Mfahamu Mzee Jumbe Muhammad Tambaza

Mfahamu Mzee Jumbe Muhammad Tambaza

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Alizaliwa January 1891 na kufariki 1978.

Ni miongoni mwa Wazee wa mwanzo, waliompokea, Mwalimu Nyerere kutoka Butiama, alipokuja Jijini Dar es Salaam.

Alimuunga mkono ktk harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika, miaka ya 1950s

Neno, ''Tambaza,'' limetokana na ''Kutambaa,'' au ''Kusambaa,'' eneo kubwa. Diwan Tambaza na nduguze walikuwa watawala wa sehemu mbalimbali za hapa Mzizima siku za nyuma kabla ya Waarabu, Wajerumani na Waingereza kufika.

Nduguze wengine ni..

Diwan Uweje, Diwan Uzasana, Diwani Mwenye-Kuuchimba na Diwan Mwinyi Ndugumbi.

Diwani Mwenye-Kuuchimba, yeye alikuwa akitawala maeneo ya Mtoni Kijichi na Mbagala.

Ukoo wa Diwan Tambaza Zarara Bin Mwinyi-Kitembe ndio waliokuwa wenyeji wa maeneo ya katikati ya Jiji wakati huo.

Eneo la Upanga, kuanzia Daraja la Selender hadi Ikulu ya Magogoni, na kutoka Aga Khan Hospital, Ocean Road..

Hospital, Kivukoni Front (makaburi ya Nduguze yapo pale Wizara ya Utumishi, Magogoni) kwenda Mnara wa Saa pale Uhuru Street.

Eneo la Majengo la Barabara ya Bibi Titi, kwenda Kisutu hadi Kariakoo, liliitwa Tindwa, na ndipo Mji ulipokuwa.

Jina la Mzizima

Eneo la Magogoni hadi Salenda lilijulikana kama Mzizima kutokana na utulivu wake pamoja na wanyama wakali waliokuwepo enzi hizo.

Ikawa kila aliyepita eneo hilo lazima mwili wake uzizime.

Auza Eneo kwa Sultan

Miaka ya 1860s, alimega kuanzia Salenda hadi Magogoni akamuuzia Sultan Majid wa Zanzibar, ambaye alijenga majengo ya Chuo Kikuu

cha Kiislamu, Daru Salaam (hivi sasa Ikulu) na hostel zake, ambazo sasa ni Hospital ya..

Saratani ya Ocean Road.

Kusanyiko la eneo lake la Tindwa, alilouza na la Mzizima alilogawa, ukichanganya na miji ya Kunduchi na Mbwa Maji, ndio yaliyounda Jiji la Dar Es Salaam, jina lililotokana na Daru Salaam.

Wakoloni Watwaa Maeneo

Wakoloni walipokuja, waliipenda madhari ya Upanga.

Wakaona Weusi hawastaili kuishi pale, kina Tambaza wakaamriwa wawapishe Wahindi (daraja la 2).

Hii ni baada ya wao Wazungu(Daraja la 1) kuchukua OysterBay (sasa Masaki)

Makaburi ya Tambaza

Wakolonii hawakutenga sehemu ya kuzikia watu weusi, makaburi ya Kisutu yalikuwa ni ya watu wenye asili ya Kiarabu.

Mwafrika alipelekwe nje ya mji, Kunduchi, Mbweni, Msasani, Bagamoyo na Mwanalumango.

Kuondoa adha hiyo, Mzee Tambaza...

alitoa bure sehemu ya eneo lake litumike kuzikia Waafrika.

Jumbe Tambaza aliwashawishi binamu zake, Mwinyimkuu Mshindo na Diwan Mwinyi Ndungumbi, na wao wakatoa sehemu watu waweze kuzikana.

Maeneo ya Mwinyimkuu, Magomeni Mapipa na Ndugumbi, Magomeni..

Makuti, makaburi ambayo mpaka sasa yanazikia watu wote.

Ziara ya Binti Mfalme
Muhimbili tunayoiona, ilijengwa mwaka 1956, kwa heshima ya Binti Mfalme Margareth II, aliyekuwa na ziara ya kutembelea makoloni, ilitengenezwa,ili aje kuifungua rasmi.

