Messi vs Ronaldo: Nani zaidi?


Nimekupa senks
 
Asee mchambuzi nakupa big up sana, hapa mtu mwenye kujua hao watu wawili (CR7 Na The Flea) hawezi bisha.

Ila kuna jamaa hapo anasema eti huwezi kuwalinganisha coz Messi yupo timu inayofanya vizuri na Ronaldo timu yake haifanyi fresh.... Sasa kazi ya mchezaji bora c ndo kufanya timu ifanye vizuri braza????

Na kama unatumia kigezo hicho kusema huwezi kulinganisha basi hata ma legends wa huko nyuma (Ronaldo the Phenomenon, Ronaldhino,Zidane,Figo etc) wacngelinganishwa kwasababu hata wao timu zao zilikuwa zinafanya vizuri mzee

Lazma ukubali kitu kimoja kipaji cha mchezaji kinaundwa na vitu vingi ,team work ikiwa ni moja wapo na uwezo wa kufit kwenye system ya timu na kuisaidia kushinda, so usiseme ivo bana, kubali yaishe Lionel Messi is from another Planet asee
 
Safi sana,
NAKUBALIANA NA WADAU WOTE WALIOCHAMBUA HAPO AWALI.
 
Nimewahi kuona upinzani katika mpira but huu wa messi na ronaldo ni kwisha kazi.Hawa jamaa ni kiboko mbaya yaani kila mmoja wao hatamani kuona anapitwa na mwenzake,na nina wasiwasi msimu huu hawa njemba wanaweza kufungana magoli.
 
wanamagoli 41 kila mmoja, so bonge battle mtu wangu.
 
nadhan itakuwa 40 kwa 39. . ila mess ana goli 63 hiv kwa mashndan yote. anataka kufikia rekodi ya mchezaj mmoja wa kijeruman aliyefunga goli 67 kwa msimu mmoja
 
wote wana magoli 41,kila mmoja ,baada ya jana mess kutupia magoli 2,ila mwisho wa cku messi atakuwa mshindi.ligi ya spain ina timu nyingi dhaifu ndio maana m2 ana uwezo wa kufunga hati trik 7,kwa msimu mmoja! Kwa epl,au bundesiliga inakuwa ngumu sana.
 
messi yuko vizuri mno japo ronaldo nae yuko vizuri bt nampa messi 60% ya kuwa mfungaji bora dhidi ya ronaldo kwa msimu huu
 
Naipenda sana Real Madrid, lakini kwa kiwango hakuna ubishi, Barca ijo juu sana na Messi ni kiboko, nitafurahi zaidi kama Ronaldo akimzidi Messi ingawa ni nahisi kama ni ngumu sana
 
nawatabiria Real kuwa mabingwa Europe na ligi ya spain kwa sababu ya Ronaldo........
 
messi yuko vizuri mno japo ronaldo nae yuko vizuri bt nampa messi 60% ya kuwa mfungaji bora dhidi ya ronaldo kwa msimu huu
msimu ulopita nani aliongoza ?
 
NANI ZAIDI?
Messi anakubalika kuwa na kipaji bora zaidi duniani kwa sasa, huku Ronaldo akikubalika kwa uchezaji maridadi zaidi
 
Kiongozi hii el clasiko tunaestream mtaa gani,ebu tupia link kwa hapa.
 
otea nani mkali zaidi wa mwenzake, mi naona Messi, Ronaldo miyeyusho, lakini nkicheki sana naona Ronaldo mkali, mbona najichanganya mara Messi mara Ronaldo.

Kati ya Messi na Ronaldo mkali nani? Mkali Messi

Kati ya Messi na Ronaldo mkali nani? Mkali Ronaldo

Mbona najichanganya mara Messi mara Ronaldo
 
Mkitaka kumpima messi na ronaldo embu ahame barcelona kama atabaki kama alivyo.Kwangu mi R9 ni mkare
 
Cristiano ni zaidi ya Messi. Siasa za FIFA na UEFA zinambeba sana Messi.

Cristiano ni mchezaji mkamilifu,anatumia miguu yote vizuri,anatumia kichwa,anafunga ndani ya 16,18 na nje hadi mita 35. Anaweza kuibeba timu yeye mwenyewe.

Messi ni mchezaji mzuri pia,ila hajakamilika. Zaidi ya mguu wake wa kushoto,hawezi kutumia mguu mwingine,kichwa utumia kwa nadra sana,na baya zaidi hawezi kucheza bila ya msaada wa Xavi na Iniesta.

Ila wote wakiwa kwenye timu zao za taifa wanakuwa kama sio wao. Ndiyo maana mimi kwa mtazamo wangu siwezi kuwaweka daraja moja na Zizou,Gaucho,El Phenomena,Pele na Maradona.

Lakini kwa kuwalinginisha,nikitumia kigezo cha ukamilifu wa kiuchezaji,Cristiano ni zaidi ya Messi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…