Mfahamu Jenerali James Kabarebe kwa ufupi

kwanza nakupongeza sana mkuu, Nyuzi kama hizi ni chache sana humu ndani
huyu jamaa ndiye alioteka Zaire, Kagame anamuamini sana huyu, kwa kifupi huyu na wenzie walikuwa na uwezo wa kumgeuka kabila na kagame waendeshe zaire wao
Hahah Kabarebe amgeuke Kagame?😂😂😂😂 Naona uko ndotoni mkuu.
 
Haya maujinga ya watusi na wahutu umeyaleta humu ya kazi gani??? Peleka huko kwao
 
Hahah Kabarebe amgeuke Kagame?😂😂😂😂 Naona uko ndotoni mkuu.
Mkuu, nazungumzia "uwezo" ,angetaka angefanya hivo kwa sababu huyu jamaa ndio alikuwa kiongozi wa ile vita na ndiye alikuwa wa kwanza kufika kinshasa akipitia mto congo
jamaa anasema yeye ndiye alimpigia simu kabila kumjulisha tayari mji wa kinshasa umetekwa, yani kwa kifupi huyu ndiye alikuwa anaongea na kabila na kagame direct
na huyu jamaa ndiye aliongoza serikali maana kabila hakufika kinshasa haraka hivo serikali ilikuwa chini yake (ukumbuke silaha nzito na sehemu nyeti kama makao makuu ya jeshi na vituo vya radio vilikuwa kinshasa)
hivo basi, kwa kusema hayo, huyu jamaa alikuwa na uwezo wa kuwageuka kagame, kabila na museveni na akatangaza rais aliyemtaka yeye au yy mwenyewe akawa Rais kwa sababu he had both majority suport and the army
 
Hahah alikua na majority support kutoka kwa nani mkuu?Ya RPA au AFDL au nani?Kama ulikua hujui mchoro wote wa Kuivuruga Congo ulichorwa Kigali na wakina Pk&associates na James alitumwa kutekeleza kilichopangwa kwny ramani tayari na kama ulikua hufahamu Kabarebe alikua ni Bodyguard wa Kagame wkt RPA(wakiwa waasi) ikipambana msituni miaka yote kwa hio huyo ni nyokaa wa PK kama ulikua hufahamu.

Kabarebe ni kichwa na strategist mzuri na alithibitisha hilo kwny Operation Kitona lkn kwenda kinyume na PK ubavu huo hana.

Kagame alishawaambia RPA boys Nyamwasa,Karegeya,wakina Kabarebe na high committee yote ya RPA/F kwamba he made them na yoyote atakayeenda kinyume atapelekwa anakostahili na wanajua hilo na alishatoa mifano kwa baadhi yao.
 
Hapana mkuu naomba nikupinge kigezo cha kwamba mtu akikufunda huwezi furukuta kwake sio cha kweli.

RCD Goma ya Kagame walipotwangana na Museveni kwa mwavuli wa UPC huko kisangani hadi UG kuzidiwa nani angetarajia ilihali Museveni akiwa Rais huyo PK alikua "junior" wake?

Kabarebe alisurvive ambush ya Kitona na siege ya Manquela Do Zombo akiwa zaidi ya 1200 km kutoka kigali hvi mtu wa hivo asingeweza Pambana na PK should he get an opportunity?

Kinachombeba Kagame ni Narrow management tu ya kupokea na kutoa taarifa kupitia channel ndogo sana ya watu hivyo inajenga uoga wa mapinduzi au usaliti otherwise hao generals wange unite wanamtoa asubuhi tu.

kwangu mimi War is about strategy and experience sio cheo au "I made you".... Mifano mingi tu tuomeona mwanafunzi akimpindua mwalimu wake from Sadat to Compaore to Mobutu hao wote waliwapindua waliowafikisha hapo!! So it's not given PK hawezi ondolewa na hao juniors wake.
 
mkuu, 1.majority support ni wananchi
p2.kwa mujibu wa interview aliyofanya huyu jamaa ni kwamba mchongo wa kuvuruga congo ulipanga hapa Tz,yani nyerere alimuintroduce kabila kwa Museven then museven akampleka kabila kwa james ambap james alitumwa na paul
ngoja nitaleta maelezo ya james mwenyewe kwenye documentary
 
Acha kuandika vitu usivyokua na uhakika navyo jomba na kama ni hio documentary ya Kabarebe iliyoko youtube nimeshaiona zaidi ya mara 4 mkuu.

Kagame alisema kama Congo itaendelea kuwapa hifadhi waasi wa serikali iliyopinduliwa/interahamwe ataivuruga Congo na hio ni 1995 na akasema wazi wazi kabisa kuivuruga Congo ni rahisi tu kwa ku train waasi na kuwapa support na ukitaka nitakuwekea hapa gazeti la US likiripoti hio habari.

Na Kagame akatoka hapo akaenda ziara US akawaeleza khs hatari ya inayomkabili kwawaasi kuhifadhiwa Congo na kupewa Support na serikali ya Mobutu,serikali ya US ikampuuza ikaona ka nchi kenyewe kadogo na ka kidwanzi kametoka kuchinjana kataiwezaje kijeshi nchi kama Congo ambayo ni kubwa mara 90 ya ka Rwanda ukitaka pia ntakuwekea hapa washngton post ikiripoti ziara hio ya PK na alichokisema PK.


Khs Kabila senior usichokijua ni kua Kabila alishajaribu kuipindua serikali ya Congo tangu 1967 kupitia chama chake cha People's Revolution Party na akashindwa miaka yote hio lkn kupitia ADFL iliyotengenezwa na wakina Kagame ndipo aliweza kushika nchi(1st congo war),Kabila alikua anaishi Dar so ni kweli M7 alim-link Kabila(nae M7 aliunganishwa na Kabila kupitia usalama wa Taifa wa Tz) kwa kina PK na wakina PK walihitaji mtu ambae wananchi wa Congo watam support kwa kuona ni Mkongo mwenzao kuliko kuona wanyamlenge ndio waliokamata nchi ya Congo.

So kusema mchongo wa kuivuruga Congo ulipangwa Tz sio kweli hata kwa 1%.
 
Sasa yuko wapi?
Ok
 
Mpaka leo yuko kwenye house arrest?
 
Muuwaji na Mhalifu wa Kivita, Jenerali Kabarebe yupo chini ya Ulinzi. Ndiyo malipo ya Utumishi wake uliotukuka kwa Mhalifu mwenzake Paul Kagame. Wacha walane wao wao kwa wao.
 

NADHANI KUMUWEKA UNDER HOUSE ARREST ANAMLINDA ASIJE PELEKWA The Hague KWANI ANATAFUTWA NA U.N.!!
 
haya mambo yanakwenda kama hayaendi vile. Miaka inayoyoma na wao wenyewe wanaendelea kuumbuana mmoja baada ya mwingine.

Wacha tuone mwisho wa movie utakuwaje!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…