Iliyokuwepo kwa ajili ya watu Weusi ilikuwa ni kama Zahanati tu, jirani na Kituo cha Kati, cha Polisi (Central Police Station) katikati ya Jiji, ikiitwa Sewa Haji Haji Hospital, iliyojengwa na mfadhili kusaidia jamii maskini.

Sewa Haji alikuwa mkazi wa Bagamoyo mwenye asili ya Kibulushi kutoka Persia.

Baada ya kujengwa hospitali ya Muhimbili, jengo moja katika yale matatu makuu, likaitwa Sewa Haji, kama kumbukumbu yake.

Harakati zake ktk kudai Uhuru

Kama niliposema Mwanzo, ktk Wazee waliompokea Mwalimu Mjini, naye ni mmoja wapo.

Alimuita Mwalimu (hapo, Mwalimu Kijana tu) nyumbani kwake, akiwa na Wazee wengine, wamsomea Dua, na kumfanyia tambiko, mabaya yasimpate.

Wakamng'arisha nyota, tayari kwa mapambano ya kudai Uhuru.


Kwenye TANU

Wakati TANU inafanya mkutano wake wa kwanza, pale Arnatoglo, walialikwa Wajumbe 20 tu, akiwemo Mzee Tambaza.

Inasemekana, ilipotokea kutokuelewa kati ya Zuberi Mtemvu..

na Nyerere, Mzee Tambaza alikuwa upande wa Mwalimu.

Kutokana na uaminifu usiotetereka kwa chama, Mzee Jumbe Tambaza na Mwinjuma Mwinyikambi walikuwa na Permanent Seats, kama Wajumbe wa Kamati Kuu, kadhalika Baraza la Wazee.

Mzee Tambaza na Serikali Waburuzana Mahakamani

Mwaka 1950 Mzee Tambaza aliingia ktk mgogoro na Serikali, ilipokuwa inajengwa upya barabara ya Umoja wa Mataifa (UN Road), kutoka Salenda, kuelekea Fire.

Iliamuliwa, baadhi ya..

makaburi yaondolewe, kunyoosha barabara, Mzee Tambaza akagoma, akaenda Mahakamani kufungua "Landmark Case", akashinda.

Ndipo faster akajenga ule Msikiti wa Tambaza, kulinda lile eneo.

Ukitokea Fire, baada ya kupta Swiss Tower, utaona barabara ina kona

Katika Kuthamini Mchango Wake

Iliyokuwa Shule ya Kihindi, enzi za ukoloni, Aga Khan Boys, ikabadilishwa jina, nakuitwa Tambaza Secondary School na Ile Muhimbili Primary, ilikuwa ikiitwa

Aga Khan Girls.

Shule hizi za Aga Khan walikuwa wakisoma Watoto wa Kihindi Tu.

Huyo Ndio Mzee Tambaza

#Gudgudinformer

🙏🏿Thank You🙏🏿
 
alizaliwa January 1891 na kufariki 1978.

Ni miongoni mwa Wazee wa mwanzo, waliompokea, Mwalimu Nyerere kutoka Butiama, alipokuja Jijini Dar es Salaam.
Alimuunga mkono ktk harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika, miaka ya 1950s
Neno, ''𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮,'' limetokana na ''𝗞𝘂𝘁𝗮𝗺𝗯𝗮𝗮,'' au ''𝗞𝘂𝘀𝗮𝗺𝗯𝗮𝗮,'' eneo kubwa. Diwan Tambaza na nduguze walikuwa watawala wa sehemu mbalimbali za hapa 𝗠𝘇𝗶𝘇𝗶𝗺𝗮 siku za nyuma kabla ya Waarabu, Wajerumani na Waingereza kufika.

Nduguze wengine ni..

𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻 𝗨𝘄𝗲𝗷𝗲, 𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻 𝗨𝘇𝗮𝘀𝗮𝗻𝗮, 𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻𝗶 𝗠𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲-𝗞𝘂𝘂𝗰𝗵𝗶𝗺𝗯𝗮 na 𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻 𝗠𝘄𝗶𝗻𝘆𝗶 𝗡𝗱𝘂𝗴𝘂𝗺𝗯𝗶.

𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻𝗶 𝗠𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲-𝗞𝘂𝘂𝗰𝗵𝗶𝗺𝗯𝗮, yeye alikuwa akitawala maeneo ya Mtoni Kijichi na Mbagala.
Ukoo wa 𝗗𝗶𝘄𝗮𝗻 𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮 𝗭𝗮𝗿𝗮𝗿𝗮 𝗕𝗶𝗻 𝗠𝘄𝗶𝗻𝘆𝗶-𝗞𝗶𝘁𝗲𝗺𝗯𝗲 ndio waliokuwa wenyeji wa maeneo ya katikati ya Jiji wakati huo.
Eneo la 𝗨𝗽𝗮𝗻𝗴𝗮, kuanzia Daraja la Selender hadi 𝗜𝗸𝘂𝗹𝘂 𝘆𝗮 𝗠𝗮𝗴𝗼𝗴𝗼𝗻𝗶, na kutoka Aga Khan Hospital, Ocean Road..
Hospital, Kivukoni Front (makaburi ya Nduguze yapo pale Wizara ya Utumishi, Magogoni) kwenda Mnara wa Saa pale 𝗨𝗵𝘂𝗿𝘂 𝗦𝘁𝗿𝗲𝗲𝘁.

Eneo la Majengo la Barabara ya Bibi Titi, kwenda Kisutu hadi Kariakoo, liliitwa 𝗧𝗶𝗻𝗱𝘄𝗮, na ndipo Mji ulipokuwa.
𝗝𝗶𝗻𝗮 𝗹𝗮 𝗠𝘇𝗶𝘇𝗶𝗺𝗮
Eneo la Magogoni hadi Salenda 𝗹𝗶𝗹𝗶𝗷𝘂𝗹𝗶𝗸𝗮𝗻𝗮 𝗸𝗮𝗺𝗮 𝗠𝘇𝗶𝘇𝗶𝗺𝗮 𝗸𝘂𝘁𝗼𝗸𝗮𝗻𝗮 𝗻𝗮 𝘂𝘁𝘂𝗹𝗶𝘃𝘂 𝘄𝗮𝗸𝗲 pamoja na wanyama wakali waliokuwepo enzi hizo.

Ikawa kila aliyepita eneo hilo lazima mwili wake uzizime.
𝗔𝘂𝘇𝗮 𝗘𝗻𝗲𝗼 𝗸𝘄𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘁𝗮𝗻
Miaka ya 1860s, alimega kuanzia Salenda hadi Magogoni akamuuzia Sultan Majid wa Zanzibar, ambaye alijenga majengo ya 𝗖𝗵𝘂𝗼 𝗞𝗶𝗸𝘂𝘂
cha Kiislamu, 𝗗𝗮𝗿𝘂 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺 (hivi sasa Ikulu) na hostel zake, ambazo sasa ni Hospital ya..
Saratani ya 𝗢𝗰𝗲𝗮𝗻 𝗥𝗼𝗮𝗱.

Kusanyiko la eneo lake la 𝗧𝗶𝗻𝗱𝘄𝗮, alilouza na la 𝗠𝘇𝗶𝘇𝗶𝗺𝗮 alilogawa, ukichanganya na miji ya 𝗞𝘂𝗻𝗱𝘂𝗰𝗵𝗶 na 𝗠𝗯𝘄𝗮 𝗠𝗮𝗷𝗶, ndio yaliyounda Jiji la 𝗗𝗮𝗿 𝗘𝘀 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺, jina lililotokana na 𝗗𝗮𝗿𝘂 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺.
𝗪𝗮𝗸𝗼𝗹𝗼𝗻𝗶 𝗪𝗮𝘁𝘄𝗮𝗮 𝗠𝗮𝗲𝗻𝗲𝗼
Wakoloni walipokuja, waliipenda madhari ya 𝗨𝗽𝗮𝗻𝗴𝗮.

Wakaona Weusi hawastaili kuishi pale, kina Tambaza wakaamriwa wawapishe Wahindi (daraja la 2).

