Meneja wa TANROADS nchini asema daraja la Kiyegeya limekatika kwa uchakavu. Je, Waziri Mkuu kumuondoa Meneja TANROADS-Morogoro alimuonea?

Meneja wa TANROADS nchini asema daraja la Kiyegeya limekatika kwa uchakavu. Je, Waziri Mkuu kumuondoa Meneja TANROADS-Morogoro alimuonea?

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Wakati meneja wa Tanroads mkoani Morogoro, Godfrey Andalwisye akiondolewa kwa madai ya kutokagua miundombinu, mtendaji mkuu wa taasisi hiyo, Patrick Mfugale amesema barabara ya Morogoro-Dodoma ni chakavu kwa kuwa imejengwa muda mrefu.

Kauli hiyo ya Mfugale imekuja siku moja baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuagiza Andalwisye arudishwe makao makuu kutokana na kutokagua barabara hiyo ambayo daraja lake la Kiyegeya lililoko wilayani Kilosa lilisombwa na maji.

Waziri Mkuu, ambaye juzi alikuwa ameenda eneo hilo kushuhudia ujenzi wa daraja hilo, alishangaa kuona mkoa wenye wahandisi 12, kushindwa kufanya ukaguzi wa barabara na madaraja.

Lakini jana, Mfugale alisema barabara hiyo ilijengwa miaka 40 iliyopita na hivyo imeshatumika muda mrefu ndio maana kila mara wamekuwa wakiifanyia ukarabati.

Alisema kukatika kwa daraja hilo ni jambo la kawaida kiutaalamu kwa kuwa uhai wa makalavati yanayowekwa si zaidi ya miaka 25.

Alisema tayari Serikali iko katika mchakato wa kuijenga upya barabara hiyo na madaraja yake.
 
Ndio,hakuwa serious na kazi zake yeye anawajibu wakukagua matatzo yote yanayojitokeza-Waziri yupo sawa

“Wakati meneja wa Tanroads mkoani Morogoro, Godfrey Andalwisye akiondolewa kwa madai ya kutokagua miundombinu,”

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnamtumbua manager wa TANROAD mkoa alafu Wizara zingine na watendaji wakuu wa taasisi zingine wanapeta. Tatizo serikali na wananchi wengi wanataka kutuaminisha kwamba mvua hizi ni kubwa kwa kuangalia mafuliko na maji yanayopita kwa kasi kwenye mito.

Madaraja yetu yatapona sio kwa TANROAD kukagua tu bali na watu wanaohusika na mazingira nao kukagua kingo za mito sambamba na wataalamu wa kilimo na kuchukua hatua kwa kuondoa shughuli za kibinadamu lakini pia hata watu wa maliasili pia kuhakikisha maeneo ya hifadhi na misitu ya asili haikatwi lakini pia sehemu za miinuko kufanyiwa kampeni ili ziendelee kuwa za kijani ili kupunguza maji kupotea kwa kukimbilia mtoni badala ya kufyonzwa ardhini.
 
Wakati meneja wa Tanroads mkoani Morogoro, Godfrey Andalwisye akiondolewa kwa madai ya kutokagua miundombinu, mtendaji mkuu wa taasisi hiyo, Patrick Mfugale amesema barabara ya Morogoro-Dodoma ni chakavu kwa kuwa imejengwa muda mrefu.

Kauli hiyo ya Mfugale imekuja siku moja baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuagiza Andalwisye arudishwe makao makuu kutokana na kutokagua barabara hiyo ambayo daraja lake la Kiyegeya lililoko wilayani Kilosa lilisombwa na maji.

Waziri Mkuu, ambaye juzi alikuwa ameenda eneo hilo kushuhudia ujenzi wa daraja hilo, alishangaa kuona mkoa wenye wahandisi 12, kushindwa kufanya ukaguzi wa barabara na madaraja.

Lakini jana, Mfugale alisema barabara hiyo ilijengwa miaka 40 iliyopita na hivyo imeshatumika muda mrefu ndio maana kila mara wamekuwa wakiifanyia ukarabati.

Alisema kukatika kwa daraja hilo ni jambo la kawaida kiutaalamu kwa kuwa uhai wa makalavati yanayowekwa si zaidi ya miaka 25.

Alisema tayari Serikali iko katika mchakato wa kuijenga upya barabara hiyo na madaraja yake.
Tatizo la Waziri Mkuu ni kutaka aonekane amembebesha mtu msalaba kisiasa.
Yeye angembebesha waziri mwenziwe Kawelwe ndo tungeelewa, lakini kumuondoa meneja wa mkoa, unyasi ni kumuonea tu.
Tunajua fika kuwa hela ya matengenezo mazito ya madaraja yote nchini serikali haina fedha hiyo.
Sasa leo Waziri Mkuu anajua kwa mfano daraja la Wami linaua kila siku, pale Dumila haipiti mika miwili daraja maji yanapita juu.
Waziri kuu upo tu.
Acheni usanii baba!!
 
