Methali zetu tujikumbushe kidogo

radika

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2014
Posts
20,440
Reaction score
32,260
Mhindi aliambiwa amalizie methali za Kiswahili
1.Nyani haoni - valise miwani
2.Debe tupu - weka dengu
3.Maskini akipata - itaacha iba jumbani
4.Penye kuku wengi -Chinja bili au tatu
5.Asiyesikia la mkuu -Peleka yeye polisi
6.Penye wengi - iko kutano ya CHADEMA
7.Asiekubali kushindwa - hio itakua CCM
8.Bandu bandu - Baba yake Somji iko Bombay
9.Simba mwenda kimya - hiyo iko Jangwani bhanaa
naogopa Yanga tuu
10. Mstahamilivu- Maalim Seif miaka isirini nasinda
lakini hakui rais
 
Mkuu hapo kwenye "kutano ya CHADEMA" umeua na "hio itakuwa ccm" nusura univunje mbavu!
 
Mi nimeipenda hiyo hiyi ya kumi ya maalim seif
 
Poor thinking capacity mleta thread
 
Poor thinking capacity mleta thread



Hahahahaha sio muda wote unaandaa akili yako kukutana na vitu vigumuvigumu kuna muda akili na ubongo vinatakiwa kuwa free lilax man
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…