Mfahamu Dikteta Hastings Kamuzu Banda wa Malawi aliyepiga marufuku kuvaa suruali

Mfahamu Dikteta Hastings Kamuzu Banda wa Malawi aliyepiga marufuku kuvaa suruali

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
122,494
Reaction score
96,074
MFAHAMU DIKTETA WA MALAWI ALIYEPIGA MARUFUKU KUVAA SURUALI​

Baba wa Taifa la Malawi, Dikteta Hastings Kamuzu Banda aliingia Malawi mwaka 1958 akitokea Uingereza alikoenda kusoma tangu 1925, alianza harakati za kudai Uhuru mwaka 1957 na Malawi ikapata Uhuru 1961 yeye akawa Raisi na kutangaza kuwa Raisi wa Malawi kwa Maisha yote.

Alitangaza mambo mengi kuwa marufuku Malawi, kwa mfano wanawake kuvaa suruali, kuonyesha magoti , wanaume kuwa na nywele ndefu au suruali fupi. Makanisa yalipaswa kutafuta kibali cha serikali, Mashahidi wa Yehova walipigwa marufuku.

Mwaka 1983 aliwaua mawaziri watatu waliokuwa wanamwambia kuhusu mfumo wa vyama vingi, alipowaua akawaweka kwenye gari gari hilo likisukumwa kwenye korongo . Radio Malawi ikatangaza Mawaziri wanne wafariki kwa Ajali baada kutumbukia kwenye Korongo. Raisi Kamuzu akaamuru wazikwe siku hiyo hiyo miili yao isioneshwe kwa kuwa imeharibika.

Mwaka huo huo alitimua Wabunge wote wa Bunge la Malawi kwa amri yake wakawa sio Wabunge tena, Alitangaza kila Mwananchi hadi watoto wawe na kadi ya chama chake cha MCP asiyekuwa na Kadi hakuruhusiwa kupata huduma muhimu mfano Matibabu, Shule, nk.

Alipiga marufuku upinzani nchini humo akidai ata Mungu alikuwa hataki upinzani ndio maana alimfukuza Shetani.

Kamuzu alikuwa anatembea na Fimbo mbili moja yenye manyoya kwa ajili ya kufukuzia Nzi akidai UK hakuwahi kuona nzi. Kamuzu hakuwahi kuoa bali alikuwa anaingiza wanawake tofauti tofauti Ikulu.

Hadi Oktoba 1992 Banda alipaswa kukubali kura ya wananchi kuhusu swali la kukubali vyama vingi baada ya Maandamano nchi nzima wakiwemo Wanajeshi na Polisi

Kura hii ilileta asilimia 64 kwa ajili ya demokrasia ya vyama vingi . Mwaka huohuo halmashauri mpya ilitangaza
katiba mpya na kuondoa "urais wa maisha".

Katika uchaguzi wa mwaka
1994 Banda aligombea tena Urais lakini alishindwa na Bakili Muluzi . Chama kipya cha Muluzi kilipata wabunge wengi.

Banda aliendelea kuwaangalia Wamalawi kama "watoto wa siasa" akatabiri ya kwamba wanahitaji "mkono wa chuma".

Mwaka 1997 alingonjeka akapelekwa kwa matibabu Afrika Kusini alipofariki tarehe 25 Novemba 1997 akiwa na
umri wa miaka 99

Huyo ndiye Kamuzu Banda aliye jitangazia kuwa ni rais wa maisha wa Malawi kwa ulevi tu wa madaraka.

FB_IMG_1593113081416.jpeg
 
Ukiisoma hii habari inatoa muendelezo wa mind programming iliyoasisiwa na mabeberu kupitia BBC pamoja na vyombo washirika ili kurasimisha hoja ya ovu kuwa waafrika hawawezi kujitawala.

Kuna mengi yanafanyika behind the scene katika harakati za kuitengeneza akili ya muafrika kuamini kuwa chochote kizuri lazima kifanywe na mtu mweupe hivyo hata marking ya utawala bora na maendeleo inaandiliwa na kikundi hicho. Bahati mbaya sana wengi tupo kwenye umaskini hivyo ni ngumu sana kung'amua hila hizo.
 
Ukiisoma hii habari inatoa muendelezo wa mind programming iliyoasisiwa na mabeberu kupitia BBC pamoja na vyombo washirika ili kurasimisha hoja ya ovu kuwa waafrika hawawezi kujitawala. Kuna mengi yanafanyika behind the scene katika harakati za kuitengeneza akili ya muafrika kuamini kuwa chochote kizuri lazima kifanywe na mtu mweupe hivyo hata marking ya utawala bora na maendeleo inaandiliwa na kikundi hicho. Bahati mbaya sana wengi tupo kwenye umaskini hivyo ni ngumu sana kung'amua hila hizo.
Kwa uhuni huu unaoendelea, Afrika ni kweli hatuwezi kujitawala, katiba ipo ambayo ndio dira, mtu anaamua kuitupilia mbali na kuongoza nchi kwa matakwa yake?!!!

Kuna nini hapo? Leo hata stahiki za mfanyakazi ambazo zipo kisheria, nazo zitegemee huruma ya kiongozi?!!! Miafrika bwana tuna lanaaaa!!!
 
Sikujua kama Banda alikuwa dikteta
Siku moja alikuwa akipata barabarani na kushangiliwa na wananchi wake wakisema kuwa "Banda is the man we want, Banda is the man we want". Aliwakatiza na kuwasahihisha akisema "what is this nonsense I hear about Banda is the man that you want? Banda is not the man you want, Banda is the man you have got"
 
Dah watawala wa africa hatari.
Kinachonishangaza inakuwaje mihimili mingine inakuwa inashindwa kuchukua hatua wakati mmoja anapokuwa anaweka rehani usalama wa Taifa.
 
Inamaana miaka yote aliyokaa UK masomoni ndio alikua anasoma huu ujinga wa URAIS WA MAISHA?![emoji1][emoji1][emoji1]
 
Jamaa alizingua sana. Sisi ambao tuko mpakani tulikuwa na taarifa zake nyingi. Inasemekana hakuwa mmalawi bali alikuwa mghana. Alipewa nchi ya malawi baada ya kumtia (alimla malikia wa Uingereza) Queen of England waka muhasi. Alifanya mkataba kuwa atapewa kutawala Malawi
 
Jamaa alizingua sana. Sisi ambao tuko mpakani tulikuwa na taarifa zake nyingi. Inasemekana hakuwa mmalawi bali alikuwa mghana. Alipewa nchi ya malawi baada ya kumtia (alimla malikia wa Uingereza) Queen of England waka muhasi. Alifanya mkataba kuwa atapewa kutawala Malawi
☺☺☺ hapana chifu
Alimtibu malikia kabla ya zoezi la kutibu akaambiwa wamuhasi kwanza ili asije akamtafuna malikia na zawadi yake ilikuwa kuwa rais wa milele nchini kwake malawi
 
Back
Top Bottom