Hii ni baada ya wao Wazungu(Daraja la 1) kuchukua OysterBay (sasa Masaki)
𝗠𝗮𝗸𝗮𝗯𝘂𝗿𝗶 𝘆𝗮 𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮
Wakolonii hawakutenga sehemu ya kuzikia watu weusi, makaburi ya Kisutu yalikuwa ni ya watu wenye asili ya Kiarabu.

Mwafrika alipelekwe nje ya mji, Kunduchi, Mbweni, Msasani, Bagamoyo na Mwanalumango.

Kuondoa adha hiyo, Mzee Tambaza...
alitoa bure sehemu ya eneo lake litumike kuzikia Waafrika.

Jumbe Tambaza aliwashawishi binamu zake, 𝗠𝘄𝗶𝗻𝘆𝗶𝗺𝗸𝘂𝘂 Mshindo na Diwan Mwinyi 𝗡𝗱𝘂𝗻𝗴𝘂𝗺𝗯𝗶, na wao wakatoa sehemu watu waweze kuzikana.

Maeneo ya Mwinyimkuu, Magomeni Mapipa na Ndugumbi, Magomeni..
Makuti, makaburi ambayo mpaka sasa yanazikia watu wote.

𝗭𝗶𝗮𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝗕𝗶𝗻𝘁𝗶 𝗠𝗳𝗮𝗹𝗺𝗲
Muhimbili tunayoiona, ilijengwa mwaka 1956, kwa heshima ya Binti Mfalme 𝗠𝗮𝗿𝗴𝗮𝗿𝗲𝘁𝗵 𝗜𝗜, aliyekuwa na ziara ya kutembelea makoloni, ilitengenezwa,ili aje kuifungua rasmi.
Iliyokuwepo kwa ajili ya watu Weusi ilikuwa ni kama Zahanati tu, jirani na Kituo cha Kati, cha Polisi (𝗖𝗲𝗻𝘁𝗿𝗮𝗹 𝗣𝗼𝗹𝗶𝗰𝗲 𝗦𝘁𝗮𝘁𝗶𝗼𝗻) katikati ya Jiji, ikiitwa 𝗦𝗲𝘄𝗮 𝗛𝗮𝗷𝗶 Haji Hospital, iliyojengwa na mfadhili kusaidia jamii maskini.
Sewa Haji alikuwa mkazi wa Bagamoyo mwenye asili ya 𝗞𝗶𝗯𝘂𝗹𝘂𝘀𝗵𝗶 kutoka 𝗣𝗲𝗿𝘀𝗶𝗮.

Baada ya kujengwa hospitali ya Muhimbili, jengo moja katika yale matatu makuu, likaitwa Sewa Haji, kama kumbukumbu yake.
𝗛𝗮𝗿𝗮𝗸𝗮𝘁𝗶 𝘇𝗮𝗸𝗲 𝗸𝘁𝗸 𝗸𝘂𝗱𝗮𝗶 𝗨𝗵𝘂𝗿𝘂
Kama niliposema Mwanzo, ktk Wazee waliompokea Mwalimu Mjini, naye ni mmoja wapo.

Alimuita Mwalimu (hapo, Mwalimu Kijana tu) nyumbani kwake, akiwa na Wazee wengine, wamsomea Dua, na kumfanyia tambiko, mabaya yasimpate.
Wakamng'arisha nyota, tayari kwa mapambano ya kudai Uhuru.

𝗞𝘄𝗲𝗻𝘆𝗲 𝗧𝗔𝗡𝗨
Wakati TANU inafanya mkutano wake wa kwanza, pale 𝗔𝗿𝗻𝗮𝘁𝗼𝗴𝗹𝗼, walialikwa Wajumbe 20 tu, akiwemo Mzee Tambaza.

Inasemekana, ilipotokea kutokuelewa kati ya 𝗭𝘂𝗯𝗲𝗿𝗶 𝗠𝘁𝗲𝗺𝘃𝘂..
na Nyerere, Mzee Tambaza alikuwa upande wa Mwalimu.

