Messi avunja rekodi ya Pele iliyodumu kwa miaka 50

poposindege

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
453
Reaction score
175
[h=2]Hat-rick ya Messi dhidi ya Rayo Vallecano ilivunja rekodi ya mmoja wa wanasoka bora duniani, Pele iliyokaa kwa zaidi ya miaka 50.[/h]Mabao hayo yamemfanya Messi kuipita rekodi ya ufungaji mabao ya Pele katika misimu yake sita ya mwanzo katika soka. Kuanzia msimu wa 2009/10, Messi ametimiza mabao 315 kutokana na Hat Trick yake ya wikiendi iliyopita.
Kwa upande wa Pele, rekodi hii aliishikilia kwa zaidi ya miaka 50 baada ya kufunga mabao 313 kuanzia mwaka 1958 mpaka 1963 na tangu hapo hakuna mwanasoka ambaye aliwahi kufunga mabao mengi katika kipindi kifupi.
Hata hivyo nyota huyo wa Barcelona anatarajiwa kufanya maajabu zaidi msimu huu kwani amebakiwa na mechi 19 mpaka msimu uishe hivyo kuwa na fursa ya kufunga magoli mengi zaidi.
Hii ni rekodi nyingine ya Pele ambayo Messi anaivun ja baada ya kuvunja ile ya kuwa na magoli mengi ndani ya mwaka mmoja iliyowekwa na Pele mwaka 1958 na kuvunjwa na Messi mwaka 2012.
Aidha mwaka huohuo 2012, Messi alivunja rekodi ya Mjerumani Gerd Muller ya kufunga mabao zaidi ya 85 ndani ya mwaka mmoja.
 
huyu jamaa ni hatari leo katupia mbili la liga
 
Ray Hudson (Commentator) - “They tell me that all men
are equal in God’s eyes, this player (Messi) makes you
seriously think about those words. ”
 
Mario Balotelli (Manchester City) - “There’s only one that
is a little stronger than me: Messi. All the othersare
behind me.”
 
Wakuu, mimi sina neno la kusema juu ya Messi.
 
World cup eludes Messi. Will his name stand out without winning a world cup medal. Clearly and categorical no!
 
Huyu mt ni ktk miuujiza iliyopo duniani kwa sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…