Mfahamu Mzee Bin Sudi (1896 – 1972)

Mfahamu Mzee Bin Sudi (1896 – 1972)

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Baada ya kuhangaika kwa miaka mingi sana leo nimejaaliwa kupata picha ya Mzee bin Sudi na picha hii kanipatia mjukuu wake Bi. Subira Mohamed Sudi.

Rafiki yangu na mzungumzaji wangu marehemu Athumani Kassanda (amefariki kiasi cha miezi kama minne iliyopita) siku moja katika mazungumzo yetu ya kawaida nilimuuliza wapi naweza kupata picha ya Mzee bin Sudi.

Sheikh Kassanda alikuwa na taarifa nyingi sana za wazee wa Kimanyema na mama yake Bi. Khadija bint Jaffar alikuwa mmoja wa akina mama katika tawi la TANU lilioanzishwa na Ali Masham.

Historia ya Ali Mshama naamini sasa ni maarufu kwa wasomaji wangu. Sheikh Kassanda akaniuliza kama namfahamu Shukuru Sudi.

Nilimwambia sijamuona miaka mingi na kwa miezi minne ikawa nahangaika kumtafuta Shukuru na leo nikapata simu yake kutoka kwa shoga yake Bi. Sikudhani Kassim ambae kwangu mimi ni shangazi yangu lau kama umri wetu unalingana.

Shukuru alishangaa sana nilipojitambulisha akaniambia mara ya mwisho mimi na yeye kuonana ilikuwa England. Nilifurahi kwa Shukuru kutumia hili neno, ‘’England.’’

Hakika mara ya mwisho mimi na shukuru kuonana ilikuwa Finsbury Park, London mwaka wa 1991.
Wakati huo sote tulikuwa vijana.

Nikamuomba Bi. Shukuru picha ya babu yake na tukafanya mazungumzo kidogo kuhusu babu yake huyu.

Bi. Shukuru akaniahidi kunipa picha nyingine na akaniambia kuwa kuna picha maarufu ya babu yake ilitoka katika gazeti magazeti ya chama Uhuru na Mzalendo.

Picha hii inamuonyesha Mzee bin Sudi akisoma hotuba mbele ya Mwalimu Nyerere na mgeni wake Raisi Jaffar Nimeiri wa Sudan wakiwa ya ofisi ya TANU mwaka wa 1972.

In Shaa Allah picha hii ikipatikana nitaiweka hapa kwa faida yetu sote. Turudi kwa babu yake Bi. Shukuru Mzee bin Sudi.

Hiyo ofisi ya TANU ambayo Mzee bin Sudi alisimama kusoma risala ilikuwa ofisi ya African Association (AA) ambayo yeye akiwa Rais wa AA alishiriki ujenzi wake katika ya mwaka wa 1929 – 1933 na ilifunguliwa na Gavana Donald Cameron mwaka wa 1933.

Picha ya sherehe hiyo ya ufunguzi ipo na bila shaka Mzee bin Sudi alikuwapo katika sherehe hii.
Katika picha hii yuko Gavana na pia Kleist Sykes aliyekuwa Katibu wa AA.

Ofisi hii ya AA ndiyo ikaja kuwa ofisi ya TAA pale mwaka wa 1948 AA ilipobadili jina lake na kuwa TAA.
Hii ndiyo nyumba ambayo TANU iliundwa mwaka wa 1954.

Bila shaka kwa Mzee bin Sudi kusimama mbele ya Nyerere na Nimeiri wakiwa katika ofisi ile ya AA ambayo yeye na wenzake walijenga zaidi ya miaka 40 iliyopita hii ni historia ya pekee.

Lakini nani katika wale wote waliokuwapo pale walikuwa wanaijua historia hii?

Mwaka wa 1933 katika uongozi wa TAA Mzee bin Sudi akiwa Rais na Kleist Sykes Katibu palitokea ugomvi baina ya Kleist Sykes na Erika Fiah.

