Mfumo wa vyama vingi Tanzania umefeli; ufutwe CCM watawale milele

Mfumo wa vyama vingi Tanzania umefeli; ufutwe CCM watawale milele

mshale21

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
2,126
Reaction score
5,068
Habarini Wanabodi!

Kulingana na hali halisi inayoendelea nchini;

1) CCM hawako tayari katika suala la Katiba mpya, badala yake wako tayarI kufunga, kubambikia kesi na kunyanyasa Vyama vingine kupitia polisi

2) CCM hawataki tume huru ya uchaguzi, na badala yake kuitumia Tume Kama fimbo ya kuwachapia wapinzani katika uchaguzi

Mimi nashauri, sheria inayohalalisha uwepo wa Vyama vingi Tanzania ifutwe, na iwekwe ya kudumu ya utawala wa chama kimoja, yaani CCM

Hii itasaidia kuondoa chuki, visasi, visa na mambo ya ajabu ajabu yanayoendelea hivi sasa!
 
Hawataki kwani hii nchi ni mali yao? Sema tu Watanzania tuna upole na uoga wa kipumbavu! Siku tukiondokana na hii hali, hakika kuna watu wataikimbia hii nchi!
 
CCM walikubali mfumo wa Vyama vingi kwa shinikizo kutoka kwa Wafadhili.
 
Kwa akili yako hiyo ya ki-ccm unaona umetoa wazo nzuri.
 
Kwa akili yako hiyo ya ki-ccm unaona umetoa wazo nzuri.
Mkuu ukitaka kujua ninachokimaanisha, share experience yako ya kisiasa hapa Kama unayo!

Umeshawah kutungwa, ushawsh kupigwa Risasi, Ulishawah kufungwa?
 
Mkuu ukitaka kujua ninachokimaanisha, share experience yako ya kisiasa hapa Kama unayo!

Umeshawah kutungwa, ushawsh kupigwa Risasi, Ulishawah kufungwa?
Ungelikuwa na akili ungeliunga mkono juhudi za kuleta katiba mpya kwani ya sasa hata Baba wa Taifa akiwa madarakani alisema ni hatari.
 
CCM walikubali mfumo wa Vyama vingi kwa shinikizo kutoka kwa Wafadhili.
Kifup hawako tayar!

Dhana ya multipartism ilikua nzur, lkn utekelezwaj wake ndio shda, ilitakiwa huu utaratibu wautuo, wakiona wako tayar kufanya siasa zinazojenga taifa warudishe! Kwa Hal ilivyo sioni Maana hasa ya Vyama vingi kwa Sasa!
 
Ungelikuwa na akili ungeliunga mkono juhudi za kuleta katiba mpya kwani ya sasa hata Baba wa Taifa akiwa madarakani alisema ni hatari.
Inaonekana hujanielewa bado, dhana ya multipartism ilikua nzur, lakin wenye mamlaka hawako tayar, ndo Maana ya kile kilichowapata akina Mbowe na wenzake juu ya mambo ya katiba mpya!
 
Mfumo Haujafeli Ila Vyama Mbadala Ndo Vimefeli Kutengeneza 'Upinzani' Wa Kweli.... Siku zote Vimejikita Kwenye Matukio, Kama Sasa Vinaidandia hoja Tozo. Wananchi wanakosa Sera Mbadala Ya Kupima...
 