Kutokana na uaminifu usiotetereka kwa chama, Mzee Jumbe 𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮 na 𝗠𝘄𝗶𝗻𝗷𝘂𝗺𝗮 𝗠𝘄𝗶𝗻𝘆𝗶𝗸𝗮𝗺𝗯𝗶 walikuwa na 𝗣𝗲𝗿𝗺𝗮𝗻𝗲𝗻𝘁 𝗦𝗲𝗮𝘁𝘀, kama Wajumbe wa Kamati Kuu, kadhalika Baraza la Wazee.
𝗠𝘇𝗲𝗲 𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮 𝗻𝗮 𝗦𝗲𝗿𝗶𝗸𝗮𝗹𝗶 𝗪𝗮𝗯𝘂𝗿𝘂𝘇𝗮𝗻𝗮 𝗠𝗮𝗵𝗮𝗸𝗮𝗺𝗮𝗻𝗶
Mwaka 1950 Mzee Tambaza aliingia ktk mgogoro na Serikali, ilipokuwa inajengwa upya barabara ya Umoja wa Mataifa (𝗨𝗡 𝗥𝗼𝗮𝗱), kutoka Salenda, kuelekea Fire.

Iliamuliwa, baadhi ya..
makaburi yaondolewe, kunyoosha barabara, Mzee Tambaza akagoma, akaenda Mahakamani kufungua "𝗟𝗮𝗻𝗱𝗺𝗮𝗿𝗸 𝗖𝗮𝘀𝗲", akashinda.

Ndipo faster akajenga ule Msikiti wa Tambaza, kulinda lile eneo.

Ukitokea Fire, baada ya kupta 𝗦𝘄𝗶𝘀𝘀 𝗧𝗼𝘄𝗲𝗿, utaona barabara ina kona
𝗞𝗮𝘁𝗶𝗸𝗮 𝗞𝘂𝘁𝗵𝗮𝗺𝗶𝗻𝗶 𝗠𝗰𝗵𝗮𝗻𝗴𝗼 𝗪𝗮𝗸𝗲
Iliyokuwa Shule ya Kihindi, enzi za ukoloni, 𝗔𝗴𝗮 𝗞𝗵𝗮𝗻 𝗕𝗼𝘆𝘀, ikabadilishwa jina, nakuitwa 𝗧𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗮 𝗦𝗲𝗰𝗼𝗻𝗱𝗮𝗿𝘆 𝗦𝗰𝗵𝗼𝗼𝗹 na Ile 𝗠𝘂𝗵𝗶𝗺𝗯𝗶𝗹𝗶 𝗣𝗿𝗶𝗺𝗮𝗿𝘆, ilikuwa ikiitwa
𝗔𝗴𝗮 𝗞𝗵𝗮𝗻 𝗚𝗶𝗿𝗹𝘀.

Shule hizi za Aga Khan walikuwa wakisoma Watoto wa Kihindi Tu.

𝙃𝙪𝙮𝙤 𝙉𝙙𝙞𝙤 𝙈𝙯𝙚𝙚 𝙏𝙖𝙢𝙗𝙖𝙯𝙖

#Gudgudinformer

🙏🏿𝗧𝗵𝗮𝗻𝗸 𝗬𝗼𝘂🙏🏿
Ahsante kwa historia nzuri,endelea mkuu!
 
Sijaona jina hata moja la mgalatia katika watu wote wenye historia na hii nchi na hasa walioupambania mji huo wa daressalaam, cha ajabu wagalatia wana wadharau waislam na wazaramo wakti ndio born town.
 
Kuna hotuba moja Nyerere anahadithia jinsi alivyorushwa shimo katika matambiko na Jumbe Tambaza, huku Jumbe Tambaza akisema Gavana Twining shwaini tu.

Nyerere na Ukatoliki wake alikuwa anaheshimu sana mambo ya mila.

Kuanzia hapo Gavana akawa hawezi kumwambia kitu Nyerere.

Mzee Pambe alikuwa anaimba wimbo wake mmoja pake makaburini. Akikumbuka siku za zamani.

"Jumbe Tambaza mfano, mtu wa watu.
Akiwa na rupia tano, atagawa tatu."
 
Historia Nzuri. Ukisoma Sheria ya Ardhi, katika Land History in Tanzania, basi huyu Mzee Muhamed Tambaza utakutana na jina lake humo. Namna ambavyo wakoloni walipata shida kwenye kutwaa eneo Lake hapo Tambaza kwa minajili ya upimaji/mipango miji.
 
Back
Top Bottom