Erika Fiah ndiyo Mwafrika wa kwanza kuwa na gazeti lake ‘’Kwetu,’’ na ingawa gazeti hili lilikuwa ndiyo sauti ya Waafrika wa Tanganyika lakini mara kwa mara Fiah akituia gazeti hili kumshambulia ‘’Mzulu,’’ Kleist Sykes.

Ugomvi huu ukafikia mahali Kleist akajitoa katika uongozi wa AA na nafasi yake ikashikiliwa na Erika Fiah. AA ikawa inadorora kwa kumkosa Kleist.

Mzee Bin Sudi akamwandikia barua Kleist barua ambayo aliianza kwa ‘’Bismillah Rahaman Rahim.’’
Sikutegemea kuona barua ya AA inatangulizwa na maneno hayo matukufu.

Hii ilinifanya nitake angalau kuona picha ya huyu Mzee bin Sudi alikuwa anafananaje.

Barua hii ni katika nyaraka za Sykes ambazo mimi imeniathiri sana si tu kwa kwa kuanza kwa Jina la Allah bali kwa yale maudhui ndani ya barua ile.

Mzee bin Sudi katika barua ile ya mwaka wa 1933 alimkumbusha Kleist madhumuni yao ya kuikomboa Tanganyika.

Mzee bin Sudi akamwambia Kleist azma yao itafikaje tamati kwa mafanikio ikiwa itakuwaje yeye anajiweka pembeni?

Ifahamike kuwa Mzee bin Sudi alikuwa Rais muaisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Kleist katika barua ya majibu alikiri kuwa kafanya kosa kujiweka pembeni na akamwandikia Mzee bin Sudi maneno haya:

‘’Tupambane kwa nguvu zetu zote kuelekea njia ya ustaarabu kama vile watu wa makabila mengine wanavyofanya. Haidhuru kitu ikiwa hatukamilishi kila kitu.

Wale watakaokuja baada yetu watakamilisha yatakayobakia.’’

Kleist hakuiona Tanganyika huru kwani alifariki mwaka wa 1949 lakini Mzee bin Sudi aliishi na kuiona Tanganyika huru.

Mzee bin Sudi akasimama miezi michache kabla ya kifo chake mwaka wa 1972 kusoma risala mbele ya Nyerere na mgeni wake Jaffar Nimeiri akiwa analiangalia jengo la kupendeza la ofisi ya TANU ambalo chanzo chake ilikuwa ile nyumba yao waliyojenga kwa miti, udongo, chokaa, mawe ya kutomea na kuezekwa na madebe.

Picha hiyo ni Mzee bin Sudi akiwa na wakeze watatu na wajukuu zake akiwa shambani kwake Kwame Mbagala miaka ya mwanzoni 1960s. Huyo aliyekunja mikono ni Shukuru.

Picha ya pili ufunguzi wa ofisi ya African Association mwaka wa 1933. Picha ya tatu ni Erika Fiah.
 
MZEE BIN SUDI (1896 – 1972)

Baada ya kuhangaika kwa miaka mingi sana leo nimejaaliwa kupata picha ya Mzee bin Sudi na picha hii kanipatia mjukuu wake Bi. Shukuru Sudi.

Rafiki yangu na mzungumzaji wangu marehemu Athumani Kassanda (amefariki kiasi cha miezi kama minne iliyopita) siku moja katika mazungumzo yetu ya kawaida nilimuuliza wapi naweza kupata picha ya Mzee bin Sudi.

Sheikh Kassanda alikuwa na taarifa nyingi sana za wazee wa Kimanyema na mama yake Bi. Khadija bint Jaffar alikuwa mmoja wa akina mama katika tawi la TANU lilioanzishwa na Ali Masham.

Historia ya Ali Msham naamini sasa ni maarufu kwa wasomaji wangu.

Sheikh Kassanda akaniuliza kama namfahamu Shukuru Sudi.

