Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 16,464
- 35,629
Alizaliwa January 1891 na kufariki 1978.
Ni miongoni mwa Wazee wa mwanzo, waliompokea, Mwalimu Nyerere kutoka Butiama, alipokuja Jijini Dar es Salaam.
Alimuunga mkono ktk harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika, miaka ya 1950s
Neno, ''Tambaza,'' limetokana na ''Kutambaa,'' au ''Kusambaa,'' eneo kubwa. Diwan Tambaza na nduguze walikuwa watawala wa sehemu mbalimbali za hapa Mzizima siku za nyuma kabla ya Waarabu, Wajerumani na Waingereza kufika.
Nduguze wengine ni..
Diwan Uweje, Diwan Uzasana, Diwani Mwenye-Kuuchimba na Diwan Mwinyi Ndugumbi.
Diwani Mwenye-Kuuchimba, yeye alikuwa akitawala maeneo ya Mtoni Kijichi na Mbagala.
Ukoo wa Diwan Tambaza Zarara Bin Mwinyi-Kitembe ndio waliokuwa wenyeji wa maeneo ya katikati ya Jiji wakati huo.
Eneo la Upanga, kuanzia Daraja la Selender hadi Ikulu ya Magogoni, na kutoka Aga Khan Hospital, Ocean Road..
Hospital, Kivukoni Front (makaburi ya Nduguze yapo pale Wizara ya Utumishi, Magogoni) kwenda Mnara wa Saa pale Uhuru Street.
Eneo la Majengo la Barabara ya Bibi Titi, kwenda Kisutu hadi Kariakoo, liliitwa Tindwa, na ndipo Mji ulipokuwa.
Jina la Mzizima
Eneo la Magogoni hadi Salenda lilijulikana kama Mzizima kutokana na utulivu wake pamoja na wanyama wakali waliokuwepo enzi hizo.
Ikawa kila aliyepita eneo hilo lazima mwili wake uzizime.
Auza Eneo kwa Sultan
Miaka ya 1860s, alimega kuanzia Salenda hadi Magogoni akamuuzia Sultan Majid wa Zanzibar, ambaye alijenga majengo ya Chuo Kikuu
cha Kiislamu, Daru Salaam (hivi sasa Ikulu) na hostel zake, ambazo sasa ni Hospital ya..
Saratani ya Ocean Road.
Kusanyiko la eneo lake la Tindwa, alilouza na la Mzizima alilogawa, ukichanganya na miji ya Kunduchi na Mbwa Maji, ndio yaliyounda Jiji la Dar Es Salaam, jina lililotokana na Daru Salaam.
Wakoloni Watwaa Maeneo
Wakoloni walipokuja, waliipenda madhari ya Upanga.
Wakaona Weusi hawastaili kuishi pale, kina Tambaza wakaamriwa wawapishe Wahindi (daraja la 2).
Hii ni baada ya wao Wazungu(Daraja la 1) kuchukua OysterBay (sasa Masaki)
Makaburi ya Tambaza
Wakolonii hawakutenga sehemu ya kuzikia watu weusi, makaburi ya Kisutu yalikuwa ni ya watu wenye asili ya Kiarabu.
Mwafrika alipelekwe nje ya mji, Kunduchi, Mbweni, Msasani, Bagamoyo na Mwanalumango.
Kuondoa adha hiyo, Mzee Tambaza...
alitoa bure sehemu ya eneo lake litumike kuzikia Waafrika.
Jumbe Tambaza aliwashawishi binamu zake, Mwinyimkuu Mshindo na Diwan Mwinyi Ndungumbi, na wao wakatoa sehemu watu waweze kuzikana.
Maeneo ya Mwinyimkuu, Magomeni Mapipa na Ndugumbi, Magomeni..
Makuti, makaburi ambayo mpaka sasa yanazikia watu wote.
Ziara ya Binti Mfalme
Muhimbili tunayoiona, ilijengwa mwaka 1956, kwa heshima ya Binti Mfalme Margareth II, aliyekuwa na ziara ya kutembelea makoloni, ilitengenezwa,ili aje kuifungua rasmi.
Iliyokuwepo kwa ajili ya watu Weusi ilikuwa ni kama Zahanati tu, jirani na Kituo cha Kati, cha Polisi (Central Police Station) katikati ya Jiji, ikiitwa Sewa Haji Haji Hospital, iliyojengwa na mfadhili kusaidia jamii maskini.
Sewa Haji alikuwa mkazi wa Bagamoyo mwenye asili ya Kibulushi kutoka Persia.
Baada ya kujengwa hospitali ya Muhimbili, jengo moja katika yale matatu makuu, likaitwa Sewa Haji, kama kumbukumbu yake.
