Mess vs Maradona nani bora kwa muda wote.?

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,284
Reaction score
38,364
Huu mjadala imetawala kwa sasa duniani kote nani zaidi kati ya Mess na Maradona..

Binafsi Mess ni bora zaidi ya Maradona, licha ya kwamba Maradona sijamwangalia wakati wake zaidi ya kwenye Mikanda na clip fupi fupi kwenye mitandao.

Wakongwe wanasema Maradona alikuwa mkali, lakini kwa muda mfupi..lakini huyu kiumbe Mess hajawahi kushuka toka dunia imtambue.
 
Messi ni mkali wa Barca, hasa katika historia ya Barca. Maradona ni mkali wa Argentina pia Napoli. Messi ana hadhi kubwa Barca ila hana hadhi kama iyo Argentina. Maradona ana hadhi kubwa Napoli na Nyumbani kwao Argentina.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maradona alikuwa bora kwa wakati wake ila Messi ndio bora wakati wote.
 

Maradona alikuwa bora kwa wakati wake ila Messi ndio bora wakati wote.

King Messi ni balaa

Muliwahi muona Maradonna ?
 
Sana tu tena. Na bado
naendelea kusubiri goli lake la kwanza ndani ya World cup knockout stage. Tunasubiri world cup yake ya 5.
2014 alifunga goal 4,timu ikafunga 7 . I mean wenzie 3.



Messi mfungaji Bora wa muda wote Argentina,63 au 65 goals.


Maradona 34 goals na kashastaafu
 
Takwimu ndo kila kitu kwenye mijadala ya aina hii otherwise ni kupoteza muda tu.Vikombe,Magoli,Tuzo etc
 
2014 alifunga goal 4,timu ikafunga 7 . I mean wenzie 3.



Messi mfungaji Bora wa muda wote Argentina,63 au 65 goals.


Maradona 34 goals na kashastaafu
Magoli 65 yameweza kuipa nini argentina upande wa vikombe? Ukiachana na olimpiki 2008.
 
Magoli 65 yameweza
kuipa nini argentina upande wa vikombe? Ukiachana na olimpiki 2008.
Argentina ni Finalist world cup2014,Na mataifa ya amerika kusini 2015 na mataifa yote America 2016

Hiyo sio riadha,ni watu kushirikiana. Huko Barcelona anashirikiana na wenzie wanashinda vikombe. Hakuna katika dunia hii mtu awe vizuri mwenyewe halafu washinde ubingwa wa soccer labda bahati. Usajili was mchezaji huangalia mtu anavyocheza sio idadi ya makombe.

Huyo Maradona Club level kachukua ubingwa gani kumzidi Messi. Utakata awezajitetea kuwa alikuwa na average players,beki uchochoro unafunga 2 mnapigwa tatu. Watu wanataka National team result ndio ziwe kipimo ,wale ambao heroes wao wamefanikiwa huko zaidi. Mimi sijawahi kuona Full match za Maradona,Kama hivi tunavyoona Barca wanapigwa 3-0 kwa Roma,Messi ndani. Tunaoneshwa vipande vitamu tu vya Maradona.

CR7 ,Messi Wapo kwenye teams ambazo wenzao Ni average. George Weah kapewa uchezaji Bora wa dunia '95 wakati Liberia haijawahifuzu World Cup.
 
Naona swali langu halijajibiwa.

Niuulize swali lingine kati ya argentina ua 86 na argentina kuanzia 1998 - 2018 ipi ilikuwa na avarage players?

Ukilinganisha napoli ambayo maradona alikuwa anahamia na barcelona ya mwaka 2008-2012, nani alikuwa anazungukwa na avarage players kati ya messi na maradona?
 
2014 alifunga goal 4,timu ikafunga 7 . I mean wenzie 3.



Messi mfungaji Bora wa muda wote Argentina,63 au 65 goals.


Maradona 34 goals na kashastaafu

hayo manne yote yalikua makundi na vibonde akina Iran na Nigeria. Kuanzia knockout round hajawahi funga goli. Na ameshacheza world cup 4. Huyo ndie munaemwita greatest player ever !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hayo manne yote yalikua makundi na vibonde akina Iran na Nigeria. Kuanzia knockout round hajawahi funga goli. Na ameshacheza world cup 4. Huyo ndie munaemwita greatest player ever !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mi nadhani labda watufafanulie maana ya mchezaji bora wa muda wote wao huwa wanamaanisha nn.
 
Wanaojuwa mpira washasema Messi ni bora kuliko all players in the world, mimi wa tandale ninaeenda kuangalizia vibanda umiza kama nani nibishe! Si nitakuwa mwendawazimu jamani!! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Binafsi najisikia mwenye bahati sana kuishi na kupata bahati ya Kumuona Lionel Messi wiki baada ya wiki akipangua defenders kwa vyenga vya uhakika,akifunga magoli lukuki kwa muda wa muongo mzima katika kiwango cha juu muda wote. Takwimu ni chakula cha akili,kama takwimu zitawabeba wengine juu ya Lionel Messi hiyo itabaki ktk akili tu lakini ndani kabisa ya Moyo Wangu unaamini...Lionel Messi ni Mchezaji Bora Zaidi kuwahi kutokea Duniani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…