Mfumuko wa bei Marekani waweka rekodi mpya toka mwaka 1982, Tanzania tunajiaandae?

Mfumuko wa bei Marekani waweka rekodi mpya toka mwaka 1982, Tanzania tunajiaandae?

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Wakati dunia ikianza kupata afueni kutokana na Covid, ghafla inaingia vita ya Russia VS Ukraine na mataifa makubwa ya magharibi yanaungana pamoja kuiwekea vikwazo Urusi. Tofauti na mataifa mengine yanayowekewa vikwazo, Urusi ni namba mbili kwa uzalishaji wa nishati duniani huku mteja wake mkubwa akiwa bara Ulaya.

Mfumuko wa bei Marekani umefika 7.9 kikiwa kiwango cha juu kwa miaka 40 sasa huku vita na vikwazo vyake vikiwa havina dalili ya kupoa. Tanzania ni mtegemezi mkubwa wa mafuta katika uchumi wake hasa sekta ya usafirishaji ambayo ina mchango mkubwa katika mabadiliko ya bei.

Angalau kwenye nishati ya umeme utegemezi wa gesi ya kusini mwa nchi unapunguza haya maumivu. China kaamua kufunga mkataba mpya wa nishati na Saudi Arabia kuyakabili yajayo.

Kama Taifa tumejiaandaje na yajayo yanayoonekana hayafurahishi kama suluhu isipopatika mapema Ukraine.
 
Mfumuko Uliopo Tanzania Ni mara 10 ya huo tokea Mwaka Jana
 
Hata wafanyakazi huko pia wanalalamika kuwa masaa ya kazi wengi wao yamepunguzwa na hata siku za kufanya kazi zimepunguzwa kutoka katika baadhi ya makampuni kutokana na kuzorota kwa uchumi
 
Tz nina uhakika tumevuka hiyo ya USA
 
Wakati dunia ikianza kupata afueni kutokana na Covid, ghafla inaingia vita ya Russia VS Ukraine na mataifa makubwa ya magharibi yanaungana pamoja kuiwekea vikwazo Urusi. Tofauti na mataifa mengine yanayowekewa vikwazo, Urusi ni namba mbili kwa uzalishaji wa nishati duniani huku mteja wake mkubwa akiwa bara Ulaya.

Mfumuko wa bei Marekani umefika 7.9 kikiwa kiwango cha juu kwa miaka 40 sasa huku vita na vikwazo vyake vikiwa havina dalili ya kupoa. Tanzania ni mtegemezi mkubwa wa mafuta katika uchumi wake hasa sekta ya usafirishaji ambayo ina mchango mkubwa katika mabadiliko ya bei.

Angalau kwenye nishati ya umeme utegemezi wa gesi ya kusini mwa nchi unapunguza haya maumivu. China kaamua kufunga mkataba mpya wa nishati na Saudi Arabia kuyakabili yajayo.

Kama Taifa tumejiaandaje na yajayo yanayoonekana hayafurahishi kama suluhu isipopatika mapema Ukraine.
marekani anajipiga makonzi mwenyewe.
 
Back
Top Bottom