Mfuko wa serikali wa kuwekeza

Mfuko wa serikali wa kuwekeza

LOVINTAH GYM

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
459
Reaction score
653
SOVEREIGN WEALTH FUND

Kwajina lengine huitwa social wealth fund.

Huu ni mfuko wa serikali ambao husaidia kuepuka athari zinazo sababishwa na nchi kuwa na rasilimali kama mafuta, gas, madini nk

Inshort, huu ni mfuko ambao husaidia kutunza pesa ambazo zinatokana na faida ya nchi kuwa na maliasili.

Huu mfuko unasaidia

1. Kizazi kijacho (akiba itatumika kwa faida ya vizazi vinavyokuja)

2.Husaidia viwanda vya ndani kutokufa kutokana na ushindani wa viwanda vya nje.

3.Sekta zote za uchumi kukua

4.Husaidia pesa kutokushuka thamani

5. Husaidia ku invest kwenye vitu vyengine kwaajili ya faida ya nchi kama gold nk

6.Kuepuka dutch disease

7.Maendeleo na miundombinu ya nchi



Mfano:

Wewe ni mfanyakazi na mshahara wako ni laki 5, ila ukacheza biko au ukashiriki mashindano flani ukapata million 10.

Sasa kwakuwa hukujiandaa kupokea ile million 10, unaweza jikuta umeitumia ile pesa vibaya na mwishowe ile pesa inaisha kwa mda mfupi bila kufanya kitu chochote cha msingi.

Sasa hivyo hivyo kwenye nchi, kuwa kabla nchi haikuwai kujua kuwa imebarikiwa na madini au mafuta au gas, kitendo cha nchi kugundua na kuanza uchimbaji basi nchi itapata pesa nyingi ambazo hazikuwa kwenye budget.

Nchi isipozitenga zile pesa na ku invest kwenye bidhaa ambazo hupanda thamani basi nchi itajikuta inarudi kuwa masikini zaidi ya mwanzo.

Norway ndio nchi inayoongoza kwa kufaidika na rasilimali ya mafuta na gesi, hii ni kwasababu walitunza pesa ambayo imepatikana kwenye mafuta na gas, kwaio wanaendelea kula faida na ile pesa itasaidia vizazi kwa vizazi hata mafuta yakiisha.



#oilandgas #gold #foreigncurrency #economics #sovereignwealthfunds #norway #dutchdisease #naturalresources
wealth-funds.jpg_org.jpg
 
Je mm raia w kawaida inanisaidiaje?
1.Inakusaidia kujua umuhimu wa kuwekeza
2. leo wewe ni wa kawaida kesho unaweza kuwa mtu muhimu katika nchi hii au jamaa ambae ukampa elimu akawa mtu fulani itasaidia nchi yetu kukua kiuchumi.
 
Back
Top Bottom