Nilimwambia sijamuona miaka mingi na kwa miezi minne ikawa nahangaika kumtafuta Shukuru na leo nikapata simu yake kutoka kwa shoga yake Bi. Sikudhani Kassim ambae kwangu mimi ni shangazi yangu lau kama umri wetu unalingana.

Shukuru alishangaa sana nilipojitambulisha akaniambia mara ya mwisho mimi na yeye kuonana ilikuwa England.

Nilifurahi kwa Shukuru kutumia hili neno, ‘’England.’’

Hakika mara ya mwisho mimi na shukuru kuonana ilikuwa Finsbury Park, London mwaka wa 1991.

Wakati huo sote tulikuwa vijana.

Nikamuomba Bi. Shukuru picha ya babu yake na tukafanya mazungumzo kidogo kuhusu babu yake huyu.

Bi. Shukuru akaniahidi kunipa picha nyingine na akaniambia kuwa kuna picha maarufu ya babu yake ilitoka katika gazeti magazeti ya chama Uhuru na Mzalendo.

Picha hii inamuonyesha Mzee bin Sudi akisoma hotuba mbele ya Mwalimu Nyerere na mgeni wake Raisi Jaffar Nimeiri wa Sudan wakiwa ya ofisi ya TANU mwaka wa 1972.

In Shaa Allah picha hii ikipatikana nitaiweka hapa kwa faida yetu sote.

Turudi kwa babu yake Bi. Shukuru Sudi.

Hiyo ofisi ya TANU ambayo Mzee bin Sudi alisimama kusoma risala ilikuwa ofisi ya African Association (AA) ambayo yeye akiwa Rais wa AA alishiriki ujenzi wake katika ya mwaka wa 1929 – 1933 na ilifunguliwa na Gavana Donald Cameron mwaka wa 1933.

Picha ya sherehe hiyo ya ufunguzi ipo na bila shaka Mzee bin Sudi alikuwapo katika sherehe hii.

Katika picha hii yuko Gavana na pia Kleist Sykes aliyekuwa Katibu wa AA.

Ofisi hii ya AA ndiyo ikaja kuwa ofisi ya TAA pale mwaka wa 1948 AA ilipobadili jina lake na kuwa TAA.

Hii ndiyo nyumba ambayo TANU iliundwa mwaka wa 1954.

Bila shaka kwa Mzee bin Sudi kusimama mbele ya Nyerere na Nimeiri wakiwa katika ofisi ile ya AA ambayo yeye na wenzake walijenga zaidi ya miaka 40 iliyopita hii ni historia ya pekee.

Lakini nani katika wale wote waliokuwapo pale walikuwa wanaijua historia hii?

Mwaka wa 1933 katika uongozi wa TAA Mzee bin Sudi akiwa Rais na Kleist Sykes Katibu palitokea ugomvi baina ya Kleist Sykes na Erika Fiah.

Erika Fiah ndiyo Mwafrika wa kwanza kuwa na gazeti lake ‘’Kwetu,’’ na ingawa gazeti hili lilikuwa ndiyo sauti ya Waafrika wa Tanganyika lakini mara kwa mara Fiah akituia gazeti hili kumshambulia ‘’Mzulu,’’ Kleist Sykes.

Ugomvi huu ukafikia mahali Kleist akajitoa katika uongozi wa AA na nafasi yake ikashikiliwa na Erika Fiah.

AA ikawa inadorora kwa kumkosa Kleist.
Mzee Bin Sudi akamwandikia barua Kleist barua ambayo aliianza kwa ‘’Bismillah Rahaman Rahim.’’

Sikutegemea kuona barua ya AA inatangulizwa na maneno hayo matukufu.

Hii ilinifanya nitake angalau kuona picha ya huyu Mzee bin Sudi alikuwa anafananaje.

