Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Taarifa iliyotolewa na Klabu hiyo imesema kuwa, uongozi umesikitishwa na kitendo kisichokuwa cha kiungwana alichokifanya Metacha hiyo anasimamishwa hadi hapo suala lake litakapofikishwa mbele ya kamati ya nidhamu ya klabu hiyo.
Pia, Uongozi umeomba radhi wanachama, wapenzi, mashabiki na wadau wa michezo kwa kitendo hicho alichokifanya Mnata
Jana usiku baada ya mchezo wa Yanga dhidi ya Ruvu Shooting kumalizika kipa huyo wa Wanajangwani, Metacha Mnata alionyesha ishara mbaya kwa kuwanyoshea vidole mashabiki waliokuwa wakimzomea.
Hiyo ni baada ya Metacha kuzozana na baadhi ya wachezaji wenzake na alipokuwa anaenda vyumbani ndio aliwaonyeshea ishara hiyo kwa mashabiki wa Yanga.
Mashabiki hao ambao hawakufurahishwa na kitendo hicho waliamua kulizunguka gari la timu yao wakimshinikiza kumtaka Metacha aliyetibua furaha yao ya kuifunga Ruvu Shooting
''Tunamsubili aje atuambie kwanini anatuonyeshea vidole kama tusipompata hapa tutamfata nyumbani kwake (akitaja anapoishi mchezaji huyo),” alisikika mmoja wa mshabiki hao.