PM yuko sawa licha ya kua limesombwa kwa uchakavu lakin Muhandisi usikanalitakiwa kutoa taarifa kama lilikua kwenye hatari libadilishwe.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Wizara inafahamu kuwa barabara imechakaa na pia inafahamu expire date ya makalvati imeshapita, sasa taarifa gani ulitaka meneja atoe? Ukweli ni kuwa maji yamezidi unga, serikali haina fedha kukabiliana na mafuriko nchi nzima inabidi iombe msaada.
 
Wizara inafahamu kuwa barabara imechakaa na pia inafahamu expire date ya makalvati imeshapita, sasa taarifa gani ulitaka meneja atoe? Ukweli ni kuwa maji yamezidi unga, serikali haina fedha kukabiliana na mafuriko nchi nzima inabidi iombe msaada.
Yeye kazi yake ni nini? Angekuwa amelikagua na kutoa taarifa kwanini hakujitetea pale alipoulizwa? Ningeona kweli ana haki kama angesema ''mheshimiwa waziri, hili daraja nilishalikagua na kutoa taarifa ngazi za juu lakini hakuna hatua iliyochukuliwa.''
 
Yeye kazi yake ni nini? Angekuwa amelikagua na kutoa taarifa kwanini hakujitetea pale alipoulizwa? Ningeona kweli ana haki kama angesema ''mheshimiwa waziri, hili daraja nilishalikagua na kutoa taarifa ngazi za juu lakini hakuna hatua iliyochukuliwa.''
Ndiyo sababu Mfugale amemjibu Waziri Mkuu kiana na kumuonyesha kuwa hajitambui na wala hajui status ya serikali yake!
 
Wizara inafahamu kuwa barabara imechakaa na pia inafahamu expire date ya makalvati imeshapita, sasa taarifa gani ulitaka meneja atoe? Ukweli ni kuwa maji yamezidi unga, serikali haina fedha kukabiliana na mafuriko nchi nzima inabidi iombe msaada.
Serikali yetu ni tajiri na hivi karibuni tutakuwa dona kantre.

Sasa hivi tumejikita kununua wanasiasa, barabara na madaraja tumesitisha kwa muda..

Ahsanteni kwa kunisikiriza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri Mkuu alikuwa sahihi,kwanini Mkuu wa Tanroad abaini uchakavu wa daraja ili hali mwakilishi wake hakujua uchavu huo.?
Somo: Mameneja wa Tanroad fanyeni auditing ya miundombinu yenu na muishauri serikali mapema.
 
PM yuko sawa licha ya kua limesombwa kwa uchakavu lakin Muhandisi usikanalitakiwa kutoa taarifa kama lilikua kwenye hatari libadilishwe.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Life Span ni 100 yrs lakini kuna kama miaka ,40 toka lijengwe je hapo unamlaumu vipi mtaalam? Suala la kukagua hata kama lipo je anavifaa vya kuonesha ubovu wa daraja au ndo anakagua kwa kuchungulia kwa macho kama polisi wa usalama barabarani wanavyokagua magari?
 
Mkuu Akishauri Ni Amri Bwana Mwenyekiti Huelewi!!!😀😁😂😄😅
 
PM yuko sawa licha ya kua limesombwa kwa uchakavu lakin Muhandisi usikanalitakiwa kutoa taarifa kama lilikua kwenye hatari libadilishwe.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Madaraja yote njia hiyo ni chakavu
.hujaelewa nn? Serikali hii haina fedha tu.kwani nchi nzima unajua machakavu yanapungua 100?
 
Waziri Mkuu hakumuonea, kama meneja ni lazima akaguwe madaraja na barabara anazozi "manage" na yakarabatiwe kabla hayajaleta athari.

Sasa siku zote alijuwa ana "manage" nini mpaka daraja kubwa linaleta athari kubwa? Huyo alijuwa ana"manage" nini zaidi ya Ku"manage" tumbo lake tu?
 
Kumbe mfugale anajua yalishachoka! Kama unajua hilo maana yke uangalizi unatakiwa kuwa karibu sana.
Mi naona mfugare nibola asingeongea hilo. Hii nikutaka kutuaminisha kuwa ipo cku watu watakufa kwatatizo wanalolijua wataaram wetu!
Ndo maana kule mwanza magu daraja la mto simiyu limeanza kufanyiwa ukarabati kila siku usiku.
Ndo inavyotakiwa siyo baada ya tatizo unasema wanajua.
 
Back
Top Bottom