Barua hii ni katika nyaraka za Sykes ambazo mimi imeniathiri sana si tu kwa kwa kuanza kwa Jina la Allah bali kwa yale maudhui ndani ya barua ile.

Mzee bin Sudi katika barua ile ya mwaka wa 1933 alimkumbusha Kleist madhumuni yao ya kuikomboa Tanganyika..

Mzee bin Sudi akamwambia Kleist azma yao itafikaje tamati kwa mafanikio ikiwa itakuwaje yeye anajiweka pembeni?

Ifahamike kuwa Mzee bin Sudi alikuwa Rais muaisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Kleist katika barua ya majibu alikiri kuwa kafanya kosa kujiweka pembeni na akamwandikia Mzee bin Sudi maneno haya:

‘’Tupambane kwa nguvu zetu zote kuelekea njia ya ustaarabu kama vile watu wa makabila mengine wanavyofanya.

Haidhuru kitu ikiwa hatukamilishi kila kitu.

Wale watakaokuja baada yetu watakamilisha yatakayobakia.’’

Kleist hakuiona Tanganyika huru kwani alifariki mwaka wa 1949 lakini Mzee bin Sudi aliishi na kuiona Tanganyika huru.

Mzee bin Sudi akasimama miezi michache kabla ya kifo chake mwaka wa 1972 kusoma risala mbele ya Nyerere na mgeni wake Jaffar Nimeiri akiwa analiangalia jengo la kupendeza la ofisi ya TANU ambalo chanzo chake ilikuwa ile nyumba yao waliyojenga kwa miti, udongo, chokaa, mawe ya kutomea na kuezekwa na madebe.

Picha hiyo ni Mzee bin Sudi akiwa na wakeze watatu.

Kushoto ni Bi. Mwashukuru bint Said, Bint Juma, Mzee bin Sudi kambeba mjukuu wake Yasin, Mzee, Shukuru, Fatuma Bint Muhammad.

Kushoto ni Bi. na wajukuu zake akiwa shambani kwake Kwame Mbagala Kuu miaka ya mwanzoni 1960s.

Picha ya pili ufunguzi wa ofisi ya African Association mwaka wa 1933.

Picha ya tatu ni Erika Fiah.

[/QUOTE]Mzee bin Sudi
Screenshot_20201126-152008.jpg
 
Kusoma lisala mbele ya mwl. Nyerere na kuandika barua kwa kuanza na Bismilah nayo ni mambo ya kuyajadili kweli jamani.
 
Kusoma lisala mbele ya mwl. Nyerere na kuandika barua kwa kuanza na Bismilah nayo ni mambo ya kuyajadili kweli jaman
Prince...
''Risala'' si ''Lisala.''

Labda ni kwa kuwa hujui historia ya Dar es Salaam ya miaka ya 1920 wakati Mzee bin Sudi na vijana wenzake wanaunda African Association (AA) mwaka wa 1929 kisha wakaona kuna mambo yanayohusu Waislam lakini wanayapitishia AA hiyo si sawa wakaunda chama kingine Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika.

Na hiyo AA wao Waislam ndiyo wanaongoza hicho chama.

Bahati mbaya huwajui watu hawa wala hujui historia yao na ndiyo unashangaa.

Hata walipokuja kuunda TANU mwaka wa 1954 walikuwa wakifungua mikutano kwa dua.

Msomaji dua alikuwa Sheikh Suleiman Takadiri aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU lililokuwa na wajumbe zaidi ya 120 wote Waislam.

Historia hii inaweza kuwa inakupa tabu kuelewa lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa.
 
Shida yako nini mzee wetu?

Kila unapoandika unasisitiza kuna masuala muhimu ya historia hayaeleweki, watu hawayajui.

Kuna mahali unahoji "nani kati ta waliokuwapo aloijua historia ile"

Inamana wewe unajua kila kitu mzee?!

