ya hewa yenye upepo mkali na mawimbi makubwa.

Mkuu wa wilaya Kyela nchini Tanzania na kamati yake ya ulinzi na usalama,wamethibitisha kadhia hiyo iliyozikumba meli hizo mbili zinazotoa huduma katika ziwa Nyasa.

Meli ya MV Mbeya II ilizinduliwa mapema mwezi Januari mwaka huu 2021 kuanza safari ktk ziwa Nyasa WAZIRI MKUU azindua meli mpya ya abiria ya MV Mbeya II katika ziwa Nyasa

Source : millard ayo

Jamvi online tv Meli ya MV Mbeya II inaudwa baada ya meli ya mwanzo ya MV Mbeya I kuzama mwaka 1975 eneo la Makonde wakati ilipokuwa ikifanya safari zake za kawaida katika ziwa hilo. Source : UJENZI WA MELI MPYA YA ABIRIA MV MBEYA II KATIKA ZIWA NYASA WAFIKIA ASILIMIA 82, AWAMU YA TANO NI VITENDO TU | Full Shangwe Blog


N.B
Utabiri hali ya hewa
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania tarehe 3 May 2021



Source : meteo tanzania
 
Duniani sehemu nyingi upepo ni mkali sana ni kujihadhari
Ila mamlaka ya hewa naona wamelala
 
Inawezekana Jobo bdo alikuwa hajaondoka. Au la kuna tetemeko la chini ya ziwa. Watu wa miamba na bahari ndio wakati wao kutuambia
Labda dragon alikuwa anakamatwa siku hio ikapelekea dhoruba
 
3 May 2021
Matema Beach,
Tanzania

MELI ZA TANZANIA ZAKUMBWA NA DHORUBA KALI KTK ZIWA NYASA

Kutoka Ziwa Nyasa meli mbili zinazomilikiwa na Mamlaka ya Bandari ya Tanzania zimekumbana na dhoruba kali inayoambatana na mvua kubwa.

Meli ya abiria MV Mbeya II imepigwa na mawimbi makali jioni hii huku ikiwa na abiria 87, maofisa na mabaharia 25 na kusukumwa mpaka Pwani na kukwama. Uwezo wa meli ya MV Mbeya II ni abiria 200 na mizigo tani 200.

Meli hii MV Mbeya II yenye mitambo ya kisasa kama echosounder, GPS, Radar , magnetic compass, spidi 11 knots na ni meli aina ya landing craft inayoweza pia kushusha mizigo na abiria popote kusipokuwepo na gati.

Meli nyingine ndogo ya mizigo MV Songea pia inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari ya Tanzania TPA imekumbwa na mawimbi makubwa makali muda wa mchana na kunasa ktk pwani ya mchanga (fungu) kutokana na hali mbaya ya hewa yenye upepo mkali na mawimbi makubwa.

Mkuu wa wilaya Kyela nchini Tanzania na kamati yake ya ulinzi na usalama,wamethibitisha kadhia hiyo iliyozikumba meli hizo mbili zinazotoa huduma katika ziwa Nyasa.

Meli ya MV Mbeya II ilizinduliwa mapema mwezi Januari mwaka huu 2021 kuanza safari ktk ziwa Nyasa WAZIRI MKUU azindua meli mpya ya abiria ya MV Mbeya II katika ziwa Nyasa

Source : millard ayo



N.B
Utabiri hali ya hewa
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania tarehe 3 May 2021



Source : meteo tanzania
Utabiribwa hali ya hewa - Mbeya,, ni mawingu na mvua katika maeneo machache.
Lakini naamini pale bandaruni kuna kitengo cha hali ya hewa. Huenda walicopy huo wa kwenye TV.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
03 June 2021
Kyela, Mbeya
Tanzania

Mengi yabainika MV Mbeya ilizinduliwa kabla ya kukamilika


Naibu waziri Mwita Waitara awa mbogo baada ya kugundua mapungufu mengi yalikuwapo ila wanasiasa waliingilia mchakato wa kiufundi na usalama wa chombo haujamalizwa.

Kufuatia kubainika kwa mapungufu hayo ya kiufundi na usalama wa meli
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara amewasimamisha kazi na kuagizwa wapangiwe majukumu mengine vigogo wawili wa Mamlaka ya Bandari (TPA) makao makuu na Bandari ya Kiwira Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya

Source : Global TV online
 
03 June 2021
Kyela, Mbeya
Tanzania

Mengi yabainika MV Mbeya ilizinduliwa kabla ya kukamilika


Naibu waziri Mwita Waitara awa mbogo baada ya kugundua mapungufu mengi yalikuwapo ila wanasiasa waliingilia mchakato wa kiufundi na usalama wa chombo haujamalizwa.

Kufuatia kubainika kwa mapungufu hayo ya kiufundi na usalama wa meli
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara amewasimamisha kazi na kuagizwa wapangiwe majukumu mengine vigogo wawili wa Mamlaka ya Bandari (TPA) makao makuu na Bandari ya Kiwira Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya

Source : Global TV online


Huyu Mlevi asiyejua jina la RAIS bado yuko kazini?
 
Nimejiuliza sana yaani meli moja abiria 87 mabaharia 25? Mbona idadi ya mabaharia na abiria inakaribiana?
Hivi hata wanamaji wa ziwani ni mabaharia? Ni nilidhani mabaharia ni wanamaji wa baharini tu!
 
Back
Top Bottom