Messi vs Ronaldo: Nani zaidi?

~ Ronaldo ni mfungaji bora sana sana saaaaaana wa wakati huu.
~ Messi ni mchezaji bora wa wakati wote, genius kutoka sayari nyingine.
kuwachanganya watu hao ni udhaifu tu wa kibinadamu.
 
Messi kipaji,Ronaldo nguvu nyingi.Pia siku hizi Messi kawa kama Zidane kazi yake kugawa mipira ya ufungaji magoli.Bila Messi hakuna Neymar wala Suarez
 
Messi anacheza soft ball!CR7 nguvu nyingi Kama mbeba vyuma'CR kitu amemzidi messi ni umri tu!lakin vingine vyoote mess anaongoza!UEFA ndio anaongoza kwa sasa dhidi ya CR'na CR kesha tolewa!la liga vita bado'TUZO ya dunia mess anaongoza!mfungaji wa la liga wa muda wote mtoto anaongoza
 
Mkuu kupingana na ukweli kuwa messi ni zaidi ya ronaldo ni sawa na kupinga kuwa Tundu lisu ni zaidi ya lusinde, ki uelewa!!!
 
Daaah Hawa watu wanaoamkia kuangalia matokeo kwenye magazeti utawajua tu .. Kama mnapenda soka jaribu hata kuchek mechi basi mambo mengine tunapoteezeana mda !
 
Titizo kubwa la CR7 ni kupambana na Messi wakati huo Messi hapambani na CR7. Ni vigumu sana kushindana na mtu ambaye yeye hana mpango. Ninacho amini CR7 atawahi kuchoka/kustaafu kuliko Messi kwa kuwa CR7 ni mkubwa kiumri. Pia CR7 akianza kuchoka Madrid watamtema faster kwakua wale ni wafanya biashara wakubwa na wanaanza kutafuta mchezaji ambae yupo hot kwenye possition ya CR7 pia Messi pale Barca naamini ndio mpira wake utaishia pale kama Puyol na Xavi ilivyo kitu ambacho kitasababisha Messi amalize record zote pale.
 
Daaah Hawa watu wanaoamkia kuangalia matokeo kwenye magazeti utawajua tu .. Kama mnapenda soka jaribu hata kuchek mechi basi mambo mengine tunapoteezeana mda !

kwa taarifa yako ninamiliki king'amuzi cha dstv na mechi zote natazama sebuleni kwangu! Naangalia mechi live, kisha naangalia replay kwa zaidi ya mara mbili. Muda mfupi uliopita nimemshuhudia Ronaldo akifunga hat trick ya saba msimu huu! Ana magoli 45! Messi nimemtazama akiambulia goli moja! Messi ajiandae kumshangilia CR7 akibeba kiatu cha dhahabu!
 

Kwa maandishi haya, nalazimika kuhoji juu ya uzima wa akili yako!

Certified insane! Lol!

Acha ushabiki mkubwa toka kwenye ako kajela upate uhuru wa kufurahia soka..inachukua miaka mingi sana Dunia kupata watu wa kariba ya messi, umepata nafasi usijinyongee..wewe furahia rhythim ya soka ya Messiah wa soka..Messi!

CR7 nampa pongezi inataka ujasiri mkubwa kujaribu kupambana na Messi..
 

Goli la messi leo ni tamu kuliko magoli 3 ya cr7, linawanyanyua wapenzi wote wa Baca dunia nzima kuupokea UBINGWA, angekuwa anajua huyo cr7wenu angejua kufunga magoli yenye kubadili matokeo, sasa yeye amefunga magoli mengi halafu timu aliyoifungia hayo magoli mengi siyo bingwa.

Inaonyesha cr7 ni mbinafsi kupindukia, hawezi kuwachezesha wenzake ili ushindi wa jumla upatikane.

Cr7 Atachungulia sana kwenye tv wakati wenzie wanajitwika ndoo msimu huu.
 

Kwa Ushauri nenda kamuone Doctor wa akili
 

Kuna watu wana akili kama za kuku, yaani Messi amshangilie Ronaldo wakati Messi yeye tayari kabeba La Liga, anacheza final ya Kombe la Copa del Ray pale Camp Nou kitu ambacho kinampa advantage ya kulibeba na bado anacheza final ya UEFA, nani wa kumshangilia mwenzie hapo sasa.
 

hi comment in maana sana,bnfsi nilkuw simkubali messi,ila baada ya kuwafanya kitu mbaya man city ninamkubali sana,he comes from another planet, MESSI NI BALAAA
 
kumbe hii thread bado ipo mimi nikajua mnauliza Messi na pele nan zaid kumbe mnaulizia kuhusu Messi na mwanariadha
 
Kwa Ushauri nenda kamuone Doctor wa akili

Umeishiwa hoja! Ronaldo na messi wote ni washambuliaji, jukumu lao la msingi ni kufunga magoli. Hivyo kigezo kizuri cha kuwalinganisha ni kwa Kiasi gani kila mmoja ametimiza jukumu hilo. Hivyo wingi wa magoli waliyofunga katika mazingira sawa ndio kigezo cha kisayansi cha kuwalinganisha! Mpaka sasa kwenye la liga Messi amecheza mechi 37 na amefunga magoli 41, na kasi yake ya kufunga magoli ni magoli 1.108 kwa mechi moja. Ronaldo amecheza mechi 34 na amefunga magoli 45, na kasi yake ya kufunga magoli ni magoli 1.324 kwa mechi moja. Hivyo ni dhahiri kabisa Ronaldo yuko JUU. Messi atasubiri sana!
 

Messi lazima mpira wake uishie barca maana aina yake ya uchezaji na aina ya watu wanaombeba wako hapo! Hawezi kutamba katika timu nyingine na katika ligi nyingine! Hana jinsi isipokuwa kuzeekea barca ili angalau alinde heshima yake! Anaogopa yasije yakamkuta yaliyomkuta Falcao!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…