Harakati zake ktk kudai Uhuru
Kama niliposema Mwanzo, ktk Wazee waliompokea Mwalimu Mjini, naye ni mmoja wapo.
Alimuita Mwalimu (hapo, Mwalimu Kijana tu) nyumbani kwake, akiwa na Wazee wengine, wamsomea Dua, na kumfanyia tambiko, mabaya yasimpate.
Wakamng'arisha nyota, tayari kwa mapambano ya kudai Uhuru.
Kwenye TANU
Wakati TANU inafanya mkutano wake wa kwanza, pale Arnatoglo, walialikwa Wajumbe 20 tu, akiwemo Mzee Tambaza.
Inasemekana, ilipotokea kutokuelewa kati ya Zuberi Mtemvu..
na Nyerere, Mzee Tambaza alikuwa upande wa Mwalimu.
Kutokana na uaminifu usiotetereka kwa chama, Mzee Jumbe Tambaza na Mwinjuma Mwinyikambi walikuwa na Permanent Seats, kama Wajumbe wa Kamati Kuu, kadhalika Baraza la Wazee.
Mzee Tambaza na Serikali Waburuzana Mahakamani
Mwaka 1950 Mzee Tambaza aliingia ktk mgogoro na Serikali, ilipokuwa inajengwa upya barabara ya Umoja wa Mataifa (UN Road), kutoka Salenda, kuelekea Fire.
Iliamuliwa, baadhi ya..
makaburi yaondolewe, kunyoosha barabara, Mzee Tambaza akagoma, akaenda Mahakamani kufungua "Landmark Case", akashinda.
Ndipo faster akajenga ule Msikiti wa Tambaza, kulinda lile eneo.
Ukitokea Fire, baada ya kupta Swiss Tower, utaona barabara ina kona
Katika Kuthamini Mchango Wake
Iliyokuwa Shule ya Kihindi, enzi za ukoloni, Aga Khan Boys, ikabadilishwa jina, nakuitwa Tambaza Secondary School na Ile Muhimbili Primary, ilikuwa ikiitwa
Aga Khan Girls.
Shule hizi za Aga Khan walikuwa wakisoma Watoto wa Kihindi Tu.
Huyo Ndio Mzee Tambaza
#Gudgudinformer
🙏🏿Thank You🙏🏿
Ni miongoni mwa Wazee wa mwanzo, waliompokea, Mwalimu Nyerere kutoka Butiama, alipokuja Jijini Dar es Salaam.
Alimuunga mkono ktk harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika, miaka ya 1950s
Neno, ''Tambaza,'' limetokana na ''Kutambaa,'' au ''Kusambaa,'' eneo kubwa. Diwan Tambaza na nduguze walikuwa watawala wa sehemu mbalimbali za hapa Mzizima siku za nyuma kabla ya Waarabu, Wajerumani na Waingereza kufika.
Nduguze wengine ni..
Diwan Uweje, Diwan Uzasana, Diwani Mwenye-Kuuchimba na Diwan Mwinyi Ndugumbi.
Diwani Mwenye-Kuuchimba, yeye alikuwa akitawala maeneo ya Mtoni Kijichi na Mbagala.
Ukoo wa Diwan Tambaza Zarara Bin Mwinyi-Kitembe ndio waliokuwa wenyeji wa maeneo ya katikati ya Jiji wakati huo.
Eneo la Upanga, kuanzia Daraja la Selender hadi Ikulu ya Magogoni, na kutoka Aga Khan Hospital, Ocean Road..
Hospital, Kivukoni Front (makaburi ya Nduguze yapo pale Wizara ya Utumishi, Magogoni) kwenda Mnara wa Saa pale Uhuru Street.
Eneo la Majengo la Barabara ya Bibi Titi, kwenda Kisutu hadi Kariakoo, liliitwa Tindwa, na ndipo Mji ulipokuwa.
Jina la Mzizima
Eneo la Magogoni hadi Salenda lilijulikana kama Mzizima kutokana na utulivu wake pamoja na wanyama wakali waliokuwepo enzi hizo.
Ikawa kila aliyepita eneo hilo lazima mwili wake uzizime.
Auza Eneo kwa Sultan
Miaka ya 1860s, alimega kuanzia Salenda hadi Magogoni akamuuzia Sultan Majid wa Zanzibar, ambaye alijenga majengo ya Chuo Kikuu
cha Kiislamu, Daru Salaam (hivi sasa Ikulu) na hostel zake, ambazo sasa ni Hospital ya..
Saratani ya Ocean Road.
