zubedayo_mchuzi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2011
- 4,873
- 1,217
Habari zenu.
Nachukua fursa hii kuwaomba hawa matajiri wawili Tanzania na wengine,wawekeze kwenye elimu hasa kuwakopesha wanafunzi wasiojiweza ili nao waweze kusoma,Ni matumaini yangu wanaweza.
unajua maana ya kuwekeza mpaka useme awekeze kwenye elimu?, tutajie kwanza kuna kodi yoyote unamlipa mengi au bakhressa? Kama unataka mkopo kweli nenda benk, kwa bakhressa inapatikana lambalamba kwa mengi habari sio mikopo
Serikali ambayo inakusanya kodi kwa mengi na bakhresa si iwakopeshe hiyo kodi hao wanafunzi? Yaani mwenye nyumba adai uwakopeshe wanawe ada na yeye anakuna kitambi pembeni! Maajabu ya guiness haya sasa
Umetumia mbinu kali sana kuitukana Serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.
una nichonganisha na WAZEE wa kutoa kucha....nimewaomba wao wawakopeshe wanafunzi hata kwa kuangalia huitaji wataalamu katika sekta zao then wakimaliza wanarudi kufanya kazi katika viwanda vyao
Je wanafunzi wapo tayari kulipa kwa liba?mfano ukipewa mil 2 unaludisha mil 8 baada ya kumaliza chuo tu kama mpo tayari benk ziingie mkataba na na wanafunzi atakae shindwa kulipa atachukuliwa cheti kwa mujibu wa sheria itakayo tungwa
mkuu umeenda mbali sana,kwani hawa jamaa hela ambazo huwa wanachangishwa kama kuna ujio wa viongozi wakubwa huwa wanarudishiwa??????Ni wazo zuri nakuunga mkono...
Mzee Mengi na Bakhresa wawakopeshe wanafunzi wa elimu ya juu!
Wasiishie hapo waikopeshe na wizara ya elimu ili iweze kuwalipa walimu stahili zao!
Waikopeshe wizara ya afya ili mgomo wa madaktari usiwepo tena na waende mbali zaidi kuikopesha serikkali ili iendeshe shughuli zake za kila siku!
Unachoomba ni kwamba zaidi ya kodi wanazotozwa, matajiri hao waisaidie zaidi serikali!