Sio kila kitu ni historia ya nchi...ukiona jambo watu wamelipuuza basi ujue hilo kwao si-ndwele! Wewe fuatilia kila unachotaka hata historia ya wakwe zako na umuhimu wao katika ujenzi wa taifa, ila sisi tunamjua Nyerere tu na ndo tunae mtambua.

Full stop
 
Shida yako nini mzee wetu?

Kila unapoandika unasisitiza kuna masuala muhimu ya historia hayaeleweki, watu hawayajui.

Kuna mahali unahoji "nani kati ta waliokuwapo aloijua historia ile"...

Inamana wewe unajua kila kitu mzee?!

Sio kila kitu ni historia ya nchi...ukiona jambo watu wamelipuuza basi ujue hilo kwao si-ndwele! Wewe fuatilia kila unachotaka hata historia ya wakwe zako na umuhimu wao katika ujenzi wa taifa...ila sisi tunamjua Nyerere tu na ndo tunae mtambua

Full stop
Kila...
Umeniuliza nini shida yangu.
Sina shida yoyote nashukuru.

Unaniuliza kama mimi ninajua kila kitu.
Hakuna binadamu anaejuwa kila kitu.

Ila mimi nimeandika vitabu kumi vingi vikiwa vya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na kwa ajili hii kueleza mengi ya Julius Nyerere ambayo hayakuwa yanafahamika.

Unasema siyo kila kitu ni historia.
Ikiwa ni tukio la zamani ni historia.

Kuna kupuuza hili ni jambo unalolijua lakini unaona si muhimu.

Sasa hapa inategemea inawezekana hilo ambalo wewe unaona si muhimu kwa mwengine likawa ni muhimu.

Hili la kutaja ''wakwe,'' hapa umenitukana na nakuona umeghadhibika.

Sielewi nini kimekukasirisha.

Unasema, ''Sisi tunamjua Nyerere tu na ndo tunamtambua.''

Hata mimi ninamjua Nyerere tena kuliko unavyoweza kufikiria.

Nyerere kakutana na baba yangu Said Salum Abdallah mwaka wa 1952 nyumbani kwa Abdulwahid Sykes Mtaa wa Sikukuu na Aggrey.

Abdul Sykes akamtambulisha baba yangu kwa Nyerere na yote yaliyopitika baina ya wazalendo hawa wawili kuanzia TAA hadi kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika baba yangu kayaona kwa macho yake.

Miaka mingi sana baadae mimi nikaja kuihifadhi historia hii katika kitabu, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London 1998.

Mimi siweki ''Full Stop.''

Mlango wangu uko wazi kwa majadiliano ya kiungwana hapana haja ya matusi na lugha kali.
 
Kaka Said pole kwa mineno isiyo staha lkn ndiyo maisha,hongera kwa uandishi usiochosha kusoma,kwa stori adhimu,usichoke kutuhabarisha,Mungu baba atakulipa sio haba
 
Kaka Said pole kwa mineno isiyo staha lkn ndiyo maisha,hongera kwa uandishi usiochosha kusoma,kwa stori adhimu,usichoke kutuhabarisha,Mungu baba atakulipa sio haba
Nnangale,
Ahsante sana ndugu yangu.

Historia ya Abdul Sykes na wenzake haikuwa inajulikana.

Ilipowatokea wengi wamepigwa na mshtuko.
Siwalaumu.
 
Huna elimu hata kidogo

Hujui kuna watu wameandikwa kwenye Vitabu vya Mabwana zenu kwa kutajwa tu kuwa ndio Mtu wa kwanza kugundua Ziwa Tanganyika wakati amekuta wenyeji wanavua samaki miaka dahri na dahri

Yaliyokukera kuhusu Huyu Mwamba ndio hayo yametufurahisha na ndio historia yenyewe!
Kusoma lisala mbele ya mwl. Nyerere na kuandika barua kwa kuanza na Bismilah nayo ni mambo ya kuyajadili kweli jaman
 
Back
Top Bottom