Kusanyiko la eneo lake la Tindwa, alilouza na la Mzizima alilogawa, ukichanganya na miji ya Kunduchi na Mbwa Maji, ndio yaliyounda Jiji la Dar Es Salaam, jina lililotokana na Daru Salaam.
Wakoloni Watwaa Maeneo
Wakoloni walipokuja, waliipenda madhari ya Upanga.
Wakaona Weusi hawastaili kuishi pale, kina Tambaza wakaamriwa wawapishe Wahindi (daraja la 2).
Hii ni baada ya wao Wazungu(Daraja la 1) kuchukua OysterBay (sasa Masaki)
Makaburi ya Tambaza
Wakolonii hawakutenga sehemu ya kuzikia watu weusi, makaburi ya Kisutu yalikuwa ni ya watu wenye asili ya Kiarabu.
Mwafrika alipelekwe nje ya mji, Kunduchi, Mbweni, Msasani, Bagamoyo na Mwanalumango.
Kuondoa adha hiyo, Mzee Tambaza...
alitoa bure sehemu ya eneo lake litumike kuzikia Waafrika.
Jumbe Tambaza aliwashawishi binamu zake, Mwinyimkuu Mshindo na Diwan Mwinyi Ndungumbi, na wao wakatoa sehemu watu waweze kuzikana.
Maeneo ya Mwinyimkuu, Magomeni Mapipa na Ndugumbi, Magomeni..
Makuti, makaburi ambayo mpaka sasa yanazikia watu wote.
Ziara ya Binti Mfalme
Muhimbili tunayoiona, ilijengwa mwaka 1956, kwa heshima ya Binti Mfalme Margareth II, aliyekuwa na ziara ya kutembelea makoloni, ilitengenezwa,ili aje kuifungua rasmi.
Iliyokuwepo kwa ajili ya watu Weusi ilikuwa ni kama Zahanati tu, jirani na Kituo cha Kati, cha Polisi (Central Police Station) katikati ya Jiji, ikiitwa Sewa Haji Haji Hospital, iliyojengwa na mfadhili kusaidia jamii maskini.
Sewa Haji alikuwa mkazi wa Bagamoyo mwenye asili ya Kibulushi kutoka Persia.
Baada ya kujengwa hospitali ya Muhimbili, jengo moja katika yale matatu makuu, likaitwa Sewa Haji, kama kumbukumbu yake.
Harakati zake ktk kudai Uhuru
Kama niliposema Mwanzo, ktk Wazee waliompokea Mwalimu Mjini, naye ni mmoja wapo.
Alimuita Mwalimu (hapo, Mwalimu Kijana tu) nyumbani kwake, akiwa na Wazee wengine, wamsomea Dua, na kumfanyia tambiko, mabaya yasimpate.
Wakamng'arisha nyota, tayari kwa mapambano ya kudai Uhuru.
Kwenye TANU
Wakati TANU inafanya mkutano wake wa kwanza, pale Arnatoglo, walialikwa Wajumbe 20 tu, akiwemo Mzee Tambaza.
Inasemekana, ilipotokea kutokuelewa kati ya Zuberi Mtemvu..
na Nyerere, Mzee Tambaza alikuwa upande wa Mwalimu.
Kutokana na uaminifu usiotetereka kwa chama, Mzee Jumbe Tambaza na Mwinjuma Mwinyikambi walikuwa na Permanent Seats, kama Wajumbe wa Kamati Kuu, kadhalika Baraza la Wazee.
Mzee Tambaza na Serikali Waburuzana Mahakamani
Mwaka 1950 Mzee Tambaza aliingia ktk mgogoro na Serikali, ilipokuwa inajengwa upya barabara ya Umoja wa Mataifa (UN Road), kutoka Salenda, kuelekea Fire.
Iliamuliwa, baadhi ya..
makaburi yaondolewe, kunyoosha barabara, Mzee Tambaza akagoma, akaenda Mahakamani kufungua "Landmark Case", akashinda.
Ndipo faster akajenga ule Msikiti wa Tambaza, kulinda lile eneo.
Ukitokea Fire, baada ya kupta Swiss Tower, utaona barabara ina kona
Katika Kuthamini Mchango Wake
Iliyokuwa Shule ya Kihindi, enzi za ukoloni, Aga Khan Boys, ikabadilishwa jina, nakuitwa Tambaza Secondary School na Ile Muhimbili Primary, ilikuwa ikiitwa
Aga Khan Girls.
Shule hizi za Aga Khan walikuwa wakisoma Watoto wa Kihindi Tu.
Huyo Ndio Mzee Tambaza
#Gudgudinformer
🙏🏿Thank You🙏🏿