pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 282
- 561
Naandika kwa masikitiko sana, Mimi ni mwenyeji wa Singida ila kishughuli naishi Dar es salaam najishughulisha na shughuli za ulinzi binafsi (bodyguard) hivyo huwa tunazunguka na wateja wangu sehemu mbalimbali (wanamuziki, wafanyabiashara, wanamichezo, wanasiasa nk).
Moja ya sehemu tunazotembelea sana ni sehemu za burudani vilabu vya usiku, kwenye na baa nk, nimesikitika sana kwa miaka hii miwili kumekuwa na idadi kubwa ya wasichana kutoka Singida ama wanyaturu ama wanyiramba wenye umri wa kuanza kidato cha kwanza wakiwa wanatoa huduma katika sehemu hizo za starehe hii inaleta tafsiri kwamba kuna genge la biashara haramu ya wasichana hao mkoa ni Singida ambalo linashawishi wazazi kuwa msichana katika umri wa Miaka 14 na kuendelea anaweza kwenda Dar na kupata ajira nasikitika mkoa wa Singida leo umekuwa kitovu cha kusambaza ma baa maid tena wenye umri wa kwenda shule.
Miaka ya nyuma nakumbuka mkoa wa Iringa ulikuwa maarufu kwa kusambaza wasichana wa ndani (house maid) hongera RC Iringa kwa kuhakikisha watoto wa kike wanaenda shule sikatai ma watoa huduma wengi kwenye baa kuwa wanasingida basi angalau wawe na miaka ya kiutu uzima na biashara ya udalali wa watoto ukomeshwe
Moja ya sehemu tunazotembelea sana ni sehemu za burudani vilabu vya usiku, kwenye na baa nk, nimesikitika sana kwa miaka hii miwili kumekuwa na idadi kubwa ya wasichana kutoka Singida ama wanyaturu ama wanyiramba wenye umri wa kuanza kidato cha kwanza wakiwa wanatoa huduma katika sehemu hizo za starehe hii inaleta tafsiri kwamba kuna genge la biashara haramu ya wasichana hao mkoa ni Singida ambalo linashawishi wazazi kuwa msichana katika umri wa Miaka 14 na kuendelea anaweza kwenda Dar na kupata ajira nasikitika mkoa wa Singida leo umekuwa kitovu cha kusambaza ma baa maid tena wenye umri wa kwenda shule.
Miaka ya nyuma nakumbuka mkoa wa Iringa ulikuwa maarufu kwa kusambaza wasichana wa ndani (house maid) hongera RC Iringa kwa kuhakikisha watoto wa kike wanaenda shule sikatai ma watoa huduma wengi kwenye baa kuwa wanasingida basi angalau wawe na miaka ya kiutu uzima na biashara ya udalali wa watoto ukomeshwe