Spitzkoppe
JF-Expert Member
- Feb 27, 2014
- 246
- 449
Kombe La Dunia Lipo Kabla Ya Messi na Ronaldo...
ARGENTINA isipofuzu Hii Dunia itatingishika na kutakua hakuna haja ya Kombe la Dunia
KabisaWorld cup bila ARGENTINA na bila King MESSI haitanoga.
Wanaomchukia wamchukie tu. King atabakia kuwa the king Na ndoo inawahusu urussi. Kama kawaida mzee wa hatrick *****,,,c mchezo
Hatarii.......World Cup bila Argentina/King Messi isingenoga__ni sawa sawa na Ndondo Cup.
View attachment 607040
Ndugu wapenzi Argentina National Teams Fans and others. Tunashukuru Mungu kuishuhudia timu yetu pendwa yenye mashabiki wengi mnoo duniani mmoja wao ni mimi BlackP__ am very happy kuona majembe yakiongozwa na Mfalme wa soka kuwahi kutokea katika ulimwengu huu wa soka THE LION MESSI/SIMBA ML10 akiibeba timu yake kwenda Russia___Argentina imeizamisha ecuador goli 3 kwa 1 hapo jana usiku. Tukumbushane kidogo hapo awali timu yetu pendwa ilikuwa inashikilia nafasi ya 6 na sasa ipo nafasi ya 3.kwa maana hiyo imeshafuzu kuelekea moja kwa moja nchini Russia kwa Super power Mr Puttin.
1-Brazil
2-Uruguay
3-ARGENTINA
4-Colombia
5-Peru___play off
Timu 4 zimeshafuzu moja kwa moja___namba 5 itacheza play off
Na mimi pia nimefurahi Argentina kufuzu kushiriki kombe la dunia
Nahodha Lionel Messi ana kazi ngumu kuivusha Argentina katika fainali hizo katika mchezo wa mwisho dhidi ya Ecuador itakapokuwa ugenini mjini Quito.
Endapo Argentina itashindwa kukata tiketi, itakuwa ya kwanza kutokushiriki fainali hizo tangu mwaka 1970.
Brazil tayari imekata tiketi na katika kundi lake inafuatiwa na Uruguay (pointi 28), Chile (26), Colombia (26), Peru (25), Argentina (25) na Paraguay (24).
Argentina wanashikilia nafasi ya sita katika msimamo wa kufuzu kwa Kombe la Dunia katika Amerika Kusini kukiwa na mechi moja ambayo imesalia kuchezwa.
Nchi zinazomaliza nne za kwanza ndizo hufuzu moja kwa moja
Atakayemaliza wa tano atacheza dhidi ya New Zealand na mshindi afuzu.
Wakati huo huo
Mabingwa wa Ulaya, Ureno wanatakiwa kushinda katika mchezo wao na Uswisi na jukumu kubwa lipo kwa nahodha Cristiano Ronaldo.
Ureno inahaha kukata tiketi kucheza fainali hizo ikiwa nafasi ya pili kwa pointi 24 nyuma ya Uswisi yenye pointi 27.
Endepa Ureno itashindwa kushinda mechi hiyo na kumaliza nafasi ya pili itasubiri kuchagulia katika timu nane bora zilizomaliza nafasi ya pili kwenye makundi na kucheza mechi mbili (play-off) za nyumbani na ugenini na mshindi kufuzu kucheza michuano hiyo ya kombe la dunia