Mfanyabiashara Ulomi apotea, familia na Polisi wanamtafuta

Mfanyabiashara Ulomi apotea, familia na Polisi wanamtafuta

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
IMG_2299.jpeg
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limesema December 12, 2024 katika kituo cha Polisi Chang'ombe, Temeke ilipokelewa taarifa ya kutafutwa na Familia yake Mtu aitwaye Daisle Simon Ulomi, Mfanyabiashara ambaye hakurudi nyumbani kwake toka alipoingia kazini kwake December 11, 2024.

Taarifa iliyotolewa leo December 14,2024 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumane Muliro imesema "Inadaiwa siku hiyo alionekana akitoka ofisini kwake Sinza Kijiweni majira ya saa 6:00 mchana kuelekea Mbagala, Bandari kavu alikodai anaenda kukagua kontena la bidhaa zake baada ya kuitwa na Watu aliodai ndiyo waliokuwa wanashughulika na kutoa kontena hilo bandarini na alikuwa akitumia pikipiki namba MC 415 DQC aliyokuwa akiendesha mwenyewe"

"Ufuatiliaji wa taarifa hiyo unafanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Ndugu ili kujua na kubaini Mtu huyo yupo wapi, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa yeyote mwenye taarita kuhusiana na Mtu huyo azitoe kwenye mamlaka yoyote ya Serikali illyo karibu yake"

Kupata matukio ya nyuma kuhusu watu wasiyojulikana ingia hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Taarifa hiyo ya Polisi imekuja saa chache baada ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob kutoa taarifa ya kupotea kwa Ulomi ambapo amesema aliondoka Sinza kwenda Mbagala Bandari kavu alipoenda kukagua kontena lake baada ya kuitwa na Watu wa TRA kwa ajili ya ukaguzi na namba yake ya simu aliyokuwa anaitumia ni 0653630313 "Ndugu zake wamemtafuta vituo vyote vya Polisi nakupewa.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limesema December 12, 2024 katika kituo cha Polisi Chang'ombe, Temeke ilipokelewa taarifa ya kutafutwa na Familia yake Mtu aitwaye Daisle Simon Ulomi, Mfanyabiashara ambaye hakurudi nyumbani kwake toka alipoingia kazini kwake December 11, 2024.

Taarifa iliyotolewa leo December 14,2024 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumane Muliro imesema "Inadaiwa siku hiyo alionekana akitoka ofisini kwake Sinza Kijiweni majira ya saa 6:00 mchana kuelekea Mbagala, Bandari kavu alikodai anaenda kukagua kontena la bidhaa zake baada ya kuitwa na Watu aliodai ndiyo waliokuwa wanashughulika na kutoa kontena hilo bandarini na alikuwa akitumia pikipiki namba MC 415 DQC aliyokuwa akiendesha mwenyewe"

"Ufuatiliaji wa taarifa hiyo unafanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Ndugu ili kujua na kubaini Mtu huyo yupo wapi, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa yeyote mwenye taarita kuhusiana na Mtu huyo azitoe kwenye mamlaka yoyote ya Serikali illyo karibu yake"

Taarifa hiyo ya Polisi imekuja saa chache baada ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob kutoa taarifa ya kupotea kwa Ulomi ambapo amesema aliondoka Sinza kwenda Mbagala Bandari kavu alipoenda kukagua kontena lake baada ya kuitwa na Watu wa TRA kwa ajili ya ukaguzi na namba yake ya simu aliyokuwa anaitumia ni 0653630313 "Ndugu zake wamemtafuta vituo vyote vya Polisi nakupewa

+
Hivi inakuaje kila drama ya utekaji huyu Jacob ndio mtoa taarifa?
 
Na kama ni mfanyabiashara hapo lazima kuna shida (kuthulumiana)
''kuthulumia'' ndiyo nini? Una mawazo ya kijinga kweli kweli. Unatumia na maneno ''kama ni mfanyabishara lazima kuwe na'' utadhani kila mfanyabiashara anayepotea sababu huwa ni kudhulumiana. Kuna wengine wanaweza kuuliwa na majambazi au sababu nyingine kama siasa au mapenzi... Jaribu kupanua upeo wako wa kufikiri...
 
Na kama ni mfanyabiashara hapo lazima kuna shida (kuthulumiana)
Kudhulumiana wakati simu yake imepigwa? Polisi kwanini wasichukue mawasiliano ya simu zilizompigia? Juzi tena yule mwingine wa TRA kauwawa, why TRA?
 
''kuthulumia'' ndiyo nini? Una mawazo ya kijinga kweli kweli. Unatumia na maneno ''kama ni mfanyabishara lazima kuwe na'' utadhani kila mfanyabiashara anayepotea sababu huwa ni kudhulumiana. Kuna wengine wanaweza kuuliwa na majambazi au sababu nyingine kama siasa au mapenzi... Jaribu kupanua upeo wako wa kufikiri...
anatetea uhalifu,Kwa hiyo akidhulumu ndo auawe?
 
Back
Top Bottom