Mercedes Benz E190

Inakula mafuta vizuri sana hasa ukiipata ya dizeli. Vipuli ni vingi ila bei imechangamka
Mkuu kama model namba ni 190E atapaje ya diesel ? Hizo herufi baada ya namba za merc zina maana yake,ya diesel namba ingefuatiwa na herufi D,kwa mfano 190D. Kwa hiyo namba ikifuatiwa na herufi E haiwezi kuwa ya diesel sasa atapaje diesel ? Siku hizi mfumo wa utambuzi wa hizo namba umebadilika kidogo lakini diesel bado ina identification tofauti kama DGI au BlueTech lakini kama unafahamu magari zile herufi na namba zinatosha kukupatia information nyingi sana za gari.
 
Mkuu ni kweli kuipata 190E ya Diesel ni ngumu ila anaweza kubadiri engine na kuweka ya Diesel akihitaji nasemea hili kwa vile Nina uzoefu na gari hii baada ya kubadiri engine ya petrol na kuweka ya Diesel na gear box kutoa auto na kuweka manual gari inanguvu spare zipo fedha yake tu kipindi cha nyuma magari mengi aina hii yalikatwa kutokana na wimbi la R/License spare zipo nyingi gari imara sana naitumia bila tatizo uoga wa TZ tu na kutishana kwingi mkuu
 
Kiongozi kama umesoma vizuri nilichoandika,190E haiwezi kuwa ya diesel,sasa kamaukufanya modification kama uliofanya basi ile namba 190E inakuwa haina maana tena. Pili Unapofanya modification kama uliyofanya kuna gharama iliyotumika,na mara nyingi lengo huwa ni kupunguza gharama za mafuta,swali hapo ni kwamba kwa mfano ulitumia million mbili,je inakuchua miaka mingapi kurejesha hizo hela kwa unafuu wa mafuta?Unaposema ina nguvu,unaweza kuweka namba ya hizo nguvu ?HP na Torque ?
 

Mkuu yote tunajaribu kumsaidia ndugu huyu kusudio lake ila ni chaguo lake kununua au kuacha. Mimi nilikuwa nalo tayali likaanza kusumbua engine ya petrol na g/box auto. Je Mkuu gari ningeiuza ikiwa mbovu nani angenunua, gharama iliyotumika ni ya kawaida Tsh 1.3m na gari ni imara na ya heshima siwezi kulinganishwa na vigari vya mjapani V baby W. Kama nilivyo sema wa Tz tunatishana sana kuhusu ununuzi wa magari ukilipenda nunua wasi wasi wa baadae kuuza au kutouza ni jambo jingine hasa ukiwa siyo mfanya biashara ya magari kununua na kuuza
 

Ile gari uliyodhani ni kama natania ni hii hapa inaendelea na matengenezo nitakurudia ikiwa tayari pia chief,shukrani kwa mawazo barikiwa sana mkuu[emoji41][emoji41][emoji41][emoji41]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…