CCM ni kama binti aliyeonja utamu wa dudu kwa maumivu kwaiyo ni nataka sitaki. Anajua akiruhusu katiba mpya mapengo aliyokua yanamfaidisha yatapungua au kuondoka kabisa, akikataa wao wenyewe wanajua hii katiba mbovu haifai kwa sababu inasababisha migogoro ambaayo hata wao inawaadhiri. Mifano ya faida na hasara za mabadiliko ya katiba kwa CCM,
FAIDA,
-mamlaka ya raisi kuteua/kutengua ikimpendeza. Hii raisi kama mwenyekiti wa chama anao uwezo kujaza makada wa chama chake kwenye nafasi mbalimbali nyeti kuhakikisha wanalinda maslahi ya chama ie majaji,polisi ata jeshini na wenyeviti wa tume mbalimbali ie uchaguzi, haki za binadabu nk
-Uwepo wa maRC na maDC Hawa kimsingi wako kutokana na asili ya katiba hii ni ya chama kimoja hivyo vyovyote vile wapo kulinda chama kwa kutumia vyombo vya ulinzi na usalama ndio maana lazima wawe wajumbe wa kamati ya siasa ya chama kwaiyo vyeo vyao sio vya kiutendaji kwa maendeleo ya wananchi
-Muingiliano wa mihimili ya serikali, hii ili ifanye kazi inabidi kuwe na check and balance Sasa kwa katiba yetu hii raisi ni mkuu wa mihimili wa dola lakini anaonekana yupo juu ya mihimili mingine bunge na mahakana ie kuteua majaji, kuwa sehemu ya bunge ie anateua mawaziri, wabunge pia anaweza kulivunja bunge kwaiyo sio bunge wala mahakama inaweza kumuingilia raisi kifupi yeye ni mfalme au malkia
-muudo wa vyombo vya ulinzi na usalama u kwa ajili ya kulinda maslahi ya serikali zaidi ya wananchi. Kwa katiba tuliyonayo tulichukua mfumo na muundo wa hivi vyombo kutoka kwa mkoloni iliachwa hivyo wakati wa chama kimoja mpaka sasa hivyo kwa nguvu ya raisi kama mwenyekiti wa chama anao uwezo kutumia vyombo kukilinda chama chake badala ya wananchi.
Kwa upande mwingine hii katiba ni Kaa la Moto kwa ccm,
-muundo wa muungano uliopo uliunda serikali ya muungano na ya mapinduzi kwaiyo unaleta mkwamo linapokuja masuala ya bara yanashughulikiwaje na serikali ipi kifupi serikali ya muungano imevaa koti la serikali ya bara
-maadili ya viongozi na utawala bora, katiba hii ikiboreshwa wakati wa vuguvugu la ujamaa ambapo viongozi hawakutakiwa kuwa wafanyabiasha lakini sasa ccm imejaa wafanyabiasha na mabwanyeye
-umoja na mshikamano wa kitaifa, kutambua uwepo wa tunu ambazo zinatufanya uwepo wa amani na mshikamano ie lugha kiswahili
Kiujumla Tanzania ya sasa inahitaji katiba itakayotokana na maridhiano pamoja ushirikishwaji wa wananchi katika makundi yote kukidhi nahitaji ya sasa na ya badaye ili kusonga mbele kwani uwepo wa sheria mama(katiba)bora utarahisisha mahusiano uzalishaji kiuchumi, kijamii na nyanja zote
 
Kwa nchi zetu za kiafrika kuwa na demokrasia ni ngumu sana kwa ajili ya umaskini. Chama chochote kikichukua madaraka hakitataka kuachia. CCM wanalijua hilo. Hiyo ndiyo sababu kubwa maana mkiondoka madarakani mtakula wapi.? Viongozi wa Afrika anahakikisha Jeshi, polisi pamoja na usalama wa Taifa wako mikononi mwa Chama kinachotawala na kupiga kura ni kiinua macho tu. Nchi za Afrika upinzani kutoboa ni ngumu sana katika kizazi hiki. Habari mbaya ni vile tu hivi vyama vinaongeza umaskini. Hivi vyama vya Afrika vingeweza kujimbambanua kama Chama kinachotawala China na kuwa serous kujenga uchumi ingekuwa afadhali. Wameharibu sana uchumi na sasa watu wake wanakimbilia Ulaya na huko njiani wanaishia kutupwa baharini. Kuna giza kubwa sana Afrika.
 
Hapana viachwe sisi ccm tunavpenda hatutaki vifutwe
JamiiForums-1797793390.jpg
 
Back
Top Bottom