Mengi,Bakheresa Kopesheni Wanafunzi wa Elimu ya juu....

Umeshajiuliza jinsi ya kuwabana hao watakao pewa mikopo ili wasikimbie kuacha kulipa deni pindi wakimaliza?

Kwa mfanyabishara hii biashara ni risky sana sana naamini hawawezi fanya hivyo otherwise wawasaidie wanafunzi kiroho safi ila sio mkopo
 
mkuu umeenda mbali sana,kwani hawa jamaa hela ambazo huwa wanachangishwa kama kuna ujio wa viongozi wakubwa huwa wanarudishiwa??????

Kuna wakati nafikiri kwamba tuliharakisha sana kuwafukuza wakoloni weupe kwa kuwa hatukuwa tumetengeneza mfumo thabiti wa kujitawala wenyewe na wakati mwingine nafikiria waasisi walikuwa sahihi kuchukua hatua ile kwa wakati ule ila waliopokea kijiti ndiyo wakavurunda.

Tumefikia mahala mwananchi anaona serikali haina msaadaa kwake na badala yake mwananchi mwenzake ndiye mwenye jukumu la kubeba mzigo uliostahili kubebwa na serikali? Kuna tofauti gani basi na mwenye dhana ya kuinuka kumvamia mwenye nacho kwa kuwa tu yeye hana?

Mengi/Bakhresa na wengine wa aina hiyo wameplay role kubwa sana kwa Watanzania wa kada mbali mbali,kuna maelfu ya watu walioajiriwa kwenye taasisi za hawa mabwana na kupitia ajira zao wameweza kuendesha familia zao kwa maana ya kuwa na makazi,kusomesha na mahitaji ya kila siku,bado hamuoni msaada wao kwa serikali? Mnataka wabebe tena majukumu ya hazina,wizara ya elimu na bodi ya mikopo? Kwanini serikali isikiri kushindwa kwanza ndipo wawaombe hawa wazee msaada?
 
Tukae tukajua elimu tunayotafuta ni kwa faida yetu,kukosa mkopo isiwe sababu ya kusahau wajibu wetu,nchi yetu inatutegemea,kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu,na ikumbukwe nchi yetu ni maskini,tushukuru kuwa baadhi yetu wamepata mkopo,waliokosa watafute njia nyingine kwa maana elimu yako inakunufaisha wewe na familia yako,so fight for it na si kuishutumu serikali,hata nchi zilizoendelea c wote wananufaika,badala ya kukaa kuongea vitu visivyowezekana ni bora kukaa na kuangalia alternatives zitakazowezesha kuyafikia malengo yetu,si CHADEMA wala CUF itakayoweza kuwaridhisha kila mmoja wetu,leo hii serikali ya marekani imewakosesha watu zaidi ya laki 8 ajira walizokuwa nazo,kwahyo ifike wakati tujifunze kujitegemea kwa kila kitu,
 
Kijana rudi upenuni mwa jamvi ubishe hodi kwanza!
 

nani kasema nchi hii ni maskini????
 

mawazo mazuri lakini swali ni HOW??
 
baba yako mzaza ameshindwa kukulea unaomba kulelewawna baba wa kambo? mwambie kikwete akukopeshe na mwaneridhiwani.
 

wewe ni msemaji wa BAKHRESA AU MENGI
 
Kama hukutaka watu watoe mawazo yao ungewaandikia barua kina Mengi ama ungeweka angalizo kwa watu wenye mawazo tofauti na yako wasichangie!
hujatoa mawazo yako ila umesimama badala yao.......unge sema mapema kuwa una manufaa na hawa watu,wanafunzi wanashida,swala la bakheresa na Mengi linawezekana kabisa kwani wao wanaweza kuangalia uhitaji wa wataalamu katika viwanda vyao na kuamua kuchukua wanafunzi na kuwasomesha alafu na kurudi tena kufanya kazi katika makampuni yao,hata wanapokuwa likizo wanaweza kurudi na kufanya hizo shughuli katika viwanda vyao,si lazima kama uwazavyo wewe au niwazavyo mimi,ila hakuna linalo shindikana........
 

Unanikumbusha kisa kimoja cha blackmailer kumteka mtoto wa mwenye nazo kisha kupiga simu kwa baba akibargain apewe kiasi fulani cha hela ndipo amwachie mtoto...Mwenye mtoto ikabidi ahoji kama watekaji wanampatia mateka chakula,maji na mahala bora pa kulala,walipomjibu ndiyo akawaambia basi warudi kuchukua na ndugu wengine wa mateka yule!

Moral ya story yangu si kuchekesha,na nidhanivyo huenda umenununa kwa kudhani nipinga proposal yako,hasha mkuu...wakiisha kukubali kubeba jukumu hilo basi ujue serikali(ambaye ni kama baba) atamwambia bwana Mengi/Bakharesa wawachukue na ndugu wengine wa mateka kwa maana wenye mahitaji ni zaidi ya wanafunzi...kwani unadhani serikali imeshindwa ama ni utaratibu/usimamizi mbovu wa zoezi zima! Bodi ya mikopo ilipanga zaidi ya miaka sijui mingapi Tirdo msasani wameshindwa kujenga walau pango lao leo wamekuja kurent jengo kubwa zaidi Mwenge,ni akili au matope!

Tuambiwe kabisa ni biashara gani wanafanya kupata kodi ya pango na marejesho yake yakoje,utitiri wa walioajiriwa bodi na baada ya muda wanaenda kusomeshwa zaidi ilihali wadogo zao wakihitaji walao kupata shahada ya kwanza! Kwanini usitengenezwe utaratibu wa hawa wakurugenzi kuomba kazi kwa kuandaa somesort of plan ya kuonesha ni namna gani ataweza kutatua tatizo la kila mara la wanafunzi kukosa mikopo?Kwanini wasianzishe vitega uchumi badala ya kupulizwa tu na viyoyozi ofisini wakisubiri hazina iwakumbuke?
 
Kila kitu kinawezekan c kukopesh 2 hata kwa kusaidia kiasi fulani wanaweza na mambo yakaendelea
 

Sasa basi muwape na uraisi kama kila sekta wawakopeshe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…