Mfanyabiashara na Dereva Kortini kwa Umiliki Haramu wa Ethanol na Kugushi Stempu za TRA

Mfanyabiashara na Dereva Kortini kwa Umiliki Haramu wa Ethanol na Kugushi Stempu za TRA

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mfanyabiashara, Novita Shirima (49) na dereva, Justine Mbise (29) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro wakikabiliwa na mashtaka sita, ikiwemo kumiliki kemikali aina ya ethanol kinyume cha sheria, kughushi stempu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kutumia nembo bandia za bidhaa za vileo.

Wakili wa Serikali, Frank Wambura, amedai mahakamani hapo kuwa Oktoba 10, 2024, Shimud alikutwa na lita 310 za ethanol, pamoja na chupa zenye nembo bandia za k-vant, konyagi, na highlife. Washtakiwa wote wamekana mashtaka hayo.

Soma Pia: Matumizi ya Kemikali ya Ethanol yanaweza kuathiri ini na kusababisha Saratani

Upande wa mashtaka uliomba washtakiwa waendelee kushikiliwa, ukidai makosa hayo hayana dhamana. Hata hivyo, mawakili wa utetezi walidai wateja wao wanastahili dhamana kisheria.

Baada ya kupitia hoja za pande zote, Hakimu Mkisi aliruhusu dhamana kwa masharti ya wadhamini wawili watumishi wa serikali, dhamana ya Sh10 milioni kwa kila mmoja, na kiwanja chenye thamani ya Sh100 milioni ndani ya Wilaya ya Moshi. Kesi hiyo itatajwa tena Machi 5, 2025.
 
Haya mavilevi feki hayanayokunywa hovyo hovyo vijana yatakuja wafikisha pabaya sana baadae.
 
Mfanyabiashara, Novita Shirima (49) na dereva, Justine Mbise (29) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro wakikabiliwa na mashtaka sita, ikiwemo kumiliki kemikali aina ya ethanol kinyume cha sheria, kughushi stempu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kutumia nembo bandia za bidhaa za vileo.

Wakili wa Serikali, Frank Wambura, amedai mahakamani hapo kuwa Oktoba 10, 2024, Shimud alikutwa na lita 310 za ethanol, pamoja na chupa zenye nembo bandia za k-vant, konyagi, na highlife. Washtakiwa wote wamekana mashtaka hayo.

Soma Pia: Matumizi ya Kemikali ya Ethanol yanaweza kuathiri ini na kusababisha Saratani

Upande wa mashtaka uliomba washtakiwa waendelee kushikiliwa, ukidai makosa hayo hayana dhamana. Hata hivyo, mawakili wa utetezi walidai wateja wao wanastahili dhamana kisheria.

Baada ya kupitia hoja za pande zote, Hakimu Mkisi aliruhusu dhamana kwa masharti ya wadhamini wawili watumishi wa serikali, dhamana ya Sh10 milioni kwa kila mmoja, na kiwanja chenye thamani ya Sh100 milioni ndani ya Wilaya ya Moshi. Kesi hiyo itatajwa tena Machi 5, 2025.
Suala la TBS na TMDA hili
 
Mangi hapa ametuangusha sana, hata kama ni tamaa ya pesa sasa huku amefika mbali, vijana wanaangamia sana kwa hizi pombe kali ambazo ni feki
 
Vinywaji feki vingi sana, ndio maana hata visunguravsiku hizi havina stimu kabisa.
 
Ohoo! hapa sasa ni kutafuna wine tu!
 
Mtuambie na product zao sasa...ethanol hiyo hawaoshei viatu!
 